Isaya 25 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 25:1-12

Msifuni Bwana

125:1 Hes 23:19; Za 40:5; Yoe 2:21-26; Isa 7:13; 14:24; 37:26; Efe 1:11Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu,

nitakutukuza na kulisifu jina lako,

kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu

umetenda mambo ya ajabu,

mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.

225:2 Isa 37:26; Yer 51:37; Isa 17:3; 13:22; Kum 13:16; Ay 12:14Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi,

mji wenye ngome kuwa magofu,

ngome imara ya wageni kuwa si mji tena,

wala hautajengwa tena kamwe.

325:3 Kut 6:2; Za 22:23; Isa 11:14; 13:11; Ufu 11:13Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu,

miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.

425:4 Yoe 3:16; Isa 33:16; Za 46:1-11; Isa 49:25; 2Sam 22:3; Za 118:8; Isa 3:14Umekuwa kimbilio la watu maskini,

kimbilio la mhitaji katika taabu yake,

hifadhi wakati wa dhoruba

na kivuli wakati wa hari.

Kwa maana pumzi ya wakatili

ni kama dhoruba ipigayo ukuta

525:5 Yer 51:25; Za 18:44; Isa 13:11na kama joto la jangwani.

Wewe wanyamazisha makelele ya wageni;

kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu,

ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.

625:6 Mt 22:4; Mit 9:2; Dan 7:14; Mwa 29:22; Za 36:8Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa

karamu ya vinono kwa mataifa yote,

karamu ya mvinyo wa zamani,

nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.

725:7 2Kor 3:15-16; Efe 4:8; 1:17; Ay 4:9Juu ya mlima huu ataharibu

sitara ihifadhiyo mataifa yote,

kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,

825:8 Hos 13:14; 1Kor 15:54-55; Yer 31:16; Ufu 7:14-17; Ebr 2:14; Isa 26:19yeye atameza mauti milele.

Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote;

ataondoa aibu ya watu wake duniani kote.

Bwana amesema hili.

925:9 Isa 40:9; Yer 14:8; Za 20:5; Kum 32:43; Isa 2:11; 49:25-26; Za 145:19Katika siku ile watasema,

“Hakika huyu ndiye Mungu wetu;

tulimtumaini, naye akatuokoa.

Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini;

sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”

1025:10 Mwa 19:37; Hes 21:29; Kum 23:6; Isa 11:14; Amo 2:1-2Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu,

bali Moabu atakanyagwa chini

kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.

1125:11 Isa 5:25; 14:26; Law 26:19; Ay 40:12; Isa 2:10-17; 16:14Watakunjua mikono yao katikati yake,

kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee.

Mungu atashusha kiburi chao

licha ya ujanja wa mikono yao.

1225:12 Ay 40:11; Isa 26:5; Yer 51:44; Isa 2:15Atabomoa kuta ndefu za maboma yako

na kuziangusha chini,

atazishusha chini ardhini,

mpaka mavumbini kabisa.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 25:1-12

赞美之歌

1耶和华啊!你是我的上帝,我要尊崇你,赞美你的名。你信实无比,

按你古时定下的计划行了奇妙的事。

2你使城邑沦为废墟,

使坚垒沦为荒场。

外族人的宫殿不复存在,

永远不能重建。

3因此,强大的民必颂扬你,

残暴之邦的城邑必敬畏你。

4你是贫穷人的避难所,

是困苦之人患难中的避难所,

你是避风港,

是酷暑中的阴凉处。

残暴之徒的气息好像吹袭墙垣的暴风,

5又像干旱之地的热气。

你平息外族人的喧哗,

止息残暴之徒的歌声,

好像云朵消去酷热。

6锡安山上,万军之耶和华必为天下万民摆设丰盛的宴席,有陈年佳酿和精选的美食。 7在这山上,祂必除去遮蔽万民的面纱和笼罩万国的幔子。 8祂必永远吞灭死亡。主耶和华必擦去各人脸上的眼泪,从世上除掉祂子民的羞辱。这是耶和华说的。 9到那日,人们必说:“看啊,这是我们的上帝,我们信靠祂,祂拯救了我们。这是耶和华,我们信靠祂,我们要因祂的救恩而欢喜快乐。” 10耶和华必伸手保护这山,但摩押人必在本地被践踏,像干草被践踏在粪池中。 11他们必在里面张开手臂,好像张开手臂游泳的人一样。耶和华必摧毁他们的骄傲,挫败他们手中的诡计。 12祂必拆毁他们高大坚固的城墙,将其夷为平地、化为尘土。