Ufunuo 14 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ufunuo 14:1-20

Mwana-Kondoo Na Wale 144,000

114:1 Ufu 5:6; Za 2:6; Ufu 7:4; 3:12Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao. 214:2 Ufu 1:15; 5:8-9; Eze 1:24; 43:2Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. 314:3 Ufu 5:9; 4:6; 4:4; 14:1Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani. 414:4 2Kor 11:2; Ufu 3:4; Yak 1:18Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 514:5 Yn 1:47; Efe 5:27Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.

Malaika Watatu

614:6 Ufu 8:13; 19:17; 3:10; 13:7Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. 714:7 Za 34:9; Ufu 15:4; 11:13; 8:10Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”

814:8 Isa 21:9; Ufu 17:2-4; 18:3Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”

914:9 Ufu 13:14Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake, 1014:10 Isa 51:17; Yer 25:15; 51:7yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 1114:11 Isa 34:10; Ufu 19:3Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” 1214:12 Ufu 13:10; 1Kor 15:18; 1The 4:16; 1Kor 15:18; 1The 4:16Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.

1314:13 1Kor 15:18; 1The 4:16; Ufu 2:7; 22:17Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.”

“Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”

Kuvuna Mavuno Ya Dunia

1414:14 Dan 7:13; Ufu 1:13; 6:2Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. 1514:15 Yoe 3:13; Mk 4:29; Yer 51:33Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.” 16Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.

1714:17 Ufu 14:15Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali. 1814:18 Ufu 6:9; 8:5; 16:7; 14:15Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.” 1914:19 Ufu 19:15Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu. 2014:20 Yoe 3:13; Ebr 13:12; Ufu 11:8Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi,14:20 Kimo cha hatamu za farasi ni kama mita moja na nusu. kwa umbali wa maili 200.14:20 Maili 200 ni sawa na kilomita 320.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

啟示錄 14:1-20

天上的新歌

1我又觀看,見羔羊站在錫安山上,與祂在一起的有十四萬四千人,他們額上都有祂和祂父的名字。 2我聽見有聲音從天上傳來,像江海澎湃,像雷霆轟鳴,又像琴師彈奏豎琴的聲音。 3他們在寶座前,在四個活物和眾長老面前唱一首新歌。除了從地上被贖出來的十四萬四千人以外,沒有人能學得會這歌。 4這些人從未沾染過婦女,都是童身。無論羔羊往哪裡去,他們都緊隨其後。他們是從世人中被贖出來的,作為初熟的果實獻給上帝和羔羊。 5他們從未說謊,純潔無瑕。

三位天使的信息

6我看見另一位天使在空中飛翔,要將永遠的福音傳給地上的各國家、各部落、各語言族群、各民族。 7他大聲說:「要敬畏上帝,歸榮耀給祂,因為祂審判的時候到了。要敬拜造天地、海洋和一切水源的上帝。」

8接著又一位天使說:「巴比倫大城倒塌了!倒塌了!她曾使萬民喝她淫亂的烈酒。」14·8 以賽亞書21·9

9之後,第三位天使高喊:「一切敬拜怪獸和獸像、在手或額上接受獸印的, 10都要喝上帝烈怒調製的酒,就是祂怒杯裡毫無摻雜的烈酒。他們要在聖天使和羔羊面前,在火和硫磺中受煎熬。 11他們受煎熬所冒的煙不斷上騰,永無休止。那些拜獸、獸像和接受了獸名印記的人晝夜不得安寧。」 12因此,持守上帝命令和耶穌真道的聖徒需要堅忍。

13我聽見天上有聲音說:「你將下面的話寫下來,從今以後,那些為主而死的人有福了!」

聖靈說:「是的!他們將得享安息,不再勞苦。他們工作的成果必隨著他們。」

地上的收割

14我又觀看,見有一朵白雲,上面坐著的好像是人子,14·14 但以理書7·13祂頭戴金冠,手拿鋒利的鐮刀。 15有一位天使從殿中出來,揚聲向坐在雲上的那位說:「揮動你的鐮刀收割吧!地上的莊稼已經熟透了,可以收割了。」 16於是,坐在雲上的那位便向大地揮動鐮刀,把地上的莊稼都收割了。

17另一位天使手裡也拿著鋒利的鐮刀從天上的殿中出來。 18又有一位掌管火的天使從祭壇那裡出來,對手拿鐮刀的天使高喊:「揮動你鋒利的鐮刀,收取地上葡萄樹的果實吧!它們已經熟透了。」 19於是,那天使揮動鐮刀,收取了地上的葡萄,拋到上帝烈怒的大榨酒池中。 20葡萄在城外的榨酒池中被踩踏,血從榨酒池中湧出,高至馬的嚼環,流了三百公里14·20 「三百公里」希臘文是「一千六百司他町」。遠。