Isaya 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 1:1-31

11:1 1Sam 3:1; Hes 12:6; 2Fal 14:21; 16:1; 1Nya 3:12-13; 2Nya 26:22; 1Sam 22:1, 5; Oba 1:1; Nah 1:1; Isa 40:9; 44:26Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.

Taifa Asi

21:2 Hag 1:12; Amu 11:10; Kum 4:26; Yer 42:5; Isa 23:4; 63:16; 65:2; Eze 24:3; Mik 1:2; Isa 63:16; Mal 1:6Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia!

Kwa maana Bwana amesema:

“Nimewalisha watoto na kuwalea,

lakini wameniasi mimi.

31:3 Yer 4:22; 9:3-6; Hos 2:8; Ay 12:9; Mwa 42:27; Kum 32:28; Isa 42:25; Ay 12:9; Hos 4:1; Isa 48:8; Hos 4:6; 7:9Ngʼombe anamjua bwana wake,

naye punda anajua hori la mmiliki wake,

lakini Israeli hajui,

watu wangu hawaelewi.”

41:4 Yer 23:14; Eze 39:7; 2Fal 19:22; Isa 1:2; Za 14:3; Kum 32:15; Isa 5:19; 31:1; 5:18; 9:17; 14:20; Za 119:87Lo! Taifa lenye dhambi,

watu waliolemewa na uovu,

uzao wa watenda mabaya,

watoto waliozoelea upotovu!

Wamemwacha Bwana,

Wamemkataa kwa dharau

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli

na kumgeuzia kisogo.

51:5 Yer 2:20; 30:17; 44:16-17; 2:30; 5:3; Ebr 3:16; Isa 31:6; 44:16-17; Mit 20:30; Mao 2:11Kwa nini mzidi kupigwa?

Kwa nini kudumu katika uasi?

Kichwa chako chote kimejeruhiwa,

moyo wako wote ni mgonjwa.

61:6 Kum 28:35; Yer 8:22; 14:19; 30:17; Mao 2:13; Eze 34:4; Lk 10:34; 2Sam 14:2; Za 45:7; 104:15; 38:3; Isa 61:3; 53:5; 30:26Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako

hakuna uzima:

ni majeraha matupu na makovu

na vidonda vitokavyo damu,

havikusafishwa au kufungwa

wala kulainishwa kwa mafuta.

71:7 Kum 28:51; Amu 6:3-6; Isa 62:8; 2Fal 18:13; Law 26:34; 26:16; Yer 5:17; Za 109:11Nchi yenu imekuwa ukiwa,

miji yenu imeteketezwa kwa moto;

nchi yenu imeachwa tupu na wageni

mbele ya macho yenu,

imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.

81:8 Za 9:14; Isa 10:32; 30:17; 49:21; Ay 27:18Binti Sayuni ameachwa kama kipenu

katika shamba la mizabibu,

kama kibanda katika shamba la matikitimaji,

kama mji uliohusuriwa.

91:9 Rum 9:29; 2Fal 21:14; Mwa 45:7; 19:24; Isa 4:2; 6:13; 27:12; Yer 23:3; Yoe 2:32Kama Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote1:9 Bwana Mwenye Nguvu Zote hapa ni Yehova Sabaoth, yaani Bwana wa Majeshi; pia Warumi 9:29 na Yakobo 5:4.

asingelituachia walionusurika,

tungelikuwa kama Sodoma,

tungelifanana na Gomora.

101:10 Isa 30:9; 28:14; 5:24; 8:20; 13:19; Ufu 11:8; Mwa 13:13; Eze 16:49; Rum 9:29Sikieni neno la Bwana,

ninyi watawala wa Sodoma;

sikilizeni sheria ya Mungu wetu,

enyi watu wa Gomora!

111:11 Amo 6:4; Yer 6:20; Ebr 10:4; Za 50:8; 40:6; Ay 22:3; Isa 66:3; 1Sam 15:22; Mal 1:10Bwana anasema, “Wingi wa sadaka zenu,

ni kitu gani kwangu?

Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi,

za kondoo dume na mafuta ya wanyama walionona.

Sipendezwi na damu za mafahali

wala za wana-kondoo na mbuzi.

121:12 Kut 23:17; Kum 31:11Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu,

ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo,

huku kuzikanyaga nyua zangu?

131:13 Mit 15:8; 1Nya 23:31; Hag 2:14; Yer 18:15; 44:8; 1Fal 11:24; Mit 28:9; Yer 7:9; Isa 41:24; 66:3Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana!

Uvumba wenu ni chukizo kwangu.

Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada:

siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.

141:14 Za 69:3; Kut 12:16; Mal 3:14; Kum 16:1-7; Neh 10:33; Ay 7:12; Hes 28:11-29; Law 23:1-44Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi, na sikukuu zenu zilizoamriwa:

moyo wangu unazichukia.

Zimekuwa mzigo kwangu,

nimechoka kuzivumilia.

151:15 Ay 27:9; Kum 31:17; 1:45; Mik 3:4; Hos 4:2; Isa 57:17; 59:2; Kut 9:29; Yoe 3:21; 1Sam 8:18Mnaponyoosha mikono yenu katika maombi,

nitaficha macho yangu nisiwaone;

hata mkiomba maombi mengi

sitasikiliza.

Mikono yenu imejaa damu;

161:16 Yer 4:14; 25:5; Hes 19:11-16; Isa 52:11; Rut 3:3; Yak 4:8; Mt 27:24jiosheni na mkajitakase.

Yaondoeni matendo yenu maovu

mbele zangu!

Acheni kutenda mabaya,

171:17 Mik 6:8; Sef 2:3; Ay 22:9; Isa 33:5; Kut 22:22; Amo 5:14-15; Za 34:14; 72:1; Isa 11:4jifunzeni kutenda mema!

Tafuteni haki,

watieni moyo walioonewa.

Teteeni shauri la yatima,

wateteeni wajane.

181:18 1Sam 2:25; Isa 41:21; 55:7; Ufu 7:14; Za 51:7; Isa 43:9; 41:1; 43:26“Njooni basi tuhojiane,”

asema Bwana.

“Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu,

zitakuwa nyeupe kama theluji;

ingawa ni nyekundu sana kama damu,

zitakuwa nyeupe kama sufu.

191:19 Ezr 9:12; Za 34:10; Ay 36:11; Isa 50:10; 62:9; Kum 30:15-16; Isa 58:14; 65:13; 30:32Kama mkikubali na kutii,

mtakula mema ya nchi,

201:20 Yer 17:27; Hes 23:19; Ay 15:22; 1Sam 12:15; Isa 3:25; 21:17; 34:16; 27:1; 65:12lakini kama mkikataa na kuasi,

mtaangamizwa kwa upanga.”

Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena.

211:21 Isa 57:3-9; Yer 2:20; 3:2-9; 13:27; Eze 23:3; Hos 2:1-13; Amo 6:12; Isa 46:13; 59:14; Mit 6:17Tazama jinsi mji uliokuwa mwaminifu

umekuwa kahaba!

Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu,

haki ilikuwa inakaa ndani yake,

lakini sasa ni wauaji!

221:22 Za 119:119Fedha yenu imekuwa takataka,

divai yenu nzuri imechanganywa na maji.

231:23 Kum 19:14; Amo 5:8; Yer 5:28; Mik 2:1-2; 6:12; Kut 23:8; Isa 10:2; Eze 22:6-7; Isa 1:2; Mik 3:9; Amo 5:12; Hab 1:4Watawala wenu ni waasi,

rafiki wa wevi,

wote wanapenda rushwa

na kukimbilia hongo.

Hawatetei yatima,

shauri la mjane haliletwi mbele yao lisikilizwe.

241:24 Mwa 49:24; Isa 34:2, 8; 47:3; 59:17; 63:4; Yer 51:6; Eze 5:13; Kum 32:43Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi:

“Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu

na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.

251:25 Yer 9:7; 6:29; Ufu 3:19; Isa 48:10; Kum 28:63; Za 78:38; 2Nya 29:15; Eze 22:22; Za 119:119Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu,

nitawasafisha takataka zenu zote

na kuwaondolea unajisi wenu wote.

261:26 Mik 4:8; Zek 8:3; Yer 31:23; 33:7; Kum 9:24; Mwa 32:28; Isa 32:16; 46:13; 4:3; 48:2Nitawarudishia waamuzi wenu kama ilivyokuwa siku za zamani,

nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni.

Baadaye utaitwa,

Mji wa Haki,

Mji Mwaminifu.”

271:27 Isa 31:6; 59:20; 35:10; 41:14; 62:12; 63:4; 30:15; Hos 2:19; Eze 18:30Sayuni itakombolewa kwa haki,

wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.

281:28 Yer 4:18; 44:12; 2The 1:8-9; Isa 33:14; 43:27; 48:8; 16:2; Kum 32:18; 32:15; Za 9:5; Yer 16:4Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa,

nao wanaomwacha Bwana wataangamia.

291:29 Eze 6:13; Hos 4:13; Isa 65:3; 42:17; 44:9; 57:5; Za 97:7; Yer 10:14; Za 97:7“Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni

ambayo mlifurahia,

mtafadhaika kwa sababu ya bustani

mlizozichagua.

301:30 Za 1:3Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka,

kama bustani isiyokuwa na maji.

311:31 Isa 4:4; 5:24; 9:18-19; 24:6; 33:14; 66:15-16, 24; Yer 5:14; 7:20; Mal 3:2; Mt 25:41Mtu mwenye nguvu atatoweka kama majani makavu yawakayo moto,

na kazi yake kama cheche ya moto;

vyote vitaungua pamoja,

wala hakuna wa kuuzima huo moto.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以賽亞書 1:1-31

1猶大烏西雅約坦亞哈斯希西迦執政期間,亞摩斯的兒子以賽亞看到了以下有關猶大耶路撒冷的異象。

上帝責備叛逆的子民

2諸天啊,請聽!

大地啊,要側耳聽!

耶和華說:

「我把孩子撫育成人,

他們竟然背叛我。

3牛認識主人,

驢也認得主人的槽,

以色列卻不認識我,

我的子民卻不明白。」

4唉!這罪惡的民族,

惡貫滿盈的百姓,

作惡的子孫,

敗壞的兒女!

他們背棄耶和華,

藐視以色列的聖者,

與祂疏遠。

5你們為什麼一再叛逆?

你們為什麼還要受責打?

你們已經頭破血流,

身心疲憊不堪。

6你們已經體無完膚,

從頭到腳傷痕纍纍,盡是瘀腫和傷口,

沒有清洗,沒有包紮,

也沒有敷藥。

7你們的土地荒涼,

城邑化為灰燼。

你們親眼目睹自己的田園被外族人侵吞、毀壞、變成不毛之地。

8僅存的少女錫安也像葡萄園裡的草棚,

像瓜田中的茅舍,

像被困無援的孤城。

9若不是萬軍之耶和華讓我們一些人存活,

我們早就像所多瑪蛾摩拉一樣滅亡了。

10你們這些所多瑪的首領啊,

要聆聽耶和華的話!

你們這些蛾摩拉的百姓啊,

要側耳聽我們上帝的訓誨!

11耶和華說:

「你們獻上許多祭物,對我有什麼用呢?

我厭煩公綿羊的燔祭和肥畜的脂肪,

我不喜歡公牛、羊羔和公山羊的血。

12「你們來朝見我的時候,

誰要求你們帶著這些來踐踏我的院宇呢?

13不要再帶毫無意義的祭物了。

我憎惡你們燒的香。

我無法容忍你們又作惡又舉行莊嚴的聚會,

就是你們的朔日1·13 「朔日」即每月初一。、安息日和大會。

14我憎惡你們的朔日及各種節期,

它們成了我的重擔,

令我厭倦。

15你們舉手禱告,我必掩面不理。

即使你們禱告再多,

我也不會聽,

因為你們雙手沾滿鮮血。

16你們要洗淨自己,

不要讓我再看見你們的惡行,

要停止作惡。

17你們要學習行善,

追求正義,

幫助受欺壓的,

替孤兒辯護,

為寡婦伸冤。」

18耶和華說:

「來吧,我們彼此理論!

你們的罪雖如朱紅,

也必潔白如雪;

你們的罪雖如緋紅,

也必白如羊毛。

19如果你們願意聽從,

就必享用這地方的美好出產。

20如果你們執意叛逆,

就必喪身刀下。」

這是耶和華親口說的。

21忠信的城竟變成了妓女!

從前充滿公平,

是公義之家,

現在卻住著兇手。

22你的銀子變為渣滓;

你的美酒摻了水份。

23你的首領是叛逆之徒,

與盜賊為伍,

個個喜愛賄賂,

貪圖好處,

不為孤兒辯護,

不替寡婦伸冤。

24所以,主——萬軍之耶和華,

以色列的大能者說:

「唉!我要向我的敵人報仇,

向我的仇敵雪恨。

25我必出手攻擊你,

用鹼煉淨你的渣滓,

除盡你的雜質。

26我必像從前一樣恢復你的審判官,

像起初一樣恢復你的謀士。

之後,你必被稱為公義之城,

忠信之邑。」

27耶和華必因祂的公正救贖錫安

必因祂的公義拯救城中悔改的人。

28但叛逆之輩和犯罪之徒必同遭毀滅,

背棄耶和華的人必滅亡。

29你們必因所喜愛的聖橡樹而抱愧,

必因所選擇的偶像園而蒙羞。

30你們必像葉子枯萎的橡樹,

又如無水的園子。

31有權勢的人像麻絨,他的行為如火花,

兩者要一同焚毀,無人能救。