2 Wakorintho 12 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Wakorintho 12:1-21

Maono Ya Paulo Na Mwiba Aliokuwa Nao

112:1 2Kor 11:16; 1Kor 2:10Yanipasa nijisifu, ingawa haifaidi kitu. Nitaenda kwenye maono na ufunuo kutoka kwa Bwana. 212:2 Rum 16:3; Mdo 8:39; Efe 4:10; 2Kor 11:11Namjua mtu mmoja katika Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alichukuliwa juu hadi mbingu ya tatu. Kama ni katika mwili au nje ya mwili, sijui, Mungu ajua. 3Nami najua ya kwamba mtu huyu, kwamba ni katika mwili au nje ya mwili mimi sijui, lakini Mungu ajua, 412:4 Lk 23:43; Ufu 2:7; 12; 5; 1Kor 2:3alinyakuliwa hadi Paradiso.12:4 Paradiso hapa ina maana mbinguni. Huko alisikia mambo yasiyoelezeka, mambo ambayo binadamu hana ruhusa ya kuyasimulia. 512:5 1Kor 2:3; 2Kor 11:9, 10, 30Nitajisifu kwa ajili ya mtu kama huyo, lakini sitajisifu kuhusu mimi mwenyewe ila mimi nitajisifia udhaifu wangu. 612:6 2Kor 10:8; 11:16Hata kama ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga, kwa maana nitakuwa nasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu yeyote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.

712:7 1Kor 2:10; Hes 33:55; Mt 4:10Ili kunizuia nisijivune kwa sababu ya ufunuo huu mkuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mjumbe wa Shetani, ili anitese. 812:8 Mt 26:39, 44Kwa habari ya jambo hili nilimsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu. 912:9 Rum 3:24; Flp 4:13; 1Fal 19:12Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uweza wangu hukamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. 1012:10 Mt 5:12; 2Kor 6:4; 2The 1:4; 2Kor 13:4Hii ndiyo sababu, kwa ajili ya Kristo, nafurahia udhaifu, katika kutukanwa, katika taabu, katika mateso na katika shida, kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo nina nguvu.

Wasiwasi Wa Paulo Kwa Wakorintho

1112:11 2Kor 11:1-5; 1Kor 15:9-10Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ilinipasa kusifiwa na ninyi, kwa sababu mimi si dhalili kuliko wale “mitume walio bora,” ingawa mimi si kitu. 1212:12 Yn 4:48Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani, ishara, miujiza na maajabu, yalifanywa miongoni mwenu kwa saburi nyingi. 1312:13 1Kor 9:12, 18; 2Kor 11:7Je, ninyi ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila tu kwamba mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili!

1412:14 2Kor 13:1; 1Kor 4:14-15; Mit 19:14Sasa niko tayari kuja kwenu kwa mara hii ya tatu, nami sitawalemea, kwa sababu sitahitaji chochote chenu, ila ninawahitaji ninyi, kwa kuwa hata hivyo watoto hawaweki akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi huweka akiba kwa ajili ya watoto wao. 1512:15 Flp 2:17; 1The 2:8; 2Kor 11:11Hivyo nitafurahi kutumia kila kitu nilicho nacho kwa ajili yenu, hata mwili wangu pia. Hata ingawa inaonekana ninavyozidi kuwapenda, ndivyo upendo wenu kwangu unavyopungua. 1612:16 2Kor 11:9Iwe iwavyo, kwa vyovyote vile mimi sikuwalemea. Lakini kwa mimi kuwa mwerevu naliwapata. 1712:17 2Nya 7:12Je, nilijipatia faida kwa kumtumia mtu yeyote niliyemtuma kwenu? 1812:18 2Kor 8:6, 16; 2:13; 10:8Nilimshawishi Tito aje kwenu, nami nilimtuma pamoja na ndugu yetu. Je, Tito aliwatumia ninyi ili kujipatia faida? Je, hatuenendi kwa roho moja, na hatuchukui hatua zile zile?

1912:19 Rum 9:1; 14:19; 1Kor 10:14; 2Kor 10:8Je, mmekuwa mkifikiri kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu? Sisi tumekuwa tukinena mbele za Mungu kama wale walio katika Kristo. Na chochote tufanyacho, ndugu wapendwa, ni kwa ajili ya kuwatia nguvu. 2012:20 2Kor 2:1-4; 1Kor 4:21; Gal 5:20; Rum 1:30; 1:29Kwa kuwa nina hofu ya kwamba nitakapokuja naweza kuwakuta nisivyotaka, nanyi mkanikuta msivyotaka. Nina hofu kwamba panaweza kuwa na ugomvi, wivu, ghadhabu, fitina, masingizio, masengenyo, majivuno na machafuko. 2112:21 2Kor 2:14; 13:2Nina hofu kwamba nitakapokuja tena kwenu, Mungu wangu atanidhili mbele yenu, nami nitasikitishwa na wengi waliotenda dhambi mbeleni, na wala hawajatubu kwa uchafu wao, uasherati, na ufisadi walioushiriki.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

哥林多後書 12:1-21

保羅得到的異象和啟示

1自誇雖然無益,但我不得不繼續誇下去,談談主給我的異象和啟示。 2我知道一位基督徒12·2 此人就是保羅本人,他不願誇耀自己的經歷。在十四年前曾被提到第三層天上,是在肉身之內還是在肉身之外,我不知道,只有上帝知道。 3-4我知道這個人曾被提到天上的樂園裡,聽見了人不可言傳的隱祕事,是在肉身之內還是在肉身之外,我不知道,只有上帝知道。 5我要為這人誇口。至於我自己,我除了誇耀自己的軟弱以外,別無可誇。 6就算我誇口,也不是傻瓜,因為我所說的都是實話。只是我不會這樣做,恐怕有人把我看得太高,超過了他對我的所見所聞。

7為了使我不至於因所受的啟示太大而自高,有一根刺在我身上,就是有撒旦的爪牙攻擊我,免得我驕傲自大。 8我曾三次祈求主叫這根刺離開我, 9但祂說:「我的恩典足夠你用,因為我的能力在人的軟弱上更顯得全備。」所以,我更喜歡誇耀自己的軟弱,好讓基督的能力蔭庇我。 10因此,為了基督的緣故,我欣然面對軟弱、凌辱、艱難、迫害和困苦,因為我什麼時候軟弱,就什麼時候剛強。

保羅關懷哥林多人

11我成了「傻瓜」,是被你們逼的!你們本該稱許我才對。我雖然算不了什麼,卻沒有一點比不上那些「超級使徒」。 12我在你們中間百般地忍耐,用神蹟、奇事、異能證明自己是使徒。 13你們什麼地方不及其他教會呢?唯一的區別是我沒有成為你們的負擔!希望各位原諒我的不公道!

14如今我打算第三次到你們那裡去。我不會拖累你們,因為我想得到的是你們,而不是你們的財物。兒女不必為父母積財,父母應當為兒女積財。 15為了你們的靈魂,我甘願付出,包括自己的生命。難道我越愛你們,就越得不到你們的愛嗎?

16算了!我沒有拖累過你們,但竟然有人說我狡猾,用詭計騙你們。 17請問,在我派到你們那裡的人當中,我藉著誰佔過你們的便宜呢? 18我懇求提多去你們那裡,並派弟兄與他同去。難道提多佔過你們的便宜嗎?我們行事為人豈不是心靈相通,步調一致嗎?

19你們一直以為我們是替自己辯白,其實我們這番話是在基督裡、在上帝面前說的。親愛的弟兄姊妹,這一切都是為了造就你們。 20因為我怕到你們那裡的時候,我對你們的期望會落空,而你們對我也大失所望。我怕你們當中有紛爭、嫉妒、惱怒、仇恨、毀謗、閒話、狂傲和混亂。 21我怕再去你們那裡時,我的上帝會使我在你們面前感到羞愧,又怕看到許多從前犯罪、道德敗壞、淫亂放蕩的人仍然不肯悔改,便心裡悲傷。