Matendo 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Matendo 1:1-26

Kanisa La Kwanza

(1:1–5:42)

Ahadi Ya Roho Mtakatifu

11:1 Lk 1:14; 3:23Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo, 21:2 Mk 16:19; 6:30; Mt 28:19-20; 10:1-4; Yn 13:18hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua. 31:3 1Kor 15:5-7; Mt 28:17; Lk 24:39-43Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu. 41:4 Lk 24:49; Yn 14:16; Mdo 2:33Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake. 51:5 Mk 1:4, 8; Mt 3:11; Mdo 11:16; 19:4; Yoe 3:18; Mdo 2:4; 11:15Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”

Yesu Apaa Mbinguni

(Marko 16:19-20; Luka 24:50-53)

61:6 Mt 17:11; Mdo 3:21; Lk 24:21; Isa 1:26; Dan 7:27; Amo 9:11Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”

71:7 Za 102:13; Mt 24:48Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. 81:8 Mdo 2:1-4; Lk 24:48Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”

91:9 Mk 16:19; Lk 24:51; Yn 6:62Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.

101:10 Lk 24:4; Yn 20:12; Mt 28:3; Mk 16:5; Mdo 10:3, 30Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao, 111:11 Mdo 2:7; Mt 16:27; Lk 21:27; 1Tim 3:16; Mdo 1:7wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”

Mathiya Achaguliwa Badala Ya Yuda

(Mathayo 27:3-10)

121:12 Lk 24:52; Mt 21:1Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato1:12 Mwendo wa Sabato hapa ina maana umbali wa mita 1,100. kutoka mjini. 131:13 Mdo 9:37; 20:8; Mt 10:2-4; Mk 3:16-19Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote1:13 Zelote hapa ina maana alikuwa mwanachama wa Wazelote, kikundi cha Kiyahudi cha kupinga jeuri ya Warumi. na Yuda mwana wa Yakobo. 141:14 Lk 18:1; 23:49-55; Mt 12:46Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.

151:15 Ufu 3:4Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema, 161:16 Mt 10:4; Yn 13:18“Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu. 171:17 Yn 6:70-71; Mt 10:4; Lk 6:16; Mdo 12:25; 20:24; 21:19Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”

181:18 Mt 26:14-15; 27:3-10(Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje. 191:19 Yn 5:2Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).

201:20 Za 69:25; 109:8“Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi,

“ ‘Mahali pake na pawe ukiwa,

wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’

na,

“ ‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’

211:21 Yn 15:27Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu, 221:22 Mk 1:4; Lk 24:48kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”

231:23 Mdo 15:22Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya. 241:24 Mdo 13:3; 14:23; 1Sam 16:7; Ufu 2:23Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua 251:25 Mdo 1:17ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.” 261:26 Mdo 2:14Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

使徒行傳 1:1-26

應許聖靈降臨

1提阿非羅啊,在前一封信中,我從耶穌的生平和教導開始, 2一直談到祂藉著聖靈吩咐了自己所選立的使徒,然後被接回天上。 3祂受難後用許多確據向使徒顯明自己活著,在四十天之內屢次向他們顯現,並談論上帝的國。 4有一次,耶穌和他們在一起吃飯的時候,叮囑他們:「你們不要離開耶路撒冷,要在那裡等候我對你們說過的天父的應許。 5因為從前約翰用水施洗,但過不了多少天,你們要受聖靈的洗。」

6他們跟耶穌在一起的時候問祂:「主啊,你要在這時候復興以色列國嗎?」 7耶穌回答說:「天父照自己的權柄定下的時間、日期不是你們可以知道的。 8但聖靈降臨在你們身上後,你們必得到能力,在耶路撒冷猶太全境和撒瑪利亞,直到地極,作我的見證人。」

9耶穌說完這些話,就在他們注視下被提升天,被一朵雲彩接去,離開了他們的視線。 10祂上升時,他們都定睛望著天空,忽然有兩個身穿白衣的人站在他們身旁, 11說:「加利利人啊!你們為什麼站在這裡望著天空呢?這位離開你們被接到天上的耶穌,你們看見祂怎樣升天,將來祂還要怎樣回來。」

選立新使徒

12於是,他們從橄欖山回到耶路撒冷。橄欖山距離耶路撒冷不遠,約是安息日允許走的路程1·12 按猶太人的傳統,在安息日只能走約一公里遠。13他們進城後,來到樓上所住的房間。當時有彼得約翰雅各安得烈腓力多馬巴多羅買馬太亞勒腓的兒子雅各、激進黨人西門雅各的兒子猶大14他們同幾個婦女,以及耶穌的弟弟們和母親瑪麗亞在一起同心合意地恆切禱告。

15那時,約有一百二十人在聚會,彼得從他們當中站起來說: 16「弟兄們,關於帶人抓耶穌的猶大,聖靈藉著大衛的口早已預言,這經文必須要應驗。 17猶大原本是我們中間的一員,與我們同擔使徒的職分。」

18他用作惡得來的錢買了一塊田,他頭朝下栽倒在地,肚破腸流。 19這消息很快傳遍了耶路撒冷,當地人稱那塊田為「亞革大馬」,就是「血田」的意思。

20彼得繼續說:「詩篇上寫道,『願他的家園一片荒涼,無人居住』1·20 詩篇69·25,又說,『願別人取代他的職位。』1·20 詩篇109·8 21-22所以,我們必須另選一個人代替猶大,與我們一同為主耶穌的復活作見證。他必須是從主耶穌接受約翰的洗禮起一直到主升天,始終與我們在一起的人。」

23於是他們推薦兩個人:別號巴撒巴又叫猶士都約瑟馬提亞24-25大家便禱告說:「主啊!你洞悉每個人的內心,求你指明這二人中你選了誰來擔負使徒的職分。猶大丟棄了這職分,去了他該去的地方。」 26然後,他們抽籤,抽中了馬提亞,就把他加到十一位使徒的行列。