Hosea 4 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Hosea 4:1-19

Shtaka Dhidi Ya Israeli

14:1 Mit 10:21; 24:2; Mik 6:2; Isa 1:3; Ay 10:2; Yer 2:9; 7:28; 51:5; Hos 2:20Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli,

kwa sababu Bwana analo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

24:2 Isa 59:3; Hos 5:2; 6:2; 7:1; 11:12; Eze 22:2-9; 1Fal 21:16Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

34:3 Yer 4:25, 28; 9:10; Amo 8:8; Isa 15:6; 33:9; Sef 1:3Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

44:4 Kum 17:12; Eze 3:26“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

54:5 Eze 7:19; 14:7; Hos 2:2Unajikwaa usiku na mchana,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

64:6 Mit 10:21; Hos 2:13; 8:1-12; Mal 2:7-8watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

74:7 Hab 2:16; Hos 9:11; 13:6Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

84:8 Isa 56:11; Mik 3:11; Hos 14:1Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

94:9 Isa 24:2; Yer 5:31; Hos 8:13; 10:10; 12:2Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

104:10 Mik 6:14; Isa 55:2; Hos 7:14; 9:17; Eze 22:9; Law 26:26“Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwacha Bwana

na kujiingiza wenyewe

114:11 Isa 28:7; Hos 5:4; Mit 20:1; Law 10:9; 1Sam 25:36katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

124:12 Yer 2:27; Ufu 17:2; Hab 2:19; Isa 44:20; Hes 15:39; Za 73:27wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

134:13 Isa 1:28; Hos 2:13; 10:9; Yer 2:20; Amo 7:17; Rum 1:28Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

144:14 Mwa 38:21; Hos 9:10; Mit 10:21“Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

154:15 Hos 9:15; 12:11; Amo 4:4; Yos 7:2“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

usipande kwenda Beth-Aveni4:15 Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

Wala usiape,

‘Hakika kama Bwana aishivyo!’

164:16 Isa 5:17; 7:25; Kut 32:9; Yer 31:18Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

174:17 Mt 15:14Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

184:18 Mik 3:11; 7:3Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

194:19 Hos 12:11; 13:15; Isa 1:29Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

Nueva Versión Internacional

Oseas 4:1-19

Pleito contra Israel

1Escuchen, israelitas, la palabra del Señor,

porque el Señor entabla un pleito

contra los habitantes del país:

«Ya no hay en esta tierra fidelidad ni amor

ni conocimiento de Dios.

2Solo hay maldición, mentira y asesinato,

robo y adulterio.

Abunda la violencia

y los homicidios se multiplican.

3Por tanto, se resecará la tierra

y desfallecerán todos sus habitantes.

¡Morirán las bestias del campo,

las aves del cielo y los peces del mar!

4»¡Que nadie acuse ni reprenda a nadie!

¡Tu pueblo parece acusar al sacerdote!

5Tropiezas de día y de noche

y los profetas tropiezan contigo.

Tu madre dejará de existir,

6pues por falta de conocimiento mi pueblo ha sido destruido.

»Puesto que rechazaste el conocimiento,

yo también te rechazo como mi sacerdote.

Ya que te olvidaste de la Ley de tu Dios,

yo también me olvidaré de tus hijos.

7Mientras más aumentaban los sacerdotes,

más pecaban contra mí;

cambiaron a quien es su gloria en algo vergonzoso.

8Del pecado de mi pueblo se alimentan;

disfrutan de su perversidad.

9¡Como es el pueblo, así será el sacerdote!

Por eso les pediré cuentas de su conducta

y les daré la paga de sus acciones.

10»Comerán, pero no quedarán satisfechos;

se prostituirán, pero no procrearán;

porque han abandonado al Señor

para entregarse 11a la prostitución,

al vino viejo y al vino nuevo,

que hacen perder la razón.

12Mi pueblo consulta a su ídolo de madera

y ese pedazo de palo le responde.

Un espíritu de prostitución los descarría;

se prostituyen en abierto desafío a su Dios.

13Sobre las cumbres de los montes ofrecen sacrificios,

queman incienso en las colinas,

bajo la agradable sombra

de robles, álamos y encinas.

Por eso se prostituyen sus hijas

y cometen adulterio sus nueras.

14»Pero no castigaré a sus hijas

por sus prostituciones

ni a sus nueras

por sus adulterios,

porque sus propios maridos se juntan con prostitutas

y participan en sacrificios ofrecidos por prostitutas de cultos paganos.

¡Un pueblo sin entendimiento

se precipita a la ruina!

15»Si tú, Israel, te prostituyes,

¡que no resulte culpable Judá!

»No vayan a Guilgal

ni suban a Bet Avén,4:15 Bet Avén, nombre que significa casa de maldad, se aplica aquí a la ciudad de Betel, que significa casa de Dios (véase también 5:8).

ni juren diciendo: “¡Tan cierto como vive el Señor!”.

16Israel es tan terco

como una novilla indómita.

¿Cómo podrá el Señor pastorearlos

en campo abierto, como a corderos?

17Efraín se ha aliado con los ídolos;

¡pues que se quede con ellos!

18Cuando ya no tienen buen vino,

se entregan de lleno a la prostitución,

¡y hasta sus gobernantes aman la deshonra!

19¡Por eso un torbellino los arrastrará

y quedarán avergonzados por sus sacrificios!