Ufunuo 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ufunuo 15:1-8

Malaika Saba Na Mapigo Saba

115:1 Ufu 12:1-3; 17:1; 21:9; Law 26:21Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika. 215:2 Ufu 4:6; 13:14Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu. 315:3 Kut 15:1; Kum 32:4; Za 111:2; 145:17Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema:

Bwana Mungu Mwenyezi,

matendo yako ni makuu na ya ajabu.

Njia zako wewe ni za haki na za kweli,

Mfalme wa nyakati zote!

415:4 Yer 10:7; Isa 66:23Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana

na kulitukuza jina lako?

Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu.

Mataifa yote yatakuja

na kuabudu mbele zako,

kwa kuwa matendo yako ya haki

yamedhihirishwa.”

515:5 Ufu 11:19; Hes 1:50Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni. 615:6 Ufu 14:15; 1:13Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao. 715:7 Ufu 4:6Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. 815:8 Isa 6:4; 1Fal 8:10-11; 2Nya 5:13-14Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

啟示錄 15:1-8

摩西的歌和羔羊的歌

1我看見天上又有一個宏大奇異的景象,有七位天使掌管著最後的七種災禍,上帝要藉這些災禍發盡祂的烈怒。 2我看見一個好像夾雜著火的玻璃海,玻璃海上站著那些戰勝怪獸、獸像及獸名代號的人。他們手裡拿著上帝所賜的豎琴, 3口裡唱著上帝的奴僕摩西的歌和羔羊的歌:

「全能的主上帝啊,

你的作為偉大奇妙!

萬國的王啊,

你的道路公義真實!

4主啊,誰敢不敬畏你,

不歸榮耀給你的名呢?

因為只有你是聖潔的,

萬民都必到你面前敬拜你,

因為你公義的作為已經彰顯出來了。」

天使降七災

5此後,我看見天上的聖殿,就是存放約櫃的聖幕打開了。 6那掌管七種災禍的七位天使都從殿中出來,身穿潔白發光的細麻布衣服,胸束金帶。 7四個活物中的一個將七隻金碗分別交給七位天使,碗中盛滿了永活上帝的烈怒。 8殿裡彌漫著上帝的榮耀和權能散發的煙霧,人們必須等到七位天使將七樣災禍降完,才能進入聖殿。