Zekaria 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Zekaria 8:1-23

Bwana Anaahidi Kuibariki Yerusalemu

1Neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia tena. 28:2 Yoe 2:18; Nah 1:2Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nina wivu sana kwa ajili ya Sayuni, ninawaka wivu kwa ajili yake.”

38:3 Zek 1:16; Isa 1:26; 48:1; 52:8; Yoe 3:21; Zek 2:10; Za 15:2; Yer 33:16; Mik 4:1; Za 48:1-2; Yer 31:23Hili ndilo asemalo Bwana: “Nitarudi Sayuni na kufanya makao Yerusalemu. Kisha Yerusalemu utaitwa mji wa kweli, mlima wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utaitwa Mlima Mtakatifu.”

48:4 Isa 65:20; 1Sam 2:31Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kwa mara nyingine tena wazee wanaume kwa wanawake walioshiba umri wataketi katika barabara za Yerusalemu, kila mmoja akiwa na mkongojo wake mkononi kwa sababu ya umri wake. 58:5 Yer 30:20; 31:13Barabara za mji zitajaa wavulana na wasichana wanaocheza humo.”

68:6 Za 118:23; 126:1-3; Yer 32:17, 27; Hes 11:23; Ay 42:2; Lk 1:37; Rum 4:21Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Mambo haya yanaweza kuonekana ya ajabu kwa mabaki ya watu wakati huo, lakini yaweza kuwa ya ajabu kwangu?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

78:7 Za 107:3; Isa 11:11; 43:5Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitawaokoa watu wangu kutoka nchi za mashariki na magharibi. 88:8 Eze 11:19-20; 36:28; 37:12; Zek 2:11; 10:10; Yer 11:4; 31:24; Isa 51:16; Ebr 8:10; Law 25:17; Yer 4:2; Zek 4:2; 13:9; Ufu 21:3Nitawarudisha waje kuishi Yerusalemu, watakuwa watu wangu nami nitakuwa mwaminifu na wa haki kwao kama Mungu wao.”

98:9 Ezr 5:1; 3:11; Hag 2:4Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Ninyi ambao sasa mnasikia maneno haya yanayozungumzwa na manabii ambao walikuwepo wakati wa kuwekwa kwa msingi wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, mikono yenu na iwe na nguvu ili Hekalu liweze kujengwa. 108:10 Isa 5:10; Hag 1:6; 2Nya 15:5Kabla ya wakati huo, hapakuwepo na ujira kwa mtu wala mnyama. Hakuna mtu aliyeweza kufanya shughuli yake kwa usalama kwa sababu ya adui yake, kwa kuwa nilikuwa nimemfanya kila mtu adui wa jirani yake. 118:11 Isa 12:1Lakini sasa sitawatendea mabaki ya watu hawa kama nilivyowatenda zamani,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

128:12 Za 65:13; 85:12; Yoe 2:22; Za 67:6; Mwa 27:28; Isa 60:21; Hos 2:21; Oba 1:17; Isa 61:7; Mt 6:33; 1Tim 4:8“Mbegu itakua vizuri, mzabibu utazaa matunda yake, ardhi itatoa mazao yake, na mbingu zitadondosha umande wake. Vitu hivi vyote nitawapa mabaki ya watu kama urithi wao. 138:13 Hes 5:27; Kum 13:15; Yer 42:18; Za 102:8; 48:8; Mwa 12:2; Yoe 2:14; Hag 2:5; Efe 6:10Jinsi mlivyokuwa kitu cha laana katikati ya mataifa, ee Yuda na Israeli, ndivyo nitakavyowaokoa, nanyi mtakuwa baraka. Msiogope, bali iacheni mikono yenu iwe na nguvu.”

148:14 Eze 24:14; Yer 31:28; 2Nya 36:16Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kama nilivyokuwa nimekusudia kuleta maangamizi juu yenu, wakati baba zenu waliponikasirisha na sikuonyesha huruma,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, 158:15 Yer 29:11; 31:28; 32:42; Mik 7:18-20“hivyo sasa nimeazimia kufanya mema tena kwa Yerusalemu na Yuda. Msiogope. 168:16 Za 15:2; Yer 33:16; Eze 18:8; 45:9; Amo 5:15; Zek 7:9; Efe 4:25; Mit 12:19Haya ndiyo mtakayoyafanya: Semeni kweli kila mtu kwa mwenzake, na mtoe hukumu ya kweli na haki kwenye mahakama zenu, 178:17 Mit 3:29; 6:16-19; Yer 7:9; Zek 5:4usipange mabaya dhidi ya jirani yako, wala msipende kuapa kwa uongo. Nayachukia yote haya,” asema Bwana.

18Neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia tena. 198:19 2Fal 25:7, 25; Yer 39:2; 52:4, 12; Za 30:11; Yer 41:1; Isa 35:10Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Saumu za miezi ya nne, tano, saba na kumi itakuwa sikukuu za furaha na za shangwe kwa Yuda. Kwa hiyo uipende kweli na amani.”

20Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Mataifa mengi na wakazi wa miji mingi watakuja, 218:21 Zek 7:2; Yer 26:19na wenyeji wa mji mmoja watakwenda kwenye mji mwingine na kusema, ‘Twende mara moja na tukamsihi Bwana, na kumtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote. Mimi mwenyewe ninakwenda.’ 228:22 Za 86:9; 117:1; Isa 2:2-3; 44:5; 45:14; 49:6; Zek 2:11Pia watu wa kabila nyingi na mataifa yenye nguvu yatakuja Yerusalemu kumtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote na kumsihi.”

238:23 Za 102:22; Isa 13:1; 14:1; 45:14; 56:3; 1Kor 14:25; Yer 23:33Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Katika siku hizo watu kumi kutoka lugha zote na mataifa, watangʼangʼania upindo wa joho la Myahudi mmoja na kusema, ‘Twende pamoja nawe kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nawe.’ ”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

撒迦利亚书 8:1-23

对耶路撒冷的应许

1万军之耶和华的话传给了我,说: 2“万军之耶和华说,‘我笃爱锡安,我为锡安而大发烈怒。 3我要回到锡安,住在耶路撒冷耶路撒冷必被称为忠信之城,万军之耶和华的山必被称为圣山。这是耶和华说的。 4必再次有年纪老迈、手拿拐杖的男女坐在耶路撒冷的街上。这是万军之耶和华说的。 5街上必到处都是玩耍的男女孩童。’ 6万军之耶和华说,‘那时,这事在这些余民看来是稀奇的,但在我看来毫不稀奇。这是万军之耶和华说的。’ 7万军之耶和华说,‘看啊,我要从日出之地和日落之处救出我的子民, 8带他们回到耶路撒冷居住。本着信实和公义,他们要做我的子民,我要做他们的上帝。’

9“万军之耶和华说,‘在奠立万军之耶和华殿的根基那天,众先知都在场。现今听见这些先知之言的人啊,你们要刚强,以便建造圣殿! 10那日之前,人和牲畜都得不到工钱。在敌人的威胁下,人们出入没有平安。因为我使众人彼此为敌。 11如今我不会像从前那样对待这些余民了。这是万军之耶和华说的。 12因为他们必平安地撒种,葡萄树必结果子,土地必出产五谷,天必降下甘霖,我必把这些福气赐给这些余民。 13犹大家和以色列家啊,从前你们在列国中是受咒诅的,现在我要拯救你们,使你们成为蒙福的人。你们不要害怕,要刚强。’

14“万军之耶和华说,‘从前你们的祖先惹我发怒,我决定毫不留情地降祸给他们。这是万军之耶和华说的。 15现在我决定赐福给耶路撒冷犹大家。你们不要害怕。 16你们所当做的是:彼此说真话,在城门口秉公断案,使人和睦。 17不可设阴谋彼此相害,不可贪爱假誓,因为这些都是我所憎恶的。这是耶和华说的。’”

18万军之耶和华的话传给了我,说: 19“万军之耶和华说,‘四月、五月、七月、十月的禁食必成为犹大家欢喜快乐的日子和幸福的节期。因此,你们要喜爱真理与和平。 20各族的人和各城的居民都必来这里。这是万军之耶和华说的。 21这一城的居民必到那一城,说,我们快去向耶和华求恩,去寻求万军之耶和华吧!我自己也去。 22许多民族和强国必来耶路撒冷寻求万军之耶和华,向耶和华求恩。 23那时,十个来自列国、讲不同语言的人必拉住一个犹大人的衣角,说,让我们跟你们同去吧,因为我们听说上帝与你们同在。这是万军之耶和华说的。’”