Walawi 24 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Walawi 24:1-23

Mafuta Na Mikate Mbele Za Bwana

1Bwana akamwambia Mose, 224:2 Kut 27:20; 39:37; Hes 8:2-4“Waagize Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili taa ziwe zinawaka daima. 324:3 Kut 12:14Nje ya pazia la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, Aroni ataziwasha taa mbele za Bwana kuanzia jioni hadi asubuhi bila kuzima. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. 424:4 Kut 25:31; 31:8Taa zilizo juu ya kinara cha dhahabu safi mbele za Bwana lazima zihudumiwe daima.

524:5 Kut 25:30; Ebr 9:2; Law 23:13; Kut 40:24“Chukua unga laini, uoke mikate kumi na miwili, ukitumia sehemu mbili za kumi za efa24:5 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo mbili. za unga kwa kila mkate. 624:6 Kut 25:23-30; Hes 4:7; 1Fal 7:48; Ebr 9:2; 1Nya 9:32Iweke katika mistari miwili, kila mstari mikate sita, uiweke mbele za Bwana juu ya meza iliyotengenezwa kwa dhahabu safi. 724:7 Law 2:1-2Kando ya kila mstari, weka uvumba safi kama sehemu ya kumbukumbu ili kuwakilisha mikate kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa kuteketezwa kwa moto. 824:8 Kut 25:30; 1Nya 9:32; 2Nya 2:2-4; Mt 12:5Mikate hii itawekwa mbele za Bwana kila wakati, Sabato baada ya Sabato, kwa niaba ya Waisraeli, kuwa Agano la kudumu. 924:9 Law 6:16-17; 8:31; Mt 12:4; Mk 2:26; Lk 6:4; 1Sam 9:21; Kut 29:33Hii ni mali ya Aroni na wanawe, watakaoila katika mahali patakatifu, kwa sababu ni sehemu takatifu sana ya fungu lao la kawaida la sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa kuteketezwa kwa moto.”

Mwenye Kukufuru Apigwa Mawe

10Basi mwana wa mama Mwisraeli na baba Mmisri alikwenda miongoni mwa Waisraeli, nayo mapigano yakatokea ndani ya kambi kati yake na Mwisraeli. 1124:11 Kut 3:15; 18:22; 20:7; 31:2; 2Fal 6:33; Ay 1:11; Hes 1:4; 7:2; 10:15; 13:2; 17:2; Yos 7:18; 1Fal 7:18Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru Jina la Bwana kwa kulaani; kwa hiyo wakamleta kwa Mose. (Jina la mama yake aliitwa Shelomithi binti wa Dibri, wa kabila la Dani.) 1224:12 Kut 18:16; Hes 15:34Nao wakamweka mahabusu mpaka mapenzi ya Bwana yawe wazi kwao.

13Ndipo Bwana akamwambia Mose: 1424:14 Law 20:2; Kum 13:9; 17:5-7; Mdo 7:58“Mchukue huyo aliyekufuru nje ya kambi. Wale wote waliomsikia akikufuru wataweka mikono juu ya kichwa chake, kisha kusanyiko lote litampiga mawe. 1524:15 Kut 22:28; Law 5:1; Hes 9:13Waambie Waisraeli: ‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani Mungu wake, atakuwa na hatia kwa uovu wake; 1624:16 Kut 22:28; 21:21; 1Fal 21:10-13; Mt 26:66; Mk 14:64; Yn 10:33; Mdo 7:58; Za 74:10, 18yeyote atakayekufuru Jina la Bwana ni lazima auawe. Kusanyiko lote litampiga kwa mawe. Iwe ni mgeni au mzawa, atakapolikufuru Jina la Bwana, ni lazima auawe.

1724:17 Mwa 9:6; Kut 21:12; Kum 27:24; Hes 35:31; Mt 26:52; Ufu 13:10“ ‘Kama mtu yeyote atamuua mtu mwingine, ni lazima auawe. 18Mtu yeyote auaye mnyama wa mtu mwingine lazima afidie, uhai kwa uhai. 19Ikiwa mtu yeyote atamjeruhi jirani yake, chochote alichomtenda naye atatendewa: 2024:20 Kut 21:24; Mt 5:38; Law 19:34; Kum 10:17-19iwapo amemvunja mfupa atavunjwa mfupa, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama alivyomjeruhi mwenzake, vivyo hivyo ndivyo atakavyojeruhiwa. 2124:21 Kut 21:33Yeyote auaye mnyama wa mtu lazima alipe fidia, lakini yeyote auaye mtu, lazima auawe. 2224:22 Kut 12:49; 22:21; Eze 47:22; Hes 9:14; 15:16Mtakuwa na sheria iyo hiyo kwa mgeni na kwa mzawa. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’ ”

2324:23 Kum 13:9; 17:7Kisha Mose akasema na Waisraeli, nao wakamchukua yule aliyekufuru nje ya kambi na kumpiga mawe. Waisraeli wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

利未記 24:1-23

燈和供餅的條例

1耶和華對摩西說: 2「你要吩咐以色列人把榨的純橄欖油給你拿來點燈,使燈常明。 3亞倫要負責照看會幕內遮掩約櫃的幔子外的燈,使燈從晚上到早晨一直在耶和華面前亮著。這是你們世代當守的永久律例。 4亞倫要在耶和華面前常常照看這些放在純金燈臺上的燈。

5「你要用細麵粉烤十二個餅,每個餅用兩公斤細麵粉。 6你要把餅擺成兩行,放在耶和華面前的純金桌子上,每行六個, 7每行餅上放一些純乳香,象徵這些餅是獻給耶和華的火祭。 8每逢安息日,要定期把餅擺在耶和華面前。這是以色列人要永遠遵守的約。 9這些餅要歸亞倫及其子孫。他們要在聖潔之處吃,因為在獻給耶和華的火祭中,這是至聖之物,要永遠歸祭司所有。」

處死褻瀆聖名者

10有一個人,母親是以色列人,父親是埃及人,他在營中與一個以色列人打起架來。 11他說咒詛的話,褻瀆了上帝的名,他們把他帶到摩西那裡。他母親叫示羅密,是支派底伯利的女兒。 12他們把他關押起來,等候耶和華的指示。 13耶和華對摩西說: 14「把那褻瀆聖名的人帶到營外,所有聽見的人都把手放在他頭上,然後全體會眾要用石頭打死他。 15你要告訴以色列人,誰咒詛上帝,誰就要承擔自己的罪。 16凡褻瀆耶和華聖名的,必須被處死,全體會眾要用石頭打死他。不論是外族人還是以色列人,凡褻瀆聖名的,都必須被處死。 17凡殺人的,必須被處死。 18打死別人牲畜的,必須賠償牲畜,以命還命。 19傷害鄰舍的,必須受同樣的傷害, 20要以傷還傷,以眼還眼,以牙還牙。他怎樣傷害別人,也要怎樣傷害他。 21打死別人牲畜的,必須賠償牲畜;殺人的,必須償命。 22不論是以色列人還是外族人,都要遵守這些律法。我是你們的上帝耶和華。」 23於是,摩西把這些話告訴以色列人,他們就按照耶和華對摩西的吩咐,把那褻瀆聖名的人帶到營外,用石頭打死了。