Kumbukumbu 31 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 31:1-30

Yoshua Kutawala Baada Ya Mose

(Hesabu 27:12-23)

1Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote: 231:2 Kut 7:7; Hes 27:17; Kum 34:7; 1Fal 3:7; Kum 3:23-26“Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’ 331:3 Hes 27:18; Kum 9:3; 7:1; 3:28Bwana Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema. 431:4 Hes 21:33Naye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao. 531:5 Kum 2:33; 7:2Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru. 631:6 Yos 1:6-9, 18; 10:23; 1Nya 22:13; 28:20; 2Nya 32:7; Yer 1:8, 17; Eze 2:6; Mwa 28:15; Kum 1:29; 20:4; Mt 28:20; Za 56:9; 118:6; Kum 4:31; 1Sam 12:22; 1Fal 6:13; Za 94:14; Isa 41:17; Ebr 13:5Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”

731:7 Hes 27:23; Yos 1:6; Kum 1:38; 3:28Kisha Mose akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ile Bwana aliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao. 831:8 Kut 13:21; Mwa 28:15; Kut 33:14; Kum 4:31Bwana mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”

Kusoma Sheria

931:9 Kut 17:14; Hes 4:15; 1Nya 15:2Kwa hiyo Mose akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano la Bwana na wazee wote wa Israeli. 1031:10 Kum 15:1; Kut 23:16; Kum 16:13; Law 23:34Kisha Mose akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda, 1131:11 Kum 16:16; 12:5; Yos 8:34-35; 2Fal 23:2; Neh 8:2Waisraeli wote wanapokuja mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao. 1231:12 Kum 4:10; Hag 1:12; Mal 1:6; 3:5, 16Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu na kufuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii. 1331:13 Kum 11:2; Za 78:6-7; Mit 22:6; Efe 6:4Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”

Kuasi Kwa Waisraeli Kunatabiriwa

1431:14 Mwa 25:8; Hes 27:13; 23; Kum 34:9; Yos 1:1-9; Hes 27:19; Kut 33:9-11Bwana akamwambia Mose, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Mose na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.

1531:15 Kut 33:9; Za 99:7Kisha Bwana akatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema. 1631:16 Mwa 15:15; Kut 34:15; Kum 4:25-28; Amu 2:12; 10:6-13; 1Fal 9:9; 18:18; 19:10; Yer 2:13; 5:19; 19:4; 2Sam 7:12; 2Fal 22:16, 17; Isa 1:4Kisha Bwana akamwambia Mose: “Unakwenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja Agano nililofanya nao. 1731:17 Kum 32:16; Amu 2:14; 20; 10:7; 2Fal 13:3; 22:13; Za 106:29, 40; Yer 7:18; 21:5; 36:17; Amu 6:13; 2Nya 15:2; 24:20; Ezr 8:22; Za 44:9; Isa 2:6; Kum 32:20; Isa 1:15; 45:15; 53:3; 54:8; Ay 13:24; Za 13:1; 27:9; 30:7; 104:29; Isa 50:6; Yer 33:5; Eze 39:29; Mik 3:4; Yer 4:20; Eze 7:26; Hes 14:42; Hos 9:12Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’ 18Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.

1931:19 Mwa 31:50“Sasa ujiandikie wimbo huu,31:19 Wimbo huu hapa ina maana wimbo wa Mose. uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao. 2031:20 Kum 6:10-12; Za 4:2; 16:4; 40:4; Yer 13:25; Dan 3:28; Amo 2:4; Kum 8:19; 11:16-17Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja Agano langu. 2131:21 Kum 4:30; 1Nya 28:9; Hos 5:3; Yn 2:24-25Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.” 22Hivyo Mose akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.

2331:23 Yos 1:6Bwana akampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”

2431:24 Kum 17:18; 2Fal 22:8; Kum 28:58Baada ya Mose kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho, 25akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Bwana agizo hili, akawaambia: 26“Chukueni Kitabu hiki cha Sheria mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu. 2731:27 Kut 23:21; 32:9; Kum 9:27; 2Nya 30:8; Za 78:8; Isa 48:4; Za 32Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Bwana nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu! 2831:28 Kum 4:26; 30:19; 32:1; Ay 20:27; Isa 26:21Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao. 2931:29 Kum 4:16; Ufu 9:20; 1Fal 9:9; 22:23; 2Fal 22:16Kwa kuwa ninajua baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata kwa sababu mtafanya maovu mbele ya macho ya Bwana, na kuchochea hasira yake kwa yale mikono yenu itakayokuwa imefanya.”

Wimbo Wa Mose

30Mose akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:

New International Version

Deuteronomy 31:1-30

Joshua to Succeed Moses

1Then Moses went out and spoke these words to all Israel: 2“I am now a hundred and twenty years old and I am no longer able to lead you. The Lord has said to me, ‘You shall not cross the Jordan.’ 3The Lord your God himself will cross over ahead of you. He will destroy these nations before you, and you will take possession of their land. Joshua also will cross over ahead of you, as the Lord said. 4And the Lord will do to them what he did to Sihon and Og, the kings of the Amorites, whom he destroyed along with their land. 5The Lord will deliver them to you, and you must do to them all that I have commanded you. 6Be strong and courageous. Do not be afraid or terrified because of them, for the Lord your God goes with you; he will never leave you nor forsake you.”

7Then Moses summoned Joshua and said to him in the presence of all Israel, “Be strong and courageous, for you must go with this people into the land that the Lord swore to their ancestors to give them, and you must divide it among them as their inheritance. 8The Lord himself goes before you and will be with you; he will never leave you nor forsake you. Do not be afraid; do not be discouraged.”

Public Reading of the Law

9So Moses wrote down this law and gave it to the Levitical priests, who carried the ark of the covenant of the Lord, and to all the elders of Israel. 10Then Moses commanded them: “At the end of every seven years, in the year for canceling debts, during the Festival of Tabernacles, 11when all Israel comes to appear before the Lord your God at the place he will choose, you shall read this law before them in their hearing. 12Assemble the people—men, women and children, and the foreigners residing in your towns—so they can listen and learn to fear the Lord your God and follow carefully all the words of this law. 13Their children, who do not know this law, must hear it and learn to fear the Lord your God as long as you live in the land you are crossing the Jordan to possess.”

Israel’s Rebellion Predicted

14The Lord said to Moses, “Now the day of your death is near. Call Joshua and present yourselves at the tent of meeting, where I will commission him.” So Moses and Joshua came and presented themselves at the tent of meeting.

15Then the Lord appeared at the tent in a pillar of cloud, and the cloud stood over the entrance to the tent. 16And the Lord said to Moses: “You are going to rest with your ancestors, and these people will soon prostitute themselves to the foreign gods of the land they are entering. They will forsake me and break the covenant I made with them. 17And in that day I will become angry with them and forsake them; I will hide my face from them, and they will be destroyed. Many disasters and calamities will come on them, and in that day they will ask, ‘Have not these disasters come on us because our God is not with us?’ 18And I will certainly hide my face in that day because of all their wickedness in turning to other gods.

19“Now write down this song and teach it to the Israelites and have them sing it, so that it may be a witness for me against them. 20When I have brought them into the land flowing with milk and honey, the land I promised on oath to their ancestors, and when they eat their fill and thrive, they will turn to other gods and worship them, rejecting me and breaking my covenant. 21And when many disasters and calamities come on them, this song will testify against them, because it will not be forgotten by their descendants. I know what they are disposed to do, even before I bring them into the land I promised them on oath.” 22So Moses wrote down this song that day and taught it to the Israelites.

23The Lord gave this command to Joshua son of Nun: “Be strong and courageous, for you will bring the Israelites into the land I promised them on oath, and I myself will be with you.”

24After Moses finished writing in a book the words of this law from beginning to end, 25he gave this command to the Levites who carried the ark of the covenant of the Lord: 26“Take this Book of the Law and place it beside the ark of the covenant of the Lord your God. There it will remain as a witness against you. 27For I know how rebellious and stiff-necked you are. If you have been rebellious against the Lord while I am still alive and with you, how much more will you rebel after I die! 28Assemble before me all the elders of your tribes and all your officials, so that I can speak these words in their hearing and call the heavens and the earth to testify against them. 29For I know that after my death you are sure to become utterly corrupt and to turn from the way I have commanded you. In days to come, disaster will fall on you because you will do evil in the sight of the Lord and arouse his anger by what your hands have made.”

The Song of Moses

30And Moses recited the words of this song from beginning to end in the hearing of the whole assembly of Israel: