Yeremia 46 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 46:1-28

Ujumbe Kuhusu Misri

146:1 Yer 25:15-38; 1:10Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:

246:2 2Fal 23:29; 2Nya 35:20; Mwa 2:14Kuhusu Misri:

Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:

346:3 Isa 21:5; Yer 51:11-12; Isa 8:9-10; Yoe 3:9-10“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo,

mtoke kwa ajili ya vita!

446:4 Eze 21:9-11; 2Nya 26:14; Neh 4:16; 1Sam 17:5, 38Fungieni farasi lijamu,

pandeni farasi!

Shikeni nafasi zenu

mkiwa mmevaa chapeo!

Isugueni mikuki yenu,

vaeni dirii vifuani!

546:5 Yer 48:44; Za 31:13; Yer 49:29; Ufu 6:15-17Je, ninaona nini?

Wametiwa hofu,

wanarudi nyuma,

askari wao wameshindwa.

Wanakimbia kwa haraka

pasipo kutazama nyuma,

tena kuna hofu kuu kila upande,”

asema Bwana.

646:6 Isa 30:16; Za 20:8; Dan 11:19; Mwa 2:14; 15:18Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia,

wala wenye nguvu hawawezi kutoroka.

Kaskazini, kando ya Mto Frati,

wanajikwaa na kuanguka.

746:7 Dan 11:22; Yer 47:2“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?

846:8 Dan 11:10; Eze 29:3, 9; 30:12; Amo 8:8Misri hujiinua kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi.

Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia,

nitaiangamiza miji na watu wake.’

946:9 Mwa 10:6; Yer 47:3; Isa 66:19; Eze 26:10Songeni mbele, enyi farasi!

Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi,

Endeleeni mbele, enyi mashujaa:

watu wa Kushi46:9 Kushi ni Naili ya Juu; sasa ni Sudan. na Putu46:9 Putu sasa ni Libya. wachukuao ngao,

watu wa Ludi46:9 Nchi iliyo Afrika ya Kaskazini, magharibi ya Mto Naili; sasa ni Libya. wavutao upinde.

1046:10 Eze 32:10; Mao 1:15; Hes 31:3; 2Fal 23:29-30; Law 3:9; Isa 34:6Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

siku ya kulipiza kisasi,

kisasi juu ya adui zake.

Upanga utakula hata utakapotosheka,

hadi utakapozima kiu yake kwa damu.

Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu

kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.

1146:11 Yer 8:22; Mwa 37:35; 2Fal 19:21; Isa 47:1; Yer 30:13“Panda hadi Gileadi ukapate zeri,

ee Bikira Binti wa Misri.

Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio;

huwezi kupona.

1246:12 Isa 19:4; Nah 3:8-10Mataifa yatasikia juu ya aibu yako,

kilio chako kitaijaza dunia.

Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine,

nao wataanguka chini pamoja.”

1346:13 Yer 43:10; Isa 19:1; Yer 27:7; Eze 32:11Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:

1446:14 Yer 43:8; Isa 19:13; 2Sam 2:26; Kum 32:42; Yer 24:8“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli,

hubiri pia katika Memfisi46:14 Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. na Tahpanhesi:46:14 Ni mji katika Misri.

‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari,

kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’

1546:15 Yos 23:5; Isa 66:15-16Kwa nini mashujaa wako wamesombwa

na kupelekwa mbali?

Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana

atawasukuma awaangushe chini.

1646:16 Law 26:37; Isa 13:14; Yer 25:38Watajikwaa mara kwa mara,

wataangukiana wao kwa wao.

Watasema, ‘Amka, turudi

kwa watu wetu na nchi yetu,

mbali na upanga wa mtesi.’

1746:17 Isa 19:11-16; 1Fal 20:10-11Huko watatangaza,

‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu,

amekosa wasaa wake.’

1846:18 Yer 48:15; Yos 19:22; 1Fal 18:42“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme,

ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima,

kama Karmeli kando ya bahari.

1946:19 Yer 48:18; Isa 20:4; 19:13; Eze 29:10-12; 35:7Funga mizigo yako kwenda uhamishoni,

wewe ukaaye Misri,

kwa kuwa Memfisi utaangamizwa

na kuwa magofu pasipo mkazi.

2046:20 Isa 14:31; Hos 10:11; Yer 47:2“Misri ni mtamba mzuri,

lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.

2146:21 2Fal 7:6; Ay 20:24; Za 18:18; Yer 18:17; Lk 15:27; Ay 18:20; Za 37:13Askari wake waliokodiwa katika safu zake

wako kama ndama walionenepeshwa.

Wao pia watageuka na kukimbia pamoja,

hawataweza kuhimili vita,

kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2246:22 Za 74:5Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia

kadiri adui anavyowasogelea na majeshi,

watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka,

kama watu wakatao miti.

2346:23 Isa 29:4; Amo 7:12; Za 74:5; Kum 28:42Wataufyeka msitu wake,”

asema Bwana,

“hata kama umesongamana kiasi gani.

Ni wengi kuliko nzige,

hawawezi kuhesabika.

2446:24 2Fal 24:7; Yer 1:15Binti wa Misri ataaibishwa,

atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”

2546:25 Eze 30:14; Nah 3:4; Yer 43:12; Isa 20:6; Eze 30:22; 2Fal 24:7Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi,46:25 Thebesi kwa Kiebrania ni No (au No-Amoni), mji katika Misri. na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao. 2646:26 Yer 44:30; Isa 19:4; Eze 32:11; 29:11-16Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.

2746:27 Yer 29:14; Isa 41:13; Yer 51:46; Isa 11:11; 43:5; 41:8; Yer 50:19“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, ee Israeli.

Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali,

uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao.

Yakobo atakuwa tena na amani na salama,

wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.

2846:28 Kut 14:22; Hes 14:9; Yer 4:27; Isa 8:9-10Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

kwa maana mimi niko pamoja nawe,”

asema Bwana.

“Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambayo miongoni mwake nimekutawanya,

sitakuangamiza wewe kabisa.

Nitakurudi, lakini kwa haki tu,

wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

耶利米書 46:1-28

關於埃及的預言

1耶和華把有關列國的事告訴了耶利米先知。 2約西亞的兒子猶大約雅敬執政第四年,埃及王法老尼哥的軍隊在幼發拉底河邊的迦基米施巴比倫尼布甲尼撒擊敗。關於埃及,耶和華說:

3「要預備大小盾牌,

衝向戰場。

4要套好戰車,

騎上戰馬,

擦亮矛槍,

頂盔貫甲,

準備作戰。

5可是,我看見什麼?

他們驚慌後退,

勇士敗逃,不敢回頭,

驚恐不安。

這是耶和華說的。

6善跑者跑不掉,

強壯者逃不了,

他們仆倒在北面的幼發拉底河邊。

7「那如尼羅河漲溢,

如江水奔騰的是誰呢?

8埃及尼羅河漲溢,

如江水奔騰。

她說,『我要漲溢,淹沒大地,

毀滅城邑和其中的居民。』

9戰馬奔騰吧!

戰車疾駛吧!

勇士啊,就是那些手拿盾牌的古實人和人以及箭法嫺熟的呂底亞人啊,出戰吧!

10因為這是主——萬軍之耶和華向敵人報仇的日子。

刀劍必吞噬他們,

痛飲他們的血,

因為要在北方的幼發拉底河邊向主——萬軍之耶和華獻祭。

11處女埃及啊,

基列取乳香吧!

然而,再多的良藥也是徒然,

你們無法得醫治。

12你們的恥辱傳遍列國,

你們的哀哭響徹大地,

你們的勇士彼此碰撞,

倒在一起。」

13關於巴比倫尼布甲尼撒要來攻打埃及的事,耶和華對耶利米先知說:

14「你們要在埃及宣佈,在密奪挪弗答比匿宣告,

『要擺好陣勢,準備作戰,

因為刀劍要吞噬你們周圍的人。』

15你們的勇士為何仆倒?

他們無法站立,

因為耶和華擊倒了他們,

16使他們跌跌絆絆,紛紛倒下。

他們說,『起來,我們回到同胞那裡,回到故鄉吧,

好躲避敵人的刀劍。』

17他們在那裡喊叫,

埃及王法老只會虛張聲勢,

他已錯失良機。』」

18名叫萬軍之耶和華的王說:

「我憑我的永恆起誓,

將有一位要來,

他的氣勢如群山中的他泊山,

又像海邊的迦密山。

19住在埃及的人啊,

收拾行裝準備流亡吧!

因為挪弗必荒廢,

淪為廢墟,杳無人跡。

20埃及像頭肥美的母牛犢,

但從北方卻來了牛虻。

21埃及的傭兵好像肥牛犢,

都轉身逃之夭夭,無力抵擋,

因為他們遭難、受罰的日子到了。

22「敵軍列隊進攻的時候,

埃及必像蛇一樣嘶嘶地溜走。

敵軍必拿著斧頭蜂擁而來,

像樵夫砍樹一樣攻擊他們。

23埃及的人口雖然稠密如林,

敵軍必像無數的蝗蟲一樣掃平他們。

這是耶和華說的。

24埃及人必蒙羞,

落在北方人的手中。」

25以色列的上帝——萬軍之耶和華說:「看啊,我要懲罰底比斯的神明亞捫埃及的其他神明、法老、首領以及依靠法老的人。 26我要把他們交在想殺他們的巴比倫尼布甲尼撒及其官長手中。然而,日後埃及必再有人居住,如往日一樣。這是耶和華說的。

27「我的僕人雅各啊,不要害怕!

以色列啊,不要驚慌!

因為我要從遠方拯救你,

從流亡之地拯救你的後裔。

雅各必重返家園,安享太平,

不受驚嚇。

28我的僕人雅各啊,不要害怕,

因為我與你同在。

我曾使你流亡到列國,

我必徹底毀滅列國,

但不會徹底毀滅你,

也不會放過你,

我必公正地懲治你。

這是耶和華說的。」