Walawi 23 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Walawi 23:1-44

Sikukuu Zilizoamriwa

1Bwana akamwambia Mose, 223:2 Hes 29:39; Eze 44:24; Kol 2:16; Isa 6:3; Mt 6:9; Yn 12:28; Kut 32:5; Hes 10:2-3; 2Nya 30:5“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Hizi ndizo sikukuu zangu zilizoamriwa, sikukuu zilizoamriwa za Bwana, ambazo mtazitangaza kuwa makusanyiko matakatifu.

Sabato

323:3 Kut 20:9-10; Ebr 4:9-10; Kum 5:13; Hes 28:26; Lk 13:14; Neh 13:22; Isa 56:2; 58:13“ ‘Kuna siku sita mnazoweza kufanya kazi, lakini siku ya saba ni Sabato ya kupumzika, siku ya kusanyiko takatifu. Hamtafanya kazi yoyote. Popote mnapoishi, ni Sabato kwa Bwana.

Pasaka Na Mikate Isiyotiwa Chachu

(Hesabu 28:16-25)

423:4 Nah 1:15; Kut 23:14“ ‘Hizi ni sikukuu za Bwana zilizoamriwa, makusanyiko matakatifu mtakayoyatangaza kwa nyakati zilizoamriwa: 523:5 Kut 12:6-11; Hes 28:16-17; Kum 16:1-8; Yos 5:10Pasaka ya Bwana huanza jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. 623:6 Kut 12:17-19Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa kwanza, Sikukuu ya Bwana ya Mikate Isiyotiwa Chachu huanza; kwa siku saba, mtakula mikate isiyotiwa chachu. 7Katika siku ya kwanza, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na msifanye kazi zenu za kawaida. 8Kwa siku saba mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Kwenye siku hiyo ya saba mtafanya kusanyiko takatifu, na msifanye kazi zenu za kawaida.’ ”

Malimbuko

9Bwana akamwambia Mose, 1023:10 Hes 15:2; Law 19:9; Kut 22:29; 34:22; Rum 11:16; Kum 16:9; Yos 3:15; Mit 3:9; 1Kor 15:20; Yak 1:18“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi nitakayowapa na kuvuna mazao ya nchi hiyo, leteni kwa kuhani mganda wa nafaka ya kwanza mtakayovuna. 1123:11 Kut 29:24; 28:38; Law 9:21; 10:14Naye atauinua huo mganda mbele za Bwana ili ukubaliwe kwa niaba yenu; kuhani ataupunga siku inayofuata Sabato. 1223:12 Law 12:6; Kut 12:5Siku hiyo mtakapoinua huo mganda, lazima mtoe kwa Bwana dhabihu ya kuteketezwa kwa moto ya mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiye na dosari, 1323:13 Law 2:14-16; 6:20; 10:9; 24:5; Hes 15:6; 28:9; Mwa 35:14pamoja na sadaka yake ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa23:13 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo mbili. za unga laini uliochanganywa na mafuta, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kupendeza, na sadaka yake ya kinywaji ya robo ya hini23:13 Robo ya hini ni sawa na lita moja. ya divai. 1423:14 Yos 5:11; Rut 2:14; 1Sam 17:17; 25:18; 2Sam 17:28; Kut 34:26; Law 3:17; Hes 10:8; 15:21; Yer 2:3Kamwe msile mkate wowote, au nafaka iliyokaangwa au nafaka mpya, mpaka siku ile mtakayomletea Mungu wenu sadaka hii. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo, popote mnapoishi.

Sikukuu Ya Majuma

(Hesabu 28:26-31)

15“ ‘Tangu siku ile iliyofuata Sabato, siku mliyotoa sadaka ya mganda wa kuinuliwa, hesabuni majuma saba kamili. 1623:16 Mdo 20:16; 2:1; Hes 28:26Mtahesabu siku hamsini mpaka siku inayofuata Sabato ya saba, ndipo mtatoa sadaka ya nafaka mpya kwa Bwana. 1723:17 Kut 34:22; 23:16; Hes 15:17-19Kutoka popote mnapoishi, mtaleta mikate miwili ya unga laini, sehemu mbili za kumi za efa, uliookwa kwa chachu, kuwa sadaka ya kuinuliwa ya malimbuko kwa Bwana. 1823:18 Kut 29:41; 30:9; 37:16; Yer 19:13; 44:18Toeni pamoja na hiyo mikate wana-kondoo saba, kila mmoja wa mwaka mmoja asiye na dosari, na fahali mchanga, na kondoo dume wawili. Watakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto iliyotolewa kwa Bwana, pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, sadaka iliyotolewa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 1923:19 Hes 28:30; Law 4:23Kisha toeni dhabihu ya mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wana-kondoo wawili, kila mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya amani. 2023:20 Kut 29:24Kuhani atawainua hao wana-kondoo wawili mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, pamoja na mkate wa malimbuko. Ni sadaka takatifu kwa Bwana kwa ajili ya kuhani. 2123:21 Kut 32:5Siku iyo hiyo mtatangaza kusanyiko takatifu, na msifanye kazi zenu za kawaida. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo, popote mnapoishi.

2223:22 Law 19:9-10; Kum 24:19-21; Rut 2:2, 15; Kut 23:11; Kum 15:1-18; Ay 20:19; Za 112:9; Mit 14:31; Isa 58:7-8; Yak 2:1“ ‘Mnapovuna mavuno ya ardhi yenu, msivune hadi mpakani mwa shamba lenu, au kukusanya masazo ya mavuno yenu. Hayo utayaacha kwa ajili ya maskini na mgeni. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’ ”

Sikukuu Ya Tarumbeta

(Hesabu 29:1-6)

23Bwana akamwambia Mose, 2423:24 Ezr 3:1; Hes 10:9-10; 29:1; 31:6; 2Fal 11:14; 2Nya 13:12; Za 98:6“Waambie Waisraeli: ‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na siku ya mapumziko, kusanyiko takatifu la ukumbusho litakaloadhimishwa kwa kupiga tarumbeta. 25Msifanye kazi zenu zozote za kawaida, lakini toeni sadaka kwa Bwana iliyoteketezwa kwa moto.’ ”

Siku Ya Upatanisho

(Hesabu 29:7-11)

26Bwana akamwambia Mose, 2723:27 Law 16:29; Kut 30:10; Hes 29:7; Isa 58:3-5; Dan 10:3, 12“Siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni Siku ya Upatanisho. Mtafanya kusanyiko takatifu, mfunge, nanyi mtoe sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. 28Msifanye kazi siku hiyo, kwa sababu ni Siku ya Upatanisho, ambapo upatanisho unafanyika kwa ajili yenu mbele za Bwana Mungu wenu. 2923:29 Mwa 17:14; Law 7:20; Hes 5:2Mtu yeyote ambaye hatafunga siku hiyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake. 3023:30 Law 20:3Mtu yeyote atakayefanya kazi siku hiyo nitamwangamiza kutoka miongoni mwa watu wake. 3123:31 Law 3:17Hamtafanya kazi kamwe. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo popote mnapoishi. 3223:32 Law 16:31; Neh 13:19Ni Sabato ya mapumziko kwenu ninyi, na lazima mfunge. Tangu jioni ya siku ya tisa ya mwezi hadi jioni inayofuata, mtaishika Sabato yenu.”

Sikukuu Ya Vibanda

(Hesabu 29:12-40)

33Bwana akamwambia Mose, 3423:34 1Fal 8:2; Hag 2:1; Kut 23:16; Yn 7:2, 37; Kut 34:22; Ezr 3:4; Neh 8:14; Zek 14:16“Waambie Waisraeli: ‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, Sikukuu ya Bwana ya vibanda itaanza, nayo itaadhimishwa kwa siku saba. 35Siku ya kwanza ni kusanyiko takatifu, msifanye kazi zenu za kawaida. 3623:36 1Fal 8:2; 2Nya 7:9; Neh 8:18; Yn 7:37; Law 1:9Kwa siku saba toeni sadaka kwa Bwana za kuteketezwa kwa moto. Kwenye siku ya nane fanyeni kusanyiko takatifu, na mtoe sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Ni kusanyiko la mwisho, msifanye kazi zenu za kawaida.

37(“ ‘Hizi ni sikukuu za Bwana zilizoamriwa, ambazo mtazitangaza kuwa makusanyiko matakatifu kwa kuleta sadaka kwa Bwana za kuteketeza kwa moto: sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, dhabihu na sadaka za vinywaji zitahitajika kila siku. 3823:38 Kut 20:10; 2Nya 2:4; Eze 45:17; Law 7:16Sadaka hizi ni nyongeza ya zile mnazozitoa katika Sabato za Bwana, na pia ni nyongeza ya matoleo yenu ya chochote mlichoweka nadhiri, na sadaka zenu zote za hiari mnazozitoa kwa Bwana.)

3923:39 Isa 62:9; Kut 23:16; Kum 16:13; Mt 21:8“ ‘Basi kuanzia siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, baada ya kuvuna mazao yote ya nchi, mtaadhimisha sikukuu kwa Bwana kwa siku saba; siku ya kwanza ni mapumziko, pia siku ya nane ni mapumziko. 4023:40 Za 9:2; 66:6; 105:43; 118:27; 137:2; Neh 8:10, 14-17; Isa 44:4; Kum 12:7; 14:26; 28:47; Yoe 2:26Siku ya kwanza mtachukua matunda mazuri ya miti, matawi ya mitende, matawi yenye majani mengi, na matawi ya mirebi, nanyi mtashangilia mbele za Bwana Mungu wenu kwa siku saba. 41Mtaadhimisha siku hii kuwa sikukuu kwa Bwana kwa siku saba kila mwaka. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo; iadhimisheni mwezi wa saba. 4223:42 Kut 23:16; Neh 8:14-16Mtaishi katika vibanda kwa siku saba: Wazawa wote wa Waisraeli wataishi katika vibanda, 4323:43 Kum 31:13; Za 78:5ili wazao wenu wajue kuwa niliwafanya Waisraeli waishi kwenye vibanda nilipowatoa Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’ ”

44Kwa hiyo Mose akawatangazia Waisraeli sikukuu zilizoamriwa na Bwana.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

利未記 23:1-44

有關節期的條例

1耶和華對摩西說: 2「你要告訴以色列人,以下是耶和華所定的節期,你們要宣佈這些節期為舉行聖會的日子。

安息日

3「你們一週可以工作六天,但第七天是完全休息的安息日,你們要舉行聖會。不可做任何工,無論你們住在哪裡,都要守耶和華的安息日。

4「以下是耶和華所定的節期,你們要在這些日子召開聖會。

逾越節和除酵節

5「從一月十四日傍晚開始是耶和華的逾越節。 6從一月十五日開始是耶和華的除酵節,你們要連續七天吃無酵餅。 7在除酵節的第一天,你們要舉行聖會,不可做日常工作。 8一連七天你們要獻火祭給耶和華。第七天,你們要舉行聖會,不可做日常工作。」

初熟節

9耶和華對摩西說: 10「你把以下條例告訴以色列人。

「你們進入耶和華將要賜給你們的那片土地以後,每逢收割莊稼之時,你們要帶一捆初熟的穀物交給祭司。 11祭司要在安息日後第一天把那捆穀物在耶和華面前搖一搖,你們所獻的就會得到悅納。 12在獻穀物那天,你們要獻給耶和華一隻毫無殘疾、一歲的公羊羔作燔祭, 13同時要把兩公斤調油的細麵粉作素祭,一起獻給耶和華作馨香的火祭,也要獻一升酒作奠祭。 14你們必須先將這些供物獻給你們的上帝後,才可以吃餅、烘烤的穀物和新鮮穗子。不論住在哪裡,這是你們世代當守的永久律例。

五旬節

15「從安息日後第一天,即你們獻上搖祭的那天算起,你們要數整整七週, 16一直數到第七個安息日後的第一天,共五十天。到那天,你們要把新收的穀物作為素祭獻給耶和華。 17你們要用兩公斤細麵粉加上酵,烤成兩個餅作搖祭,從你們居住的地方帶來獻給耶和華作初熟之祭。 18你們要把七隻毫無殘疾的一歲公羊羔、一頭公牛犢、兩隻公綿羊和那兩個餅,一起獻給耶和華作燔祭。這些一起獻上的燔祭、素祭和奠祭,是蒙耶和華悅納的馨香火祭。 19你們也要獻一隻公山羊作贖罪祭,兩隻一歲的公綿羊作平安祭。 20祭司要把這兩隻公綿羊和初熟之物做的餅作為搖祭,在耶和華面前搖一搖。這些是獻給耶和華的聖物,歸祭司所有。 21你們要在那天召開聖會,不可做日常工作。不論住在哪裡,這是你們世代當守的永久律例。 22你們收割時,不可割盡田角地邊的莊稼,也不可撿落在地裡的,要把這些留給窮人和外族人。我是你們的上帝耶和華。」

吹號節

23耶和華對摩西說: 24「你告訴以色列人:你們要在七月一日完全休息,要吹號作紀念,召開聖會。 25你們不可做日常工作,要獻火祭給耶和華。」

贖罪日

26耶和華對摩西說: 27「七月十日是贖罪日,你們要舉行聖會,禁食,獻火祭給耶和華。 28那是在你們的上帝耶和華面前為自己贖罪的日子,你們不可工作。 29那天,凡不禁食的,要將他從民中剷除; 30凡在那天工作的,耶和華要毀滅他。 31你們不可做任何工作。不論住在哪裡,這是你們世代當守的永久律例。 32那是你們完全休息的安息日。從七月九日傍晚至次日傍晚,你們必須禁食。」

住棚節

33耶和華對摩西說: 34「你把以下條例告訴以色列人。

「從七月十五日開始,你們要一連七天向耶和華守住棚節。 35第一天,你們要舉行聖會,不可做日常工作。 36一連七天你們要獻火祭給耶和華。第八天要舉行聖會,獻火祭給耶和華。這是莊嚴的聚會,你們不可做日常工作。

37「以上是耶和華所定的節期。在這些節期裡,你們要召開聖會,按規定的日子獻給耶和華燔祭、素祭、奠祭和其他祭物。 38除了守安息日並向耶和華獻供物、還願祭和自願獻的祭以外,你們還要守這些節期。

39「你們收割完後,從七月十五日起,要一連七天慶祝耶和華的節期,第一天和第八天是完全休息的安息日。 40第一天,你們要摘下樹上結的上好果子,折下棕樹枝、葉子濃密的樹枝與河邊的柳枝,在你們的上帝耶和華面前歡慶七天。 41在每年七月的這七天,你們要向耶和華守這節期。這是你們世代當守的永久律例。 42你們要搭棚居住七天,所有以色列人都要住在棚裡。 43這樣,你們的後代就會知道,我帶領以色列人離開埃及後,曾讓他們住在棚裡。我是你們的上帝耶和華。」

44於是,摩西以色列人宣佈了耶和華所定的這些節期。