11:1 2Fal 22:1; 2Tim 3:16; 2Pet 1:21; 1Nya 3:14Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
Onyo La Maangamizi Yanayokuja
21:2 Mwa 6:7Bwana asema,
“Nitafagia kila kitu
kutoka kwenye uso wa dunia.”
31:3 Yer 4:25; 50:3; Hos 4:3; Eze 14:17“Nitafagilia mbali watu na wanyama;
nitafagilia mbali ndege wa angani
na samaki wa baharini.
Wafanyao maovu watapata tu kokoto,
nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,”
asema Bwana.
Dhidi Ya Yuda
41:4 Yer 6:12; 15:6; Mik 5:13; Sef 2:11; Hos 10:5“Nitaiadhibu Yuda
na wote wakaao Yerusalemu.
Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali
kila mabaki ya Baali,
majina ya wapagani na makuhani
waabuduo sanamu:
51:5 Yer 5:7; 8:2; 1Fal 11:33; Law 18:21wale ambao husujudu juu ya mapaa
kuabudu jeshi la vitu vya angani,
wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana
na ambao pia huapa kwa Malkamu,
61:6 Yer 2:13; Isa 9:13; Hos 7:7wale wanaoacha kumfuata Bwana,
wala hawamtafuti Bwana
wala kutaka shauri lake.
71:7 Isa 13:6; 41:1; Eze 7:19; Yoe 3:14; Amo 5:18-20; Yer 46:10Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi,
kwa maana siku ya Bwana iko karibu.
Bwana ameandaa dhabihu,
amewaweka wakfu wale aliowaalika.
81:8 Isa 24:21; Yer 39:6Katika siku ya dhabihu ya Bwana
nitawaadhibu wakuu
na wana wa mfalme
na wale wote wanaovaa
nguo za kigeni.
91:9 1Sam 5:5; Amo 3:10Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao
hukwepa kukanyaga kizingiti,
ambao hujaza hekalu la miungu yao
kwa dhuluma na udanganyifu.”
101:10 Isa 22:5; Neh 3:13; 2Nya 33:14; Amo 5:16Bwana asema, “Katika siku hiyo
kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki,
maombolezo kutoka mtaa wa pili,
na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
111:11 Yak 5:1; Hos 9:6; Ufu 18:11, 12Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni;
wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa,
wote ambao wanafanya biashara ya fedha
wataangamizwa.
121:12 Amo 6:1; Ay 21:15; Za 10:11-13; Yer 48:11; Eze 8:12; 2Fal 21:16; Ay 22:13Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa,
na kuwaadhibu wale ambao
wanakaa katika hali ya kuridhika,
ambao ni kama divai
iliyobaki kwenye machicha,
ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote,
jema au baya.’
131:13 2Fal 24:13; Yer 15:13; Mik 6:15; Kum 28:30-39; Mao 5:2; Amo 5:11Utajiri wao utatekwa nyara,
nyumba zao zitabomolewa.
Watajenga nyumba,
lakini hawataishi ndani yake;
watapanda mizabibu
lakini hawatakunywa divai yake.
Siku Kubwa Ya Bwana
141:14 Yer 30:7; Ufu 6:17; Yoe 1:15; 2:1; Mal 4:5; Eze 7:7; Dan 7:13“Siku kubwa ya Bwana iko karibu:
iko karibu na inakuja haraka.
Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana
kitakuwa kichungu,
hata shujaa atapiga kelele.
151:15 1Sam 2:9; Mk 13:24-25; Yoe 2:2Siku ile ni siku ya ghadhabu,
siku ya fadhaa na dhiki,
siku ya uharibifu na ukiwa,
siku ya giza na utusitusi,
siku ya mawingu na giza nene,
161:16 Yer 4:19; 8:16; Hos 5:8; Amo 3:6; Kum 28:52; Isa 2:15siku ya tarumbeta na mlio wa vita
dhidi ya miji yenye ngome
na dhidi ya minara mirefu.
171:17 Kum 28:52; Isa 59:10; Yer 9:22; Za 79:3; 83:10Nitawaletea watu dhiki,
nao watatembea kama vipofu,
kwa sababu wametenda dhambi
dhidi ya Bwana.
Damu yao itamwagwa kama vumbi
na matumbo yao kama taka.
181:18 Ay 20:20; 40:11; Eze 7:11; 7:19; Kum 29:20; Sef 3:8; Mwa 6:7Fedha yao wala dhahabu yao
hazitaweza kuwaokoa
katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana.
Katika moto wa wivu wake
dunia yote itateketezwa,
kwa maana ataleta mwisho
wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
1猶大王亞們的兒子約西亞執政期間,耶和華對希西迦的玄孫、亞瑪利亞的曾孫、基大利的孫子、古示的兒子西番雅說:
耶和華審判的日子
2「我必毀滅地上的一切。
這是耶和華說的。
3我必毀滅人類、獸類、
天上的鳥和海裡的魚。
我必使惡人倒斃,
我必剷除地上的人類。
這是耶和華說的。
4「我必伸手攻擊猶大,
以及所有住在耶路撒冷的人,
剷除巴力的餘跡及拜偶像之祭司的名號。
5我必剷除那些在屋頂祭拜天上萬象的人,
剷除敬拜我、憑我起誓又憑米勒公起誓的人,
6剷除離棄我、不尋求我、不求問我的人。」
7要在主耶和華面前肅靜,
因為耶和華的日子近了。
耶和華已準備好祭物,
潔淨了祂邀請的人。
8耶和華說:「在我獻祭的日子,
我必懲罰首領和王子,
以及所有穿外族服裝的人。
9到那日,我必懲罰所有跳過門檻1·9 「跳過門檻……的人」指祭拜偶像的人,參見撒母耳記上5·5。、
使主人的家充滿暴力和欺詐的人。
10到那日,魚門必傳出哭喊聲,
新區必響起哀號聲,
山陵必發出崩裂的巨響。
這是耶和華說的。
11市場區的居民啊,哀哭吧!
因為所有的商人必滅亡,
所有做買賣的必被剷除。
12那時,我必提著燈巡查耶路撒冷,
懲罰那些安於罪中的人。
他們心想,『耶和華不賜福也不降禍。』
13他們的財物必遭搶掠,
家園必淪為廢墟。
他們建造房屋,卻不能住在裡面;
栽種葡萄園,卻喝不到葡萄酒。
14「耶和華的大日子近了,
近了,很快就到了。
那將是痛苦的日子,
勇士也必淒聲哀號。
15那是降烈怒的日子,
是困苦艱難的日子,
是摧殘毀壞的日子,
是黑暗幽冥的日子,
是陰霾密佈的日子,
16是吹號呐喊、
攻打堅城高壘的日子。
17「我要使人們災難臨頭,
以致他們行路像瞎子,
因為他們得罪了我。
他們的血必被倒出,如同灰塵;
他們的屍體必被丟棄,如同糞便。
18在耶和華發怒的日子,
他們的金銀救不了他們。
祂的怒火必吞噬大地,
祂必驟然毀滅一切世人。」