Walawi 15 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Walawi 15:1-33

Kutokwa Na Umajimaji Usababishao Unajisi

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 215:2 Law 22:4; Hes 5:2; 2Sam 3:29; Mt 9:20; Mk 5:25; Lk 8:43“Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi. 3Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:

4“ ‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi. 515:5 Law 11:24-25; 14:8; 17:15; Ebr 9:10Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 6Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

715:7 Law 22:4-5“ ‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

815:8 Hes 12:14; Ay 30:10; 2Kor 7:1“ ‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

9“ ‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi, 1015:10 Hes 19:10na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

11“ ‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

1215:12 Law 6:28; 11:32“ ‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.

1315:13 Law 8:33; 14:8; Hes 12:14; 19:11“ ‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika. 1415:14 Law 14:22; Hes 6:10-14Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani. 1515:15 Law 5:7; 14:18-19, 31; Ebr 9:14; 10:1Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.

1615:16 Kum 23:10-11; Law 22:4; 15:18; 1Sam 21:4“ ‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni. 17Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni. 18Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.

1915:19 Law 12:2; Eze 36:17“ ‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.

20“ ‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi. 21Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 2215:22 2Kor 7:1; Eze 36:17Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 23Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.

2415:24 Law 12:2; 18:19; 20:18; Eze 18:6“ ‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.

2515:25 Mt 9:20; Lk 8:43; Mk 5:25“ ‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake. 26Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi. 27Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

28“ ‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada. 2915:29 Law 14:22; 15:30; 5:10; 14:20, 31; 18:19; 2Sam 11:4; Mk 5:25; Lk 8:43Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania. 30Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.

3115:31 Law 20:3; Hes 5:3; 19:13, 20; 2Sam 15:25; 2Fal 21:7; Za 33:14; 74:7; 76:2; Eze 5:11; 23:38“ ‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu,15:31 Yaani maskani ya Mungu. ambayo yapo katikati yao.’ ”

32Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa, 33kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.

New International Version

Leviticus 15:1-33

Discharges Causing Uncleanness

1The Lord said to Moses and Aaron, 2“Speak to the Israelites and say to them: ‘When any man has an unusual bodily discharge, such a discharge is unclean. 3Whether it continues flowing from his body or is blocked, it will make him unclean. This is how his discharge will bring about uncleanness:

4“ ‘Any bed the man with a discharge lies on will be unclean, and anything he sits on will be unclean. 5Anyone who touches his bed must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening. 6Whoever sits on anything that the man with a discharge sat on must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

7“ ‘Whoever touches the man who has a discharge must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

8“ ‘If the man with the discharge spits on anyone who is clean, they must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

9“ ‘Everything the man sits on when riding will be unclean, 10and whoever touches any of the things that were under him will be unclean till evening; whoever picks up those things must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

11“ ‘Anyone the man with a discharge touches without rinsing his hands with water must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

12“ ‘A clay pot that the man touches must be broken, and any wooden article is to be rinsed with water.

13“ ‘When a man is cleansed from his discharge, he is to count off seven days for his ceremonial cleansing; he must wash his clothes and bathe himself with fresh water, and he will be clean. 14On the eighth day he must take two doves or two young pigeons and come before the Lord to the entrance to the tent of meeting and give them to the priest. 15The priest is to sacrifice them, the one for a sin offering15:15 Or purification offering; also in verse 30 and the other for a burnt offering. In this way he will make atonement before the Lord for the man because of his discharge.

16“ ‘When a man has an emission of semen, he must bathe his whole body with water, and he will be unclean till evening. 17Any clothing or leather that has semen on it must be washed with water, and it will be unclean till evening. 18When a man has sexual relations with a woman and there is an emission of semen, both of them must bathe with water, and they will be unclean till evening.

19“ ‘When a woman has her regular flow of blood, the impurity of her monthly period will last seven days, and anyone who touches her will be unclean till evening.

20“ ‘Anything she lies on during her period will be unclean, and anything she sits on will be unclean. 21Anyone who touches her bed will be unclean; they must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening. 22Anyone who touches anything she sits on will be unclean; they must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening. 23Whether it is the bed or anything she was sitting on, when anyone touches it, they will be unclean till evening.

24“ ‘If a man has sexual relations with her and her monthly flow touches him, he will be unclean for seven days; any bed he lies on will be unclean.

25“ ‘When a woman has a discharge of blood for many days at a time other than her monthly period or has a discharge that continues beyond her period, she will be unclean as long as she has the discharge, just as in the days of her period. 26Any bed she lies on while her discharge continues will be unclean, as is her bed during her monthly period, and anything she sits on will be unclean, as during her period. 27Anyone who touches them will be unclean; they must wash their clothes and bathe with water, and they will be unclean till evening.

28“ ‘When she is cleansed from her discharge, she must count off seven days, and after that she will be ceremonially clean. 29On the eighth day she must take two doves or two young pigeons and bring them to the priest at the entrance to the tent of meeting. 30The priest is to sacrifice one for a sin offering and the other for a burnt offering. In this way he will make atonement for her before the Lord for the uncleanness of her discharge.

31“ ‘You must keep the Israelites separate from things that make them unclean, so they will not die in their uncleanness for defiling my dwelling place,15:31 Or my tabernacle which is among them.’ ”

32These are the regulations for a man with a discharge, for anyone made unclean by an emission of semen, 33for a woman in her monthly period, for a man or a woman with a discharge, and for a man who has sexual relations with a woman who is ceremonially unclean.