Sefania 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Sefania 2:1-15

12:1 2Nya 20:4; Yoe 1:14; 2:16; Yer 3:3; 6:15Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja,

enyi taifa lisilo na aibu,

22:2 Isa 17:13; Hos 13:3; 2Fal 23:26; Yer 4:4; 10:25; Eze 7:19; Mao 4:11kabla ya wakati ulioamriwa haujafika

na siku ile inayopeperusha kama makapi,

kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu,

kabla siku ya ghadhabu ya Bwana

haijaja juu yenu.

32:3 Amo 5:6; Yoe 2:4; Isa 1:17; Za 45:4; 57:1; 76:9Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi,

ninyi ambao hufanya lile analoamuru.

Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu;

labda mtahifadhiwa

siku ya hasira ya Bwana.

Dhidi Ya Ufilisti

42:4 Mwa 10:19; Amo 1:6-8; Zek 9:5-7; Yer 6:4; 47:5Gaza utaachwa

na Ashkeloni utaachwa magofu.

Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu

na Ekroni utangʼolewa.

52:5 1Sam 30:14; Law 26:31; Eze 25:16; Yos 13:3; Isa 14:30Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari,

enyi Wakerethi;

neno la Bwana liko dhidi yenu,

ee Kanaani, nchi ya Wafilisti.

“Mimi nitawaangamiza,

na hakuna atakayebaki.”

62:6 Isa 5:17; 17:2Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi,

patakuwa mahali pa wachungaji

na mazizi ya kondoo.

72:7 Isa 11:11; Hag 1:12; Mik 5:7; 4:10; Kut 4:31; Lk 1:68; Mwa 45:7; Kum 30:3; Za 126:4; Yer 23:3; 32:44; Hos 6:11; Eze 39:25; Yoe 3:1; Amo 1:6-8Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda,

hapo watapata malisho.

Wakati wa jioni watajilaza chini

katika nyumba za Ashkeloni.

Bwana Mungu wao atawatunza,

naye atawarudishia wafungwa wao.

Dhidi Ya Moabu Na Amoni

82:8 Mwa 19:37; Yer 48:27; 49:1; Eze 25:3, 8; 21:28; Mao 3:61; Isa 16:6“Nimeyasikia matukano ya Moabu

nazo dhihaka za Waamoni,

ambao waliwatukana watu wangu

na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.

92:9 Kum 23:6; 29:23; Isa 11:14; Yer 48:1-47; 49:1-6; Eze 25:1-11; 2Fal 19:31; Amo 1:13; 2:1-3Hakika, kama niishivyo,”

asema Bwana Mwenye Nguvu Zote,

Mungu wa Israeli,

“hakika Moabu itakuwa kama Sodoma,

Waamoni kama Gomora:

mahali pa magugu na mashimo ya chumvi,

nchi ya ukiwa milele.

Mabaki ya watu wangu watawateka nyara;

mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”

102:10 Ay 40:12; Isa 16:6; Yer 48:27; Za 9:6Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao,

kwa kutukana na kudhihaki

watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.

112:11 Mwa 49:10; 10:5; Za 2:8; 22:27; Isa 2:2, 3; Mal 1:11; Yn 4:21; 1Tim 2:8; Yoe 2:11; 1Nya 19:1; Eze 25:6-7; Isa 12:4; Za 86:9; Sef 3:9Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao

atakapoangamiza miungu yote ya nchi.

Mataifa katika kila pwani yatamwabudu,

kila moja katika nchi yake.

Dhidi Ya Kushi

122:12 Mwa 10:6; Isa 18:1; 20:4; Yer 46:10“Ninyi pia, ee Wakushi,

mtauawa kwa upanga wangu.”

Dhidi Ya Ashuru

132:13 Mwa 10:5-11; Zek 10:11; Mik 5:6Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini

na kuangamiza Waashuru,

akiiacha Ninawi ukiwa

na pakame kama jangwa.

142:14 Isa 5:17; 13:21; 14:23; Ufu 18:2; Za 102:6Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale,

viumbe vya kila aina.

Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba

wataishi juu ya nguzo zake.

Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani,

kifusi kitakuwa milangoni,

boriti za mierezi zitaachwa wazi.

152:15 Isa 32:9; 47:8; Eze 27:36; 28:2; Ufu 18:7; Yer 49:33; Nah 3:19Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha

wakijisikia salama.

Ulisema moyoni mwako,

“Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.”

Jinsi gani umekuwa gofu,

mahali pa kulala wanyama pori!

Wote wanaopita kando yake wanauzomea

na kutikisa mkono kwa dharau.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

西番雅書 2:1-15

呼籲百姓悔改

1-2不知羞恥的國民啊,

趁命令尚未發出、

日子尚未消逝如風中的糠秕、

耶和華的烈怒尚未臨到你們、

祂向你們發怒的日子尚未來臨,

要聚集,聚集起來!

3世上所有遵守耶和華典章的謙卑人啊,

要尋求耶和華,追求公義,追求謙卑。

也許在耶和華發怒的日子,

你們可以得到庇護。

審判以色列的鄰國

4迦薩必被拋棄,

亞實基倫必淪為廢墟,

亞實突的居民必在中午被趕走,

以革倫必被連根拔除。

5住在海邊的基利提人啊,

你們有禍了!

非利士人的迦南啊,

耶和華宣告要毀滅你,

使你杳無人煙。

6沿海地區必成為草場,

有牧人的居所和羊圈。

7那裡必歸給猶大家的餘民,

他們必在那裡放牧,

晚上睡在亞實基倫的房屋裡,

因為他們的上帝耶和華必眷顧他們,

使他們回歸故土。

8-9以色列的上帝——萬軍之耶和華說:

「我聽見了摩押人的譭謗和亞捫人的辱罵。

他們譭謗我的子民,揚言侵佔他們的土地。

我憑自己的永恆起誓,

摩押亞捫必刺草叢生、鹽坑遍地、永遠荒廢,

所多瑪蛾摩拉一樣。

我餘下的子民必擄掠他們,

我倖存的百姓必承受他們的土地。」

10這是他們的報應,

因為他們狂妄自大,

羞辱萬軍之耶和華的子民。

11耶和華必令他們恐懼,

因為祂要削弱世上的神明。

天下萬民必在本地敬拜祂。

12古實人啊,

你們也必死在耶和華的刀下。

13祂必伸手攻擊北方,毀滅亞述

使尼尼微一片荒涼,

如乾旱的曠野。

14牲畜和野獸必躺臥在那裡,

貓頭鷹和刺蝟棲身在房柱上,

窗口傳出鳥鳴,

門庭都必破敗,

露出香柏木梁。

15這就是那歡樂安逸、

自以為天下無雙的城,

現在竟然如此荒涼,

成為野獸棲息之地!

路過的人都搖手嘲笑它。