Kumbukumbu 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 3:1-29

Kushindwa Kwa Ogu Mfalme Wa Bashani

(Hesabu 21:31-35)

13:1 Hes 21:33; 32:19Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei. 23:2 Yos 10:8; 2Fal 19:6; Isa 7:4Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”

33:3 Hes 21:24; 21:35Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja. 43:4 Hes 21:24, 33; 1Fal 4:13Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani. 5Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta. 63:6 Kum 2:24; Za 135:10-12; 136:19-21Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto. 73:7 Kum 2:35Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.

83:8 Hes 32:33; Yos 13:8-12; Kum 4:48; Yos 11:3; 12:1; 13:5; Amu 3:3; 1Nya 5:23; Za 42:6; 89:12; 133:3; Wim 4:8Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni. 93:9 Za 29:6; 89:12; 1Nya 5:23; Wim 4:8; Eze 27:5; Kum 4:48(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.) 103:10 Yos 12:5; 13:11; 1Nya 5:11; Kum 4:49Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani. 113:11 Mwa 14:5; Yos 13:25; 15:60; 2Sam 11:1; 12:26; 17:27; 1Nya 20:7; Yer 49:2; Eze 21:20; 25:5; Amo 1:14; 2:9(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa3:11 Dhiraa tisa ni sawa na mita 4. na upana wa dhiraa nne.3:11 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)

Mgawanyo Wa Nchi Mashariki Ya Yordani

(Hesabu 32:1-42)

123:12 Kum 2:36; Hes 32:32-38; Yos 13:8-13Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake. 133:13 Kum 29:8; Mwa 14:5Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai. 143:14 Hes 32:41; Yos 12:5; 13:11-13; 2Sam 10:6; 23:34; 2Fal 25:23; 1Nya 4:19; Yer 40:8; Yos 19:46-47; Za 49:11; 1Nya 2:22Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.) 153:15 Mwa 50:23; Hes 32:39-40Nikampa Makiri nchi ya Gileadi. 163:16 Hes 21:24; 2Sam 24:5; Hes 21:24Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni. 173:17 2Sam 2:29; 4:7; Eze 47:8; Hes 34:11; 14:3; Yos 12:3; 13:27Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.

183:18 Yos 1:13; Hes 32:17Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli. 193:19 Yos 1:14; Hes 32:16Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa, 203:20 Yos 22:4mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”

Mose Akatazwa Kuvuka Yordani

21Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo. 223:22 Kum 1:29; 7:18; 20:4; 31:6; 2Nya 32:8; Za 23:4; Isa 41:10; Kut 14:143:22 Yos 23:10Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”

233:23 Kum 1:37; 31:2; 32:52; 34:4Wakati huo nilimsihi Bwana: 243:24 Kum 5:24; 11:2; 32:3; Kut 8:10; Za 71:16; 86:8; 106:2; 145:12; 150:2; 2Sam 7:22; Neh 9:32; Yer 32:18-21; Kut 15:11“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe? 253:25 Kum 4:25; 1:7; Yos 1:4; 9:1; 11:17; 12:7; 13:5; Amu 3:3; 9:13; 1Fal 4:33Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”

263:26 Kum 1:37; 31:2Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena. 273:27 Hes 21:20; 27:12; Mwa 13:14; Hes 20:12; Kum 32:52Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani. 283:28 Hes 27:18-23; Kum 31:7; 1:38; 31:3-23Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.” 293:29 Hes 23:28; Kum 4:46; 34:6; Yos 13:20Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 3:1-29

击败巴珊王噩

1“之后,我们前往巴珊巴珊率全军在以得来迎战我们。 2耶和华对我说,‘不要怕他,因为我已把他及其众民和土地交在你手中,你要像从前对付希实本亚摩利西宏一样对付他。’

3“我们的上帝耶和华把巴珊及其众民交在我们手中,我们杀了他们,一个不留。 4我们占领了亚珥歌伯全境,即巴珊的所有城邑,共六十座。 5这些城邑围墙高耸,门闩牢固。我们还占领了许多没有城墙的乡村。 6像对付希实本西宏一样,我们将这些城邑夷为平地,城中的男女老幼一个不留, 7只留下牲畜和财物作战利品。 8于是,我们攻占了约旦河东两个亚摩利王的土地,从亚嫩谷一直到黑门山—— 9西顿人称黑门山为西连亚摩利人称之为示尼珥—— 10我们攻占了高原的城邑、整个基列巴珊,远至巴珊的城邑撒迦以得来11巴珊是最后一个利乏音人。他的床是铁做的,存放在亚扪人的拉巴城,长四米,宽一米八。

分配约旦河东之地

12“我们占领了这片土地后,我把亚嫩谷边的亚罗珥以北地区和基列山区的一半及其城邑,分给吕便支派和迦得支派, 13基列山区的另一半,以及的王国巴珊全境——整个亚珥歌伯分给玛拿西半个支派。巴珊地区又被称为利乏音人之地。 14玛拿西的子孙雅珥得到亚珥歌伯全境,远至基述人和玛迦人的边界。他按自己的名字给巴珊取名叫哈倭特·雅珥,沿用至今。 15我又把基列分给玛吉16把从基列亚嫩谷,以谷中央为界,远至亚扪人的边界雅博河地区,分给吕便支派和迦得支派。 17我还把亚拉巴,就是以约旦河为界,从基尼烈直到东面毗斯迦山脚的亚拉巴海,即盐海地区给了他们。

18“那时我吩咐他们说,‘你们的上帝耶和华已经把这些地方赐给你们,但你们所有的战士必须带着兵器过河,做以色列同胞的先锋。 19我知道你们有许多牲畜,你们的妻子、儿女和牲畜可以留在我分给你们的城邑。 20等你们的上帝耶和华使其他以色列人和你们一样有了安身之所,占领了耶和华赐给他们的约旦河西之地后,你们才可以返回我分给你们的家园。’ 21那时我吩咐约书亚说,‘你们的上帝耶和华怎样对付那两个王,你都亲眼看见了。耶和华必以同样的方式对付你将去攻占的各国。 22不要怕他们,因为你的上帝耶和华将为你们争战。’

摩西不得进入迦南

23“那时,我恳求耶和华,说, 24‘主耶和华啊,你已向仆人彰显你的伟大和权能,天上地下没有神明可与你的大能作为相比! 25求你让我过去看看约旦河那边的佳美之地,那美好的山区和黎巴嫩。’ 26但因你们的缘故,耶和华向我发怒,不听我的恳求,祂对我说,‘够了,不要再跟我提这件事。 27你可以上毗斯迦山顶,向东南西北眺望,亲眼看看那片土地,因为你不可过约旦河。 28你要委任约书亚,勉励他,支持他,因为他必带领以色列人过河,使他们承受你眺望的那片土地。’ 29当时,我们驻扎在伯·毗珥对面的谷中。