Yeremia 51 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 51:1-64

151:1 Isa 41:16; Mt 3:12; Yer 50:14; Isa 13:5-951:1 Yer 46:4; Isa 41:25; Yer 50:28, 45; Isa 13:3; Yer 50:9; Isa 21:5; 41:2Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.51:1 Leb-Kamai ni Ukaldayo, yaani Babeli, kwa fumbo.

2Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

351:3 Yer 50:29; 46:4Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

451:4 Isa 13:15-18; Yer 50:30Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.

551:5 Law 26:44; Isa 54:6-8; Za 91:14; Hos 4:1Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

651:6 Ufu 18:4; Isa 48:20; Yer 50:8, 15; Ay 21:19; Isa 1:24; Mao 3:64; Hes 16:26“Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi cha Bwana,

atamlipa kile anachostahili.

751:7 Isa 51:22; Ufu 17:4; Yer 25:15-16; 49:12; Ufu 14:8-10Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

851:8 Isa 14:15; Ufu 14:8; Yer 8:22; Ufu 18:9; Yer 46:11; Isa 21:9Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

951:9 Isa 13:14; 31:9; Ufu 18:4-5; Yer 50:16“ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu hadi mawinguni.’

1051:10 Mik 7:8-9; Za 64:9; Yer 50:28“ ‘Bwana amethibitisha haki yetu;

njooni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’

11“Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwana atalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

1251:12 Za 20:5; 2Sam 18:24; Eze 33:2Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwana atatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

1351:13 Yer 50:38; Ufu 17:15; Eze 22:27; Hab 2:9; Isa 45:3Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

1451:14 Mwa 22:16; Amo 6:8; Nah 3:15; Yer 50:15Bwana Mwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

1551:15 Ay 9:8; Isa 40:26; Mdo 14:15; Za 104:24; 136:5“Aliiumba dunia kwa uweza wake;

akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

1651:16 Za 18:11-13; Kum 28:12; Yn 1:12; Ay 28:26; Za 135:7Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua,

naye huuleta upepo kutoka ghala zake.

1751:17 Isa 44:20; Hab 2:18-19; Yer 50:2“Kila mtu ni mjinga na hana maarifa;

kila sonara ameaibishwa na sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yavyo.

1851:18 Yer 18; 15; Yn 2:8Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.

1951:19 Za 119:57; Kut 34:9Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwani ndiye Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

2051:20 Isa 10:5; Zek 9:13; Mik 4:13; Ay 34:24; Isa 45:1“Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita:

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

2151:21 Kut 15:1; Isa 43:17; Yer 50:37kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

2251:22 2Nya 36:17; Isa 13:17-18kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

2451:24 Kum 32:41; Mao 3:64; Yer 50:15; Isa 45:1“Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.

2551:25 Yer 21:13; 50:23; Kut 3:20; Zek 4:7“Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asema Bwana.

“Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

2651:26 Isa 13:19-22; Yer 50:12Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asema Bwana.

2751:27 Isa 13:2; Za 20:5; Mwa 8:4; 10:3; Yer 25:14“Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

2951:29 Isa 13:20; Yer 50:13; Amu 5:4; Yer 49:21; Za 33:11; Yer 48:9Nchi inatetemeka na kugaagaa,

kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.

3051:30 Yer 50:24; 2Sam 19:16; Mao 2:9; Nah 3:13; Isa 47:14; 45:2Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

3151:31 Yer 50:24; 2Sam 18:19-31; Dan 5:30Tarishi mmoja humfuata mwingine,

na mjumbe humfuata mjumbe,

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

3251:32 Isa 47:14; Yer 50:36Vivuko vya mito vimekamatwa,

mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

3351:33 Isa 21:10; 17:5; Hos 6:11; Mt 13:30; Isa 13:22Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

3451:34 Yer 50:17; Nah 2:12; Hos 8:8“Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35Jeuri iliyofanyiwa miili yetu51:35 Au: Jeuri tuliyofanyiwa sisi na watoto wetu. na iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

3651:36 Za 140:12; Mao 3:58; Yer 20:12; Rum 12:19; Hos 13:15; Yer 50:34; Isa 11:15Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

3751:37 Isa 13:22; Ufu 12:8; Yer 50:39; 18:16; Ufu 18:2; Nah 3:6; Mal 2:9Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

3951:39 Isa 21:5; Yer 50:24; Za 13:3Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asema Bwana.

40“Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

4151:41 Yer 25:26; Isa 13:19; Dan 4:30; Yer 50:13“Tazama jinsi Sheshaki51:41 Sheshaki ni Babeli kwa fumbo. atakamatwa,

majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

4251:42 Za 18:4; Isa 8:7-8Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

4351:43 Isa 13:20; Yer 2:6; Isa 21:1Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

4451:44 Isa 21:9; 2Fal 25:4; Isa 25:12; 46:1; Yer 50:15Nitamwadhibu Beli katika Babeli,

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

4551:45 Ufu 18:4; Yer 50:8; Isa 48:20; Za 76:10; 79:6“Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali ya Bwana.

4651:46 Yer 46:27; 2Fal 19:7; Za 18:45Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi,

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

4751:47 Isa 46:1-2; Yer 50:12; 27:7; 50:12Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu,

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

4851:48 Isa 44:23; Ufu 18:20; Yer 25:26; Isa 41:25; Za 149:2; Ay 3:7Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asema Bwana.

4951:49 Za 137:8; Yer 50:29“Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

5151:51 Za 44:13-16; 79:4; Mao 1:10“Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”

5251:52 Ay 24:12“Lakini siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

5351:53 Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Ay 15:21; Yer 49:16Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asema Bwana.

54“Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

5551:55 Za 18:4; Isa 25:5Bwana ataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

5651:56 Ay 15:21; Mwa 4:24; Za 46:9; Hab 2:8; Za 94:1-2Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

5751:57 Za 76:5; Yer 25:27; Isa 6:5; Yer 46:18; Ay 5:13; Isa 21:7Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.

5851:58 2Fal 25:4; Isa 15:4; 47:14; Hab 2:13; Isa 13:2Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”

5951:59 Yer 36:4; 52:1; 28:1Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 6051:60 Kut 17:14; Yer 30:2; 36:2Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli. 61Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa. 6251:62 Isa 13:20; Yer 9:11; 50:13Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’ 6351:63 Mwa 2:14Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati. 6451:64 Ay 31:40; Za 18:21; Eze 26:21; 28:19Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

New Russian Translation

Иеремия 51:1-64

1Так говорит Господь:

«Я поднимаю губительный вихрь51:1 Или: «Я возбуждаю дух губителя…»

на Вавилон и жителей Лев-Камая51:1 Лев-Камай. Криптограмма названия Халдея..

2Я пошлю в Вавилон чужеземцев,

они развеют его и разграбят его землю,

обступят его со всех сторон

в день бедствий.

3Не давайте лучнику натянуть лук,

не давайте надеть кольчугу.

Не щадите юношей Вавилона,

полностью истребите51:3 См. Исх. 22:20 и сноску к нему. его войско.

4Падут они мертвыми на земле халдейской,

смертельно пронзенными на его улицах».

5Ведь Израиль с Иудеей не покинуты

их Богом, Господом Сил,

хотя их земля51:5 Или: а земля вавилонян. и полна вины

перед Святым Израиля.

6Бегите из Вавилона!

Спасайтесь бегством,

чтобы не погибнуть за его грехи!

Настало время Господней мести;

Он воздаст Вавилону по заслугам.

7Вавилон был золотым кубком в руке Господа;

он напоил всю землю.

Народы пили его вино,

и вот они безумствуют.

8Вавилон внезапно падет и погибнет.

Рыдайте о нем!

Принесите бальзам для его ран,

может быть, он исцелится.

9«Мы лечили Вавилон,

но нет ему исцеления.

Оставим его, и пусть каждый идет в свою землю,

так как его кара достигла небес,

поднялась до облаков».

10«Господь оправдал нас!

Пойдем и поведаем на Сионе

о делах Господа, нашего Бога».

11Точите стрелы,

готовьте щиты!

Господь распалил царей Мидии,

потому что решил погубить Вавилон.

Это Господне возмездие!

Это возмездие за Его храм!

12Поднимите боевое знамя против стен Вавилона!

Усильте охрану,

расставьте дозорных,

устройте засаду!

Что Господь задумал, то Он и сделает,

что Он сказал о жителях Вавилона, то и исполнит.

13Ты живешь у великих вод,

богат сокровищами,

но твоя гибель близка,

нить твоей жизни отрезана.

14Клянется Собой Господь Сил:

«Непременно наполню тебя войсками, Вавилон,

как пожирающей саранчой,

и они поднимут против тебя победный клич».

15Он создал землю Своим могуществом,

утвердил мир Своей мудростью,

распростер небеса Своим разумом.

16Когда Он возвышает голос, шумят небесные воды;

Он поднимает тучи с края земли.

Он посылает молнии среди ливня

и выводит ветер из Своих кладовых.

17Все люди глупы и нет у них знания;

всякий плавильщик позорит себя своими идолами.

Его изваяния лживы,

и нет в них дыхания.

18Они ничтожны и смешны;

пробьет их час, и они погибнут.

19Но Он, Удел Иакова, не таков, как они,

потому что Он — Творец всего,

и Израиль — народ Его наследия;

Господь Сил — вот Его имя.

20«Ты, Вавилон, — Моя булава,

оружие для сражений;

тобой Я сокрушу народы,

тобой Я погублю царства,

21тобой Я сокрушу и коня, и всадника,

тобой Я сокрушу и колесницу, и возничего;

22тобой Я сокрушу и мужчин, и женщин,

тобой Я сокрушу и стариков, и юных,

тобой Я сокрушу и юношей, и девушек;

23тобой Я сокрушу и пастуха, и стадо,

тобой Я сокрушу и пахаря, и волов,

тобой Я сокрушу и наместников, и военачальников.

24На ваших глазах Я воздам Вавилону и всем, кто живет в землях халдеев, за всё то зло, какое они причинили Сиону», — возвещает Господь.

25«Я против тебя, гора погибели,

губящая всю землю», —

возвещает Господь.

«Я простру на тебя Свою руку

и низвергну тебя со скал;

Я сделаю тебя обгорелой горой.

26Не возьмут из тебя ни камня на угол,

ни камня на фундамент;

ты будешь пребывать в вечном запустении», —

возвещает Господь.

27«Поднимите боевое знамя над страной!

Трубите в рог среди народов!

Подготовьте народы к войне с Вавилоном;

созовите эти царства, чтобы восстать против него:

Арарат и Минни с Ашкеназом.

Поставьте военачальника против него;

пошлите конницу, как стаю саранчи.

28Приготовьте народы к войне с Вавилоном:

царей Мидии,

их наместников, их военачальников

и все подвластные им края.

29Земля содрогается и трепещет;

сбываются замыслы Господа о Вавилоне —

превратить вавилонский край в пустыню,

где никто не будет жить.

30Перестали сражаться вавилонские воины

и сидят в своих крепостях.

Они истощены,

стали трусливы, как женщины.

Дома Вавилона сожжены,

засовы его ворот сломаны.

31Гонец сменяет гонца,

и вестник идет за вестником,

чтобы возвестить царю Вавилона,

что весь его город взят,

32что броды уже захвачены,

что укрепления горят

и воины в ужасе».

33Так говорит Господь Сил, Бог Израиля:

«Дочь Вавилона подобна гумну,

когда люди обмолачивают на нем зерно;

скоро настанет время ее жатвы».

34«Навуходоносор, царь Вавилона пожирал нас,

привел нас в замешательство,

сделал нас пустым кувшином.

Он глотал нас, как морское чудовище;

набивал свой живот нашими сластями,

но потом извергнул нас.

35Пусть воздастся Вавилону за жестокость против нас51:35 Или: против нас и наших детей.», —

скажут жители Сиона.

«Пусть воздастся за нашу кровь

живущим в стране халдеев», —

скажут жители Иерусалима.

36Поэтому так говорит Господь:

«Я заступлюсь за вас

и отомщу за вас.

Я осушу вавилонские реки

и иссушу его источники.

37Вавилон станет грудой развалин,

логовом шакалов,

ужасом и посмешищем,

необитаемой землей.

38Заревут его жители вместе, как львы,

зарычат, словно львята.

39Когда они разгорячатся

Я устрою им пир и напою их,

чтобы они развеселились

и потом уснули вечным сном, и не проснулись больше», —

возвещает Господь.

40«Сведу их,

как ягнят, на убой,

как баранов с козлами.

41О, как будет взят Шешах51:41 Шешах. Криптограмма названия Вавилон.,

захвачена слава всей земли!

Каким ужасом явится Вавилон

среди народов!

42Море поднимется над Вавилоном,

и ревущие волны покроют его.

43Его города станут пустынями,

иссохшей и безлюдной землей,

землей, где никто не живет,

по которой никто не ходит.

44Я накажу Бела51:44 См. 50:2. в Вавилоне

и заставлю его извергнуть проглоченное.

Не будут больше стекаться к нему народы,

и падут вавилонские стены.

45Выходи, Мой народ, из Вавилона!

Спасайся бегством от пылающего гнева Господня!

46Не падай духом,

не бойся слухов,

что ходят в стране;

в этом году — один слух,

в следующем — другой;

слухи о зверствах в стране,

о ссорах правителей.

47Ведь непременно настанут дни,

когда Я накажу идолов Вавилона.

Вся его земля будет опозорена,

и падут там все пораженными.

48А небо, земля и всё, что на ней,

будут кричать от радости,

потому что разорители Вавилона явятся с севера», —

возвещает Господь.

49«Падет Вавилон,

потому что убивал израильтян

и другие народы по всей земле.

50Уцелевшие от меча,

уходите, не мешкайте!

Помните Господа в дальнем краю

и думайте об Иерусалиме».

51«Мы устыдились,

когда услышали оскорбления,

и позор покрыл наши лица,

когда чужеземцы вошли

в святыни дома Господа».

52«Но наступают дни, — возвещает Господь, —

когда Я накажу идолов Вавилона,

и по всей его земле застонут раненые.

53Даже если поднимется Вавилон до небес

и укрепит свои высокие крепости,

Я пошлю на него разорителей», —

возвещает Господь.

54«Звук вопля донесется из Вавилона,

звук великого разрушения — из земли халдеев.

55Погубит Господь Вавилон

и заставит его великий шум умолкнуть.

Враги его заревут, как волны могучих вод,

разнесется шум их голосов.

56Опустошитель придет в Вавилон;

его воины будут захвачены,

их луки будут сломаны.

Ведь Господь — это Бог воздаяния,

Он воздает сполна.

57Я напою его вождей и мудрецов,

наместников, начальников и воинов,

и они уснут вечным сном и не проснутся больше», —

возвещает Царь, Чье имя Господь Сил.

58Так говорит Господь Сил:

«Толстые стены Вавилона сравняют с землей,

а высокие ворота сожгут дотла.

Народы изнуряют себя напрасно,

их труды — лишь пища для огня».

59Вот послание, которое пророк Иеремия вручил главному служащему Серае, сыну Нирии, сыну Махсеи, когда тот уходил в Вавилон с Цедекией, царем Иудеи, в четвертом году его правления51:59 В 593 г. до н. э.. 60Иеремия записал в свиток все бедствия, которым суждено было случиться с Вавилоном — всё, что было записано о Вавилоне. 61Он сказал Серае:

— Когда придешь в Вавилон, прочитай все эти слова вслух 62и скажи: «Господь! Ты сказал, что погубишь этот край, чтобы не жили здесь ни человек, ни животное, чтобы эта земля лежала в вечном запустении». 63Дочитав свиток, привяжи к нему камень и брось в реку Евфрат. 64И скажи: «Так потонет Вавилон, и он не поднимется больше из-за бедствий, которые Я нашлю на него. И все его жители погибнут».

Здесь заканчиваются слова Иеремии.