Yeremia 51 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 51:1-64

151:1 Isa 41:16; Mt 3:12; Yer 50:14; Isa 13:5-951:1 Yer 46:4; Isa 41:25; Yer 50:28, 45; Isa 13:3; Yer 50:9; Isa 21:5; 41:2Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.51:1 Leb-Kamai ni Ukaldayo, yaani Babeli, kwa fumbo.

2Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

351:3 Yer 50:29; 46:4Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

451:4 Isa 13:15-18; Yer 50:30Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.

551:5 Law 26:44; Isa 54:6-8; Za 91:14; Hos 4:1Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

651:6 Ufu 18:4; Isa 48:20; Yer 50:8, 15; Ay 21:19; Isa 1:24; Mao 3:64; Hes 16:26“Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi cha Bwana,

atamlipa kile anachostahili.

751:7 Isa 51:22; Ufu 17:4; Yer 25:15-16; 49:12; Ufu 14:8-10Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

851:8 Isa 14:15; Ufu 14:8; Yer 8:22; Ufu 18:9; Yer 46:11; Isa 21:9Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

951:9 Isa 13:14; 31:9; Ufu 18:4-5; Yer 50:16“ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu hadi mawinguni.’

1051:10 Mik 7:8-9; Za 64:9; Yer 50:28“ ‘Bwana amethibitisha haki yetu;

njooni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’

11“Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwana atalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

1251:12 Za 20:5; 2Sam 18:24; Eze 33:2Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwana atatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

1351:13 Yer 50:38; Ufu 17:15; Eze 22:27; Hab 2:9; Isa 45:3Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

1451:14 Mwa 22:16; Amo 6:8; Nah 3:15; Yer 50:15Bwana Mwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

1551:15 Ay 9:8; Isa 40:26; Mdo 14:15; Za 104:24; 136:5“Aliiumba dunia kwa uweza wake;

akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

1651:16 Za 18:11-13; Kum 28:12; Yn 1:12; Ay 28:26; Za 135:7Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua,

naye huuleta upepo kutoka ghala zake.

1751:17 Isa 44:20; Hab 2:18-19; Yer 50:2“Kila mtu ni mjinga na hana maarifa;

kila sonara ameaibishwa na sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yavyo.

1851:18 Yer 18; 15; Yn 2:8Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.

1951:19 Za 119:57; Kut 34:9Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwani ndiye Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

2051:20 Isa 10:5; Zek 9:13; Mik 4:13; Ay 34:24; Isa 45:1“Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita:

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

2151:21 Kut 15:1; Isa 43:17; Yer 50:37kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

2251:22 2Nya 36:17; Isa 13:17-18kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

2451:24 Kum 32:41; Mao 3:64; Yer 50:15; Isa 45:1“Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.

2551:25 Yer 21:13; 50:23; Kut 3:20; Zek 4:7“Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asema Bwana.

“Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

2651:26 Isa 13:19-22; Yer 50:12Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asema Bwana.

2751:27 Isa 13:2; Za 20:5; Mwa 8:4; 10:3; Yer 25:14“Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

2951:29 Isa 13:20; Yer 50:13; Amu 5:4; Yer 49:21; Za 33:11; Yer 48:9Nchi inatetemeka na kugaagaa,

kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.

3051:30 Yer 50:24; 2Sam 19:16; Mao 2:9; Nah 3:13; Isa 47:14; 45:2Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

3151:31 Yer 50:24; 2Sam 18:19-31; Dan 5:30Tarishi mmoja humfuata mwingine,

na mjumbe humfuata mjumbe,

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

3251:32 Isa 47:14; Yer 50:36Vivuko vya mito vimekamatwa,

mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

3351:33 Isa 21:10; 17:5; Hos 6:11; Mt 13:30; Isa 13:22Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

3451:34 Yer 50:17; Nah 2:12; Hos 8:8“Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35Jeuri iliyofanyiwa miili yetu51:35 Au: Jeuri tuliyofanyiwa sisi na watoto wetu. na iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

3651:36 Za 140:12; Mao 3:58; Yer 20:12; Rum 12:19; Hos 13:15; Yer 50:34; Isa 11:15Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

3751:37 Isa 13:22; Ufu 12:8; Yer 50:39; 18:16; Ufu 18:2; Nah 3:6; Mal 2:9Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

3951:39 Isa 21:5; Yer 50:24; Za 13:3Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asema Bwana.

40“Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

4151:41 Yer 25:26; Isa 13:19; Dan 4:30; Yer 50:13“Tazama jinsi Sheshaki51:41 Sheshaki ni Babeli kwa fumbo. atakamatwa,

majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

4251:42 Za 18:4; Isa 8:7-8Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

4351:43 Isa 13:20; Yer 2:6; Isa 21:1Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

4451:44 Isa 21:9; 2Fal 25:4; Isa 25:12; 46:1; Yer 50:15Nitamwadhibu Beli katika Babeli,

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

4551:45 Ufu 18:4; Yer 50:8; Isa 48:20; Za 76:10; 79:6“Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali ya Bwana.

4651:46 Yer 46:27; 2Fal 19:7; Za 18:45Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi,

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

4751:47 Isa 46:1-2; Yer 50:12; 27:7; 50:12Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu,

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

4851:48 Isa 44:23; Ufu 18:20; Yer 25:26; Isa 41:25; Za 149:2; Ay 3:7Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asema Bwana.

4951:49 Za 137:8; Yer 50:29“Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

5151:51 Za 44:13-16; 79:4; Mao 1:10“Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”

5251:52 Ay 24:12“Lakini siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

5351:53 Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Ay 15:21; Yer 49:16Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asema Bwana.

54“Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

5551:55 Za 18:4; Isa 25:5Bwana ataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

5651:56 Ay 15:21; Mwa 4:24; Za 46:9; Hab 2:8; Za 94:1-2Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

5751:57 Za 76:5; Yer 25:27; Isa 6:5; Yer 46:18; Ay 5:13; Isa 21:7Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.

5851:58 2Fal 25:4; Isa 15:4; 47:14; Hab 2:13; Isa 13:2Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”

5951:59 Yer 36:4; 52:1; 28:1Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 6051:60 Kut 17:14; Yer 30:2; 36:2Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli. 61Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa. 6251:62 Isa 13:20; Yer 9:11; 50:13Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’ 6351:63 Mwa 2:14Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati. 6451:64 Ay 31:40; Za 18:21; Eze 26:21; 28:19Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

耶利米书 51:1-64

1耶和华说:

“看啊,我要使毁灭的暴风袭击巴比伦和住在立加米的人。

2毁灭巴比伦人的日子一到,

我要差遣外族人从四面八方攻击他们,

从地上消灭他们,如同狂风卷走碎秸。

3不要让他们的弓箭手有机会射箭,

不要让他们的战士有机会穿铠甲,

不要放过他们的青年,

要使他们全军覆没。

4他们将被杀死在自己的土地上,

横尸街头。

5虽然以色列犹大在他们的圣者面前充满罪恶,

但他们的上帝——万军之耶和华却没有撇弃他们。

6“离开巴比伦,各自逃命吧!

不要让她的罪恶连累你们,

以致你们灭亡,

因为这是耶和华报应她的时候,

耶和华要惩罚她。

7巴比伦在耶和华手中曾是灌醉天下的金杯,

列国喝了她的酒,都变得癫狂。

8转瞬之间,巴比伦必崩溃毁灭。

你们要为她哀悼,

拿药为她止痛,

或许可以治好她。

9寄居在巴比伦的人说,

‘我们试过了,却没有治好。

我们离开她,各自返回故乡吧!

因为她罪恶滔天,必受至高的审判。

10耶和华已为我们申冤。

来吧!我们要在锡安述说我们上帝耶和华的作为。’

11“要磨尖箭头,拿起盾牌!

耶和华已激起玛代诸王的敌意,

因为祂决意要毁灭巴比伦

祂要报仇,为祂的圣殿被毁报仇。

12要竖起旗帜,

攻打巴比伦的城墙;

要加强防卫,

派人巡逻,设下埋伏。

因为耶和华言出必行,

祂必按计划惩罚巴比伦人。

13住在河边、拥有许多财宝的巴比伦人啊,

你们的结局到了,

你们的末日来了。”

14万军之耶和华凭自己起誓说:

“我要使敌人如蝗虫一样铺天盖地而来,

占据你们的家园,

向你发出胜利的呐喊。”

15耶和华以大能创造大地,

以智慧建立世界,

以聪明铺展诸天。

16祂一声令下,天上便大水澎湃;

祂使云从地极升起,

使闪电在雨中划过,

使风从祂的仓库吹出。

17世人都愚昧无知,

金匠都因所造的偶像而羞愧,

因为神像是骗人的,

它们没有生命气息。

18它们毫无价值,荒唐可笑,

刑罚一到,必被毁灭。

19雅各的上帝51:19 “雅各的上帝”希伯来文是“雅各的产业”。截然不同,

因为祂是万物的创造者,

以色列子民是祂的产业,

万军之耶和华是祂的名字。

20巴比伦啊!你是我的锤子,

我作战的兵器,

我要用你打碎列国,

毁灭列邦。

21我要用你打碎战马和骑士,

打碎战车和车夫,

22打碎男人和妇女,

打碎老人和小孩,

打碎少男和少女,

23打碎牧人和牲畜,

打碎农夫和耕牛,

打碎省长和总督。”

24耶和华说:“我要当着我子民的面报应巴比伦51:24 “巴比伦人”希伯来文是“巴比伦和迦勒底人”。,因为他们在锡安犯罪作恶。

25“毁灭整个大地的山岳——巴比伦啊,

我与你为敌,

我要伸手攻击你,

把你从悬崖上滚下去,

使你化为灰烬。

这是耶和华说的。

26再无人用你的石头做房角石或基石,

你要永远荒凉。

这是耶和华说的。

27“要在大地上竖起旌旗,

在列国吹响号角,

让他们预备攻打巴比伦

要召集亚拉腊米尼

亚实基拿各国攻打她,

要派遣将领率多如蝗虫的骑兵攻打她。

28要让列国预备攻打巴比伦

要让玛代的诸王及其省长、总督和所统治的人预备攻打她。

29大地要颤抖,痛苦地扭动,

因为耶和华决意要攻击巴比伦

使她荒无人烟。

30巴比伦的勇士不再作战,

躲在堡垒里,

士气消沉,像妇女一样无力;

巴比伦的房屋被火焚烧,

城门被攻破。

31报信的人接踵而来,

巴比伦王禀告,

‘整座城已失守,

32渡口被占,

沼泽地被烧,

战士惊慌失措。’”

33以色列的上帝——万军之耶和华说:

巴比伦城要像麦场一样被踏为平地,

收割她的时节很快就要到了。”

34以色列人说:

巴比伦尼布甲尼撒吞噬我们、击垮我们,

把我们洗劫一空。

他像海怪一样吞吃我们,

饱餐我们的美物,

然后把我们赶走。”

35锡安的居民说:

巴比伦人残暴地对待我们和我们的亲人,

愿他们受报应。”

耶路撒冷人说:

“愿迦勒底人偿还我们的血债。”

36因此,耶和华说:

“看啊,我要为你们申冤,

替你们报仇;

我要使巴比伦的江河枯竭,

泉源干涸。

37巴比伦必沦为废墟,杳无人迹,

沦为豺狼出没的地方,

令人惊骇和嗤笑。

38迦勒底人像群狮一样怒吼,

又像幼狮一样咆哮。

39他们食欲大振时,

我要为他们设盛宴,

使他们酩酊大醉,狂欢乱叫,

长眠不醒。

这是耶和华说的。

40我要把他们像羊羔、

公绵羊和公山羊一样带往宰杀之地。

41巴比伦51:41 “巴比伦”希伯来文是“示沙克”,巴比伦的别名。怎么沦陷了!

天下引以为傲的怎么被攻占了!

巴比伦的下场让列国恐惧!

42海水涨溢,漫过巴比伦

汹涌的波涛淹没了她。

43她的城邑沦为废墟,

变成干旱的沙漠,

荒无人烟,杳无人迹。

44我要惩罚巴比伦的神明彼勒

使它吐出所吞噬的。

万国必不再涌向它,

巴比伦的城墙必倒塌。

45“我的子民啊,你们要离开巴比伦

各自逃命,躲避耶和华的烈怒。

46境内谣言四起时,

你们不要惊慌害怕,

因为今年传这风声,

明年却传那风声,

说境内必有暴乱,

官长要互相残杀。

47“看啊,时候将到,我必惩罚巴比伦的神像,

使巴比伦全国蒙羞,

尸横遍野。

48毁灭者要从北方前来攻击巴比伦

那时天地万物都要因巴比伦的灭亡而欢呼。

这是耶和华说的。

49巴比伦必因屠杀以色列人而倒毙,

正如各地因巴比伦屠杀而倒毙的人一样。

50“刀下逃生的人啊,

你们快走吧!

不要停留!

在远方要记住耶和华,

要追想耶路撒冷

51你们说外国人闯入耶和华殿的圣所,

使你们蒙羞受辱,满脸尽是耻辱。

52“看啊,时候将到,我要惩罚巴比伦的神像,

使巴比伦到处都是受伤者的呻吟。

这是耶和华说的。

53即使巴比伦城高耸入云,

堡垒坚不可摧,

我仍要差遣毁灭者攻击她。

这是耶和华说的。

54巴比伦传出哭喊声,

迦勒底人之地响起大毁灭的声音,

55因为耶和华正在毁灭巴比伦

要使城中的喧嚣变成一片死寂。

毁灭者如怒海狂涛一样涌来,

不断高声呐喊。

56毁灭者正前来攻打巴比伦

擒拿她的勇士,

折断他们的弓弩。

因为耶和华是追讨罪恶、

报应恶人的上帝。

57我要使她的首领、谋士、省长、

总督和勇士都酩酊大醉,

长眠不醒。”

这是名为万军之耶和华的君王说的。

58万军之耶和华说:

巴比伦宽阔的城墙要被夷为平地,

高大的城门要被付之一炬,

列邦一切的辛劳都是徒然,

列国劳碌的成果都化为灰烬。”

59-60耶利米先知把所有将要发生在巴比伦的灾祸,就是有关巴比伦的事都写在卷轴上。犹大西底迦执政第四年,玛西雅的孙子、尼利亚的儿子、宫廷总管西莱雅犹大王一同前往巴比伦的时候, 61耶利米西莱雅说:“你到巴比伦后务要大声宣读这卷轴上的一切话, 62并且要说,‘耶和华啊!你曾说要毁灭这地方,使这里人畜绝迹、永远荒凉。’ 63读完后,你要把卷轴绑在一块石头上,扔进幼发拉底河, 64然后说,‘耶和华降的灾祸必使巴比伦像这卷轴一样沉没、永不复兴,巴比伦人必灭亡。’”

耶利米的话到此为止。