Habakuki 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Habakuki 2:1-20

12:1 Isa 21:8; Za 48:13; 85:8; Eze 3:17; Za 73:16, 17; 5:3Nitasimama katika zamu yangu,

na kujiweka mwenyewe juu ya maboma;

nitatazama nione atakaloniambia,

na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.

Jibu La Bwana

22:2 Isa 8:1; 30:8; Kum 27:8; Rum 4:24; 15:4; Yer 36:2; Eze 24:2; Ufu 1:19Kisha Bwana akajibu:

“Andika ufunuo huu,

na ukaufanye wazi juu ya vibao,

ili mpiga mbiu akimbie nao.

32:3 Dan 10:14; 11:27; 8:17; Za 27:14; Eze 12:25Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika;

unazungumzia mambo ya mwisho,

na kamwe hautakosea.

Iwapo utakawia, wewe usubiri;

kwa hakika utakuja na hautachelewa.

42:4 Eze 18:9; Yn 3:36; 2Kor 5:7; Rum 1:17; Gal 3:11; Ebr 10:37-38“Tazama, amejaa majivuno;

anavyovitamani si vya unyofu:

lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:

52:5 Mit 20:1; Isa 2:11; Mit 27:20; 30:15-16; Hab 1:9hakika mvinyo humsaliti;

ni mwenye kiburi na hana amani.

Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu

na kama kifo kamwe hatosheki;

anajikusanyia mataifa yote

na kuchukua watu wote mateka.

62:6 Isa 14:4; Amo 2:8“Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema,

“ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa

na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu!

Ataendelea hivi kwa muda gani?’

72:7 Mit 29:1Je, wadai wako hawatainuka ghafula?

Je, hawataamka na kukufanya utetemeke?

Kisha utakuwa mhanga kwao.

82:8 Zek 1:122:8 Isa 33:1; Yer 50:17-18; Oba 1:15; Zek 2:8-9; Eze 39:10Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi,

watu waliobaki watakuteka nyara wewe.

Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.

92:9 Yer 22:13; 51:13; Ay 39:27; Isa 10:14“Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu,

awekaye kiota chake juu,

ili kukimbia makucha ya uharibifu!

102:10 Yer 26:19; Nah 3:6Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi,

ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.

112:11 Yos 24:27; Zek 5:4; Lk 19:40Mawe ya kuta yatapiga kelele,

na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.

122:12 Eze 22:2; Mik 3:10“Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga

damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!

132:13 Isa 50:11; 47:13Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha

kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto,

na kwamba mataifa

yanajichosha bure?

142:14 Kut 16:7; Hes 14:21; Isa 11:9Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana,

kama maji yaifunikavyo bahari.

152:15 Mit 23:20“Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo,

akiimimina kutoka kwenye kiriba

cha mvinyo mpaka wamelewa,

ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.

162:16 Eze 23:32-34; Hos 4:7; Law 10:9; Mao 4:21; Za 16:5; Isa 51:22Utajazwa na aibu badala ya utukufu.

Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue!

Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia,

na aibu itafunika utukufu wako.

172:17 Yer 50:33; 51:35; 50:15Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika,

na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha.

Kwa sababu umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.

182:18 1Sam 12:21; Amu 10:14; Isa 40:19; Yer 5:21; 14:22; 10:14; 1Kor 12:2“Sanamu ina thamani gani,

kwani mwanadamu ndiye alichonga?

Ama kinyago kinachofundisha uongo?

Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza

hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe;

hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.

192:19 1Fal 18:27; Yer 10:4; Hos 4:12; Dan 5:4, 23Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’

Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’

Je, linaweza kuongoza?

Limefunikwa kwa dhahabu na fedha;

hakuna pumzi ndani yake.

202:20 Za 11:4; Isa 41:1Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu;

dunia yote na inyamaze mbele yake.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

哈巴谷書 2:1-20

1我要登上瞭望台,

站在望樓上守候,

看耶和華要對我說什麼,

我要怎樣向祂分訴。

耶和華的答覆

2耶和華對我說:

「將我的啟示記下來,

清楚地刻在板上,

便於人們閱讀。

3這啟示還未到實現之時,

它關乎結局,沒有虛假。

即使緩慢,也要等候,

因為這事終必發生,不再遲延。

4看那驕傲之人,他們心術不正,

但義人必靠信心2·4 「信心」或譯「忠信」。而活。

5財富2·5 「財富」參照死海古卷,多個希伯來抄本為「酒」。會欺騙驕傲之人,

使他們永不安分,

像陰間一樣貪得無厭,

如死亡一般永不滿足。

因此,他們征服萬國,

擄掠萬民。

6「但萬國萬民必用詩歌和俗語嘲諷他們,說,

『你們有禍了!

你們吞沒別人的財產,

靠剝削別人囤積財富,

要到何時呢?』

7你們的債主必突然行動,

使你們戰戰兢兢,

淪為他們的俘虜。

8你們從前擄掠許多國家,

殺人流血,

摧毀他們的土地、城市和人民,

所以各國的餘民必掠奪你們。

9「為自己的家積蓄不義之財、

在高處搭窩躲避災禍的人啊,

你們有禍了!

10你們陰謀毀滅各族,

以致自辱己家,自害己命。

11牆上的石頭必高聲控訴,

房子的梁木必同聲響應。

12「以人血建城邑,

以罪惡造城池的人啊,

你們有禍了!

13列邦的勞碌都化為灰燼,

列國的辛勞盡是虛空。

這不都是出於萬軍之耶和華嗎?

14因為大地必充滿對耶和華之榮耀的認識,

如同海洋被水充滿。

15「讓鄰居喝酒直到灌醉他們,好觀看他們祼體的人啊,

你們有禍了!

16你們必飽受羞辱,毫無榮耀。

你們喝吧,露出下體吧!

耶和華右手中的杯將傳給你們,

你們的榮耀將變成羞辱。

17你們以暴虐對待黎巴嫩

自己必被暴虐吞噬;

你們毀滅野獸,

自己必被恐怖籠罩。

因為你們殺人流血,

摧毀土地、城市和人民。

18「雕刻的偶像有什麼益處?

騙人的鑄像有什麼用處?

製造者竟信靠自己造的啞巴偶像!

19對木頭說『醒醒吧』,

對啞巴石頭說『起來吧』的人啊,你們有禍了!

它們能教導你們嗎?

看啊,它們外面包金裹銀,

裡面卻毫無生命。

20但耶和華住在祂的聖殿中,

世人都要在祂面前肅靜。」