Isaya 26 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 26:1-21

Wimbo Wa Ushindi

126:1 Isa 14:32; Zek 2:5; Isa 10:20; 30:29; 32:18; Zek 9:8; Za 48:13Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda:

Tuna mji ulio na nguvu,

Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.

226:2 Isa 58:8; 62:2; Ufu 21:13; Za 24:4-7; 83:13; Isa 1:26; 50:8Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia,

taifa lile lidumishalo imani.

326:3 Ay 22:21; Flp 4:7; Isa 9:6-7; 1Nya 5:20; Za 28:7; 22:5Utamlinda katika amani kamilifu

yeye ambaye moyo wake ni thabiti

kwa sababu anakutumaini wewe.

426:4 Isa 12:2; 50:10; Za 62:8; Mwa 49:24Mtumaini Bwana milele,

kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.

526:5 Isa 25:12; 25:5; Eze 26:11Huwashusha wale wajikwezao,

huushusha chini mji wenye kiburi,

huushusha hadi ardhini

na kuutupa chini mavumbini.

626:6 Isa 5:5; 49:26; 3:15; 14:30Miguu huukanyaga chini,

miguu ya hao walioonewa,

hatua za hao maskini.

726:7 Kum 32:4; Kut 14:19; Isa 42:16; Za 26:12; 25:8; Isa 40:4Mapito ya wenye haki yamenyooka.

Ewe uliye Mwenye Haki,

waisawazisha njia ya mtu mnyofu.

826:8 Za 18:22; 145:2; Isa 12:4; Kum 18:18; Isa 65:5; Za 37:9Naam, Bwana, tukienenda katika sheria zako,

twakungojea wewe,

jina lako na sifa zako

ndizo shauku za mioyo yetu.

926:9 Za 42:1-2; Mt 6:33; Za 63:6; 119:55; 1Nya 16:14; Za 78:34Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku,

wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku.

Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia,

watu wa ulimwengu hujifunza haki.

1026:10 Isa 32:6; 1Sam 12:24; Rum 2:4; Mhu 8:12; Mt 5:45; Isa 22:12-13; Yer 2:19; Yn 5:38Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu,

hawajifunzi haki,

hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya

wala hawazingatii utukufu wa Bwana.

1126:11 Ay 34:27; Isa 18:3; 44:9, 18; Ebr 10:27; Za 10:12; Yoe 2:18; Zek 1:14; Mik 7:16Ee Bwana, mkono wako umeinuliwa juu,

lakini hawauoni.

Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe,

moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.

1226:12 Za 119:165; Isa 9:6; Za 68:28Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu,

yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.

1326:13 Za 66:12; Isa 42:8; 2:8; 63:7Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala,

lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu.

1426:14 Kum 4:28; Za 9:5; Isa 10:3; Ay 28:5Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai,

roho za waliokufa hazitarudi tena.

Uliwaadhibu na kuwaangamiza,

umefuta kumbukumbu lao lote.

1526:15 Isa 33:17; 14:2; Ay 12:23Umeliongeza hilo taifa, Ee Bwana,

umeliongeza hilo taifa.

Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe,

umepanua mipaka yote ya nchi.

1626:16 Amu 6:2; Hos 5:15; Isa 5:30; Za 39:11; Isa 29:4Bwana, walikujia katika taabu yao,

wewe ulipowarudi,

waliweza kuomba kwa kunongʼona tu.

1726:17 Isa 21:3; Ufu 12:2; Yn 16:21Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa

anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake,

ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Bwana.

1826:18 Isa 59:4; Mwa 49:10; Za 17:14; Isa 42:6; 49:6; 51:4; Yer 12:16Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu,

lakini tulizaa upepo.

Hatukuleta wokovu duniani,

hatujazaa watu katika ulimwengu huu.

1926:19 Hos 13:14; Efe 5:14; Isa 25:8; Eze 37:1-14; Dan 12:2; Isa 18:4; Mwa 27:28; Za 22:29Lakini wafu wenu wataishi,

nayo miili yao itafufuka.

Ninyi mnaokaa katika mavumbi,

amkeni mkapige kelele kwa furaha.

Umande wenu ni kama umande wa asubuhi,

dunia itawazaa wafu wake.

2026:20 Kut 12:23; Za 30:5; Ay 14:13; 2Kor 4:17; Isa 10:25; 30:27Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu

na mfunge milango nyuma yenu,

jificheni kwa kitambo kidogo

mpaka ghadhabu yake ipite.

2126:21 Yud 14; Mik 1:3; Ay 16:18; Isa 29:6; 18:4; Lk 11:50-51; Isa 30:12-14Tazama, Bwana anakuja kutoka makao yake

ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao.

Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake,

wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 26:1-21

犹大的凯歌

1到那日,犹大境内的人必唱这首歌:

“我们有一座坚城,

耶和华使祂的拯救成为保护我们的城墙和屏障。

2打开城门,

让忠信的公义之民进来。

3你使坚信不移的人全然平安,

因为他们信靠你。

4要永远信靠耶和华,

因为耶和华上帝是永远屹立的磐石。

5祂贬抑高傲的人,

拆毁他们高耸的城邑,

把它们夷为平地、化为尘土,

6被困苦人的脚践踏,被贫穷人的足踩踏。”

7义人的道路是平坦的,

公正的主啊,你必修平义人所走的道路。

8耶和华啊,我们在你行审判的路上等候你,

我们心里渴慕你的尊名和威望。

9在夜间,我的心思慕你,

我的灵切切地寻求你。

你在世上施行审判的时候,

世人就学习行义。

10虽然你恩待恶人,

他们却仍然不学习行义。

即使在公正之地,

他们依然作恶,

全不把耶和华的威严放在眼里。

11耶和华啊,你的手高高举起,

他们却看不见。

愿他们因看见你向你子民所发的热心而感到羞愧。

愿你为敌人预备的火烧灭他们。

12耶和华啊,你必赐我们平安,

因为我们所做的事都是你为我们成就的。

13我们的上帝耶和华啊!

除你以外曾有别的主人管辖我们,

但我们只尊崇你的名。

14他们都已死去,再不能复生,

逝去的灵魂不能再回来。

因此你惩罚他们,毁灭他们,

使他们被人彻底遗忘。

15耶和华啊,你增添我们的国民,

增添我们的国民,

扩张我们的疆界,

你得到了荣耀。

16耶和华啊,我们在危难中寻求你。

你管教我们的时候,

我们就向你低声祷告。

17耶和华啊,我们曾在你面前呼求,

如临产的妇人在阵痛中呼喊。

18我们曾怀胎,经历产痛,

但产下来的却是风。

我们没有给世界带来拯救,

也没有给世上带来生命。

19然而,属你的逝者必复活,

他们的尸体必站起来。

睡在尘土中的人啊,要醒来欢唱!

你的甘露如清晨的甘露,

使地下的死人重获生机。

20我的百姓啊,

回到你们的房子里,

关上门躲藏一会儿,

等耶和华的愤怒平息。

21看啊,耶和华要走出祂的居所,

惩罚世上犯罪的人。

大地必不再隐藏被杀之人的尸首,

必将流在地上的血显露出来。