Kumbukumbu 20 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 20:1-20

Kwenda Vitani

120:1 Za 20:7; Isa 31:1; Hes 14:9; Kum 3:22; 1Sam 17:45; Isa 41:10; 2Nya 32:7-8; Hes 23:21; Kum 31:6, 8; 2Nya 13:12; 32:7, 8Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi. 2Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi. 320:3 1Sam 17:32; Ay 23:16; Za 22:14; Isa 7:4; 35:4; Yer 51:46Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao. 420:4 2Nya 20:14-22; Kut 14:14; 1Nya 5:22; Neh 4:20; Amu 12:3; 15:18; Za 44:7; 144:10; Kum 1:30Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”

520:5 Neh 12:27Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu. 620:6 Yer 31:5; Eze 28:26; Mik 1:6; 1Kor 9:7Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia. 720:7 Kum 24:5; Mit 5:18Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.” 820:8 Amu 7:3Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.” 9Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.

1020:10 Kum 2:26; Lk 14:31-32; 2Sam 20:18-20Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani. 1120:11 2Fal 6:22; 1Fal 9:21; 1Nya 22:2; Isa 31:7Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia. 12Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita. 1320:13 Hes 31:7Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake. 1420:14 Yos 8:2; 22:8; Hes 31:11; 31:53Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu. 1520:15 Yos 9:9Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.

1620:16 Kut 23:31-33; Hes 21:2-3; Kum 7:2; Yos 6:21; 10:1; 11:14Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua. 17Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru. 1820:18 Kut 34:16; 10:7; 23:33; Kum 12:30-31; Yos 23:12-13; 1Kor 15:33; 2Fal 21:3, 15; Za 106:34-41; Hos 8:11La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.

19Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire? 20Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 20:1-20

交战的条例

1“你们和敌人交战时,面对比你们强大的军队及战车战马,不要害怕,因为你们的上帝耶和华与你们同在,祂曾带你们出埃及2你们出战之前,祭司要上前鼓舞士气, 3说,‘以色列人啊,听着!今天你们要和敌人交战,不要胆小害怕,也不要惊慌失措。 4因为你们的上帝耶和华要与你们同去,为你们争战,使你们战胜仇敌。’ 5官长要对士兵说,‘你们谁建了新房子还没有举行奉献礼20:5 “举行奉献礼”指入住前举行的仪式。?他可以回家去,以免他阵亡了,别人为他的房子举行奉献礼。 6谁栽种了葡萄园还没有享受过园中的果子?他可以回家去,以免他阵亡了,别人享受他园中的果子。 7谁订了亲还没有迎娶?他可以回家去,以免他阵亡了,别人娶他的未婚妻。’ 8官长也要告诉士兵,‘有没有胆怯、害怕的?他可以回家去,免得影响他人士气。’ 9他们讲完后,就要委派将领率军出战。

攻城之略

10“你们进攻一座城之前,要先给城中居民求和的机会。 11如果他们开城求和,城里所有人都要做你们的奴隶,为你们服劳役。 12如果他们不肯求和,要交战,你们就要围攻那城。 13你们的上帝耶和华把城交给你们时,你们要用刀杀光城里所有的男子, 14但可以留下城中的妇女、孩童、牲畜及其他一切作战利品。你们可以享用仇敌的财物,那是你们的上帝耶和华赐给你们的。 15上述做法只适用于离你们很遥远的城邑,你们附近各族的城邑除外。 16你们的上帝耶和华将把你们附近各族的城邑赐给你们作产业,你们要将里面有气息的全部消灭。 17要遵照你们的上帝耶和华的吩咐,彻底灭绝人、亚摩利人、迦南人、比利洗人、希未人和耶布斯人, 18免得他们将祭拜自己神明的可憎习俗传给你们,以致你们得罪你们的上帝耶和华。

19“你们围攻一座城久攻不下时,不可用斧头砍掉那里的树木,因为你们可以吃树上的果子。田间的树木岂是人,让你们围攻吗? 20但你们可以砍那些不结果子的树来建围城的工事,直到攻陷为止。