Mwanzo 33 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 33:1-20

Yakobo Akutana Na Esau

133:1 Mwa 32:6Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike. 2Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma. 333:3 Mwa 42:6Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.

4Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia. 533:5 Za 127:3; Isa 8:18Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?”

Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”

6Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu. 7Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.

833:8 Mwa 24:9; 32:14-16Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?”

Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”

933:9 Mwa 13:6Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”

1033:10 Mwa 16:13Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa. 1133:11 1Sam 25:27Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.

12Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”

1333:13 Isa 40:11Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa. 1433:14 Kut 12:38Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”

1533:15 Mwa 32:5Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.”

Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”

1633:16 Mwa 14:6Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri. 1733:17 Amu 8:5, 6, 8, 14-16Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi,33:17 Sukothi maana yake Vibanda. mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.

1833:18 Mwa 12:6Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji. 1933:19 Yos 24:32; Yn 4:5Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake. 20Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.33:20 El-Elohe-Israeli maana yake Mungu, Mungu wa Israeli au Mwenye Nguvu ni Mungu wa Israeli.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 33:1-20

弟兄重逢

1雅各抬頭看見以掃帶著四百人迎面而來,便把孩子們分別交給利亞拉結和兩個婢女, 2又讓兩個婢女和她們的孩子走在前面,利亞和她的孩子跟在後面,拉結約瑟走在最後。 3他自己則走在他們前面,接連俯伏下拜七次,直到他哥哥跟前。

4以掃跑上去迎接他,擁抱他,親吻他,二人抱頭痛哭。 5以掃抬眼看見跟在雅各後面的婦女和孩子,就問:「這些和你同行的是誰?」雅各說:「這些孩子是上帝施恩賜給你僕人的。」 6雅各的兩個婢女和她們的孩子上前下拜, 7利亞和她的孩子也上前下拜,最後約瑟拉結也上前向以掃下拜。

8以掃說:「我在路上遇見的那一群群牲畜是怎麼回事?」雅各回答說:「我帶來這些是想在我主面前蒙恩。」 9以掃說:「弟弟,我已經有很多了,你自己留著吧!」 10雅各說:「不,你若賞臉,就請收下!我見了你的面就像見了上帝的面,因為你這樣善待我。 11請你收下我的禮物吧,因為上帝恩待了我,使我富足。」雅各再三懇求,以掃才收下。

12以掃說:「我們走吧!我陪你們走。」 13雅各卻說:「我主知道孩子們還幼小,而且,我還要照料正在哺乳的牛羊,如果整天趕路,牛羊都會累死。 14請我主先走,我遷就牲畜和孩子的腳步慢慢走,我在西珥與我主會合。」

15以掃說:「我給你留幾個隨從吧。」雅各說:「不用了,能得到我主的恩待就夠了。」 16於是,以掃在當天先回西珥去了, 17雅各卻去了疏割,在那裡為自己建造房屋,為牲畜搭起棚子。因此那地方叫疏割33·17 「疏割」意思是「棚子」。

18這樣,雅各巴旦·亞蘭平安地回到迦南示劍城,在城外搭營居住。 19他搭營居住的這塊地是他用一百塊銀子向示劍的父親哈抹的子孫買的。 20雅各在那裡築了一座壇,稱之為伊利·伊羅伊·以色列33·20 「伊利·伊羅伊·以色列」意思是「以色列的上帝」。