Matendo 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 2:1-47

Kushuka Kwa Roho Mtakatifu

12:1 Law 23:15-16; 1Kor 16:18; Mdo 1:14Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja. 22:2 Mdo 4:31Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi. 32:3 Mt 3:11Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao. 42:4 Mk 16:17; 1Kor 12:10Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.

52:5 Lk 2:25; Mdo 8:2Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu. 6Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 72:7 Mdo 1:11Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya? 8Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa? 92:9 Mdo 18:2; 1Pet 1:1; 2Kor 1:8; Ufu 1:4Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia, 102:10 Mdo 16:6; 18:23; 14:24; Mt 27:32Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi, 11Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.” 12Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”

132:13 1Kor 14:23; Efe 5:18Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”

Petro Ahutubia Umati

14Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize. 152:15 1The 5:7Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi! 162:16 Yoe 2:28-32La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:

172:17 Eze 39:29; Yn 7:37-39; Mdo 21:9“ ‘Katika siku za mwisho, asema Mungu,

nitamimina Roho wangu

juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu na binti zenu watatabiri,

vijana wenu wataona maono,

na wazee wenu wataota ndoto.

182:18 Mdo 21:9-12; 1Kor 12:10, 28; 14:1Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho wangu,

nao watatabiri.

192:19 Yoe 2:30, 31; Lk 21:11Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni,

na ishara chini duniani:

damu, moto, na mawimbi ya moshi.

202:20 Mt 24:29Jua litakuwa giza

na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,

kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana

iliyo tukufu.

212:21 Yoe 2:28-32; Rum 10:13Na kila mtu atakayeliitia

jina la Bwana, ataokolewa.’

222:22 Yn 4:48; Mdo 10:38; Yn 3:2“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo. 232:23 Isa 53:10; Lk 22:22; 24:20; Mt 16:21Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani. 242:24 Rum 8:11; Ebr 13:20; Yn 20:9Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti. 252:25 Za 16:8Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye:

“ ‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima.

Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,

sitatikisika.

26Kwa hiyo moyo wangu unafurahia,

na ulimi wangu unashangilia;

mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.

272:27 Mdo 13:35Kwa maana hutaniacha kaburini,

wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.

282:28 Za 16:8-11Umenionyesha njia za uzima,

utanijaza na furaha mbele zako.’

292:29 Mdo 7:8-9; 1Fal 2:10; Neh 3:16“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo. 302:30 2Sam 7:12; Mt 1:1; Za 132:11; Lk 1:32, 69; Rum 1:3; 2Tim 2:8Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi. 312:31 Za 16:10; Mdo 13:35Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo,2:31 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. 322:32 Mdo 1:8; 2:24; Lk 24:48Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo. 332:33 Flp 2:9; Mk 16:19; Yn 14:26; Mdo 10:45; Yn 15:26Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia. 342:34 Za 110:1; Mt 22:44; 1Kor 15:25; Efe 1:20; Ebr 1:13Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema,

“ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu:

“Keti mkono wangu wa kuume,

352:35 Za 110:1; Mt 22:44hadi nitakapowaweka adui zako

chini ya miguu yako.” ’

362:36 Lk 2:11; Mdo 5:31; Mt 28:18“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”

Waumini Waongezeka

372:37 Lk 3:10-14; Mdo 16:30Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”

382:38 Mdo 22:16; Kol 2:12; Yer 36:3Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 392:39 Isa 44:3; 66:23; 57:19; Efe 2:13Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”

402:40 Kum 32:5; Flp 2:15Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.” 412:41 Mdo 2:47; 4:4; 5:14; 9:31, 35, 42; 11:21, 24; 14:1, 21Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.

Ushirika Wa Waumini

422:42 Mdo 1:14Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali. 432:43 Mdo 5:12Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume. 442:44 Mdo 4:32Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika. 452:45 Mt 19:21; Lk 12:33Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake. 462:46 Lk 24:53; Mdo 3:1; 20:7; Mt 14:19Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe, 472:47 Rum 14:18; Mdo 5:14wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 2:1-47

聖靈降臨

1五旬節那天,門徒聚集在一起。 2忽然,天上發出一陣響聲,好像狂風呼嘯而過,充滿了他們所在的房子, 3又有火焰般的舌頭顯現出來,分別落在各人的頭上。 4大家都被聖靈充滿,得到聖靈所賜的才能,說起別的語言來。

5當時耶路撒冷住著從各國回來的虔誠的猶太人。 6眾人聽見這陣響聲便趕過來,聽見門徒在說他們各自的語言,都十分納悶, 7驚詫地說:「看啊!這些說話的不都是加利利人嗎? 8怎麼會說我們各自的語言呢? 9我們這裡有帕提亞人、瑪代人、以攔人,以及住在美索不達米亞猶太加帕多迦本都亞細亞10弗呂迦旁非利亞埃及和靠近古利奈利比亞的人,還有從羅馬來的猶太人和改信猶太教的人、 11克里特人和阿拉伯人。我們都聽見他們在用我們各自的語言訴說上帝的偉大!」 12他們都大感驚奇和困惑,彼此議論說:「這到底是怎麼回事?」

13有些人就譏笑說:「他們不過是被新酒灌醉了!」

彼得講道

14彼得和其他十一位使徒都站起來,他大聲對眾人說:「各位猶太同胞和住在耶路撒冷的人啊,請留心聽!我告訴你們這是怎麼回事。 15你們以為這些人是醉了,其實不是,因為現在才早上九點鐘。 16你們眼前看見的正是先知約珥所說的,

17『上帝說,在末後的日子,

我要將我的靈澆灌所有的人,

你們的兒女要說預言,

青年要見異象,

老人要做異夢。

18那時,我要將我的靈澆灌我的奴僕和婢女,

他們都要說預言。

19在天上,我要顯異兆;

在地上,我要行神蹟,有血、有火、有濃煙。

20太陽要變得昏暗,

月亮要變得血紅。

這都要發生在主偉大榮耀的日子來臨以前。

21那時,凡求告主名的,都必得救。』

22「各位以色列人啊,請留心聽。上帝藉著拿撒勒人耶穌在你們中間行了異能、奇事和神蹟,以證明拿撒勒人耶穌是祂派來的。這是你們都知道的。 23上帝照著自己的計劃和預知把耶穌交在你們手裡,你們藉著邪惡之人的手把祂釘死在十字架上了。 24但上帝為祂解除了死亡的痛苦,使祂從死裡復活,因為祂不可能被死亡拘禁。 25論到耶穌,大衛曾說,

『我看見主常在我面前,

祂在我右邊,我必不動搖。

26因此我的心歡喜,我的口頌讚,

我的身體也要活在盼望中。

27因為你不會把我的靈魂撇在陰間,

也不會讓你的聖者身體朽壞。

28你已把生命之路指示我,

叫我在你面前充滿喜樂。』

29「弟兄們,我肯定地對你們說,先祖大衛死了,埋葬了,他的墳墓至今還在這裡。 30大衛是先知,知道上帝曾起誓要從他的後裔中選立一人繼承他的王位。 31他預先知道這事,講到基督的復活,說,『祂的靈魂不會被撇在陰間,祂的身體也不會朽壞』。 32上帝已經使這位耶穌復活了!我們都是這件事的見證人。 33現在祂升到上帝的右邊,從天父領受了所應許的聖靈,並將聖靈澆灌下來,你們今天也耳聞目睹了。 34大衛並沒有升到天上,但他曾說,

『主對我主說,

你坐在我的右邊,

35等我使你的仇敵成為你的腳凳。』

36「所以,全體以色列人啊!你們應當確實地知道,上帝已經立這位被你們釘在十字架上的耶穌為主,為基督了。」

37他們聽了彼得的話,覺得扎心,就對彼得和其他使徒說:「弟兄們,我們該怎麼辦呢?」 38彼得說:「你們每一個人都要悔改,奉耶穌基督的名受洗,使你們的罪得到赦免,你們就必領受上帝所賜的聖靈。 39因為這應許是給你們和你們的兒女,以及遠方的人,就是所有被主——我們的上帝呼召的人。」

40然後,彼得還講了許多話警戒、勸勉他們,說:「你們要保守自己脫離這邪惡的世代。」

41結果,那天約有三千人相信了他傳的道,接受了洗禮。 42他們都一心遵守使徒的教導,一起團契、掰餅、禱告。

43大家都滿心敬畏上帝。使徒又行了很多神蹟奇事。 44信徒聚在一起,共用所有的東西。 45他們把田產家業變賣了,按照各人的需要把錢分給大家。 46他們天天同心合意地聚集在聖殿裡敬拜上帝,又在各人家中擘餅聚會,以歡喜、慷慨的心分享食物, 47讚美上帝,受到眾人的喜愛。主使得救的人數與日俱增。