الأمثال 21 – NAV & NEN

New Arabic Version

الأمثال 21:1-31

1قَلْبُ الْمَلِكِ فِي يَدِ الرَّبِّ كَجَدَاوِلِ مِيَاهٍ يُمِيلُهُ حَيْثُمَا شَاءَ. 2جَمِيعُ تَصَرُّفَاتِ الإِنْسَانِ تَبْدُو نَقِيَّةً فِي عَيْنَيْ نَفْسِهِ، وَلَكِنَّ الرَّبَّ مُطَّلِعٌ عَلَى حَوَافِزِ الْقُلُوبِ. 3إِجْرَاءُ الْعَدْلِ وَالْحَقِّ أَكْثَرُ قُبُولاً عِنْدَ الرَّبِّ مِنَ الذَّبِيحَةِ. 4تَشَامُخُ الْعَيْنَيْنِ مِنْ غَطْرَسَةِ الْقَلْبِ، وَسِرَاجُ الأَشْرَارِ خَطِيئَةٌ. 5خُطَطُ الْمُجْتَهِدِ تُفْضِي حَتْماً إِلَى الْخِصْبِ، وَالْعَجُولُ مَصِيرُهُ الْعَوَزُ. 6ادِّخَارُ الْكُنُوزِ بِلِسَانٍ مُنَافِقٍ، دُخَانٌ مَتَلاشٍ وَفَخٌّ مُمِيتٌ. 7جَوْرُ الأَشْرَارِ يَجْرُفُهُمْ لِرَفْضِهِمْ إِجْرَاءَ الْعَدْلِ. 8طَرِيقُ الْمُذْنِبِ مُعَوَّجَةٌ، أَمَّا تَصَرُّفُ الزَّكِيِّ فَقَوِيمٌ. 9الإِقَامَةُ فِي رُكْنِ سَطْحٍ خَيْرٌ مِنْ مُشَاطَرَةِ بَيْتٍ مَعَ زَوْجَةٍ نَكِدَةٍ. 10نَفْسُ الْمُنَافِقِ تَشْتَهِي الشَّرَّ، وَقَرِيبُهُ لَا يَحْظَى بِرِضَاهُ. 11إِذَا عُوقِبَ الْمُسْتَهْزِئُ صَارَ الْجَاهِلُ حَكِيماً، وَإِنْ أُرْشِدَ الْحَكِيمُ اكْتَسَبَ مَعْرِفَةً.

12يَتَأَمَّلُ الصِّدِّيقُ فِي بَيْتِ الشِّرِّيرِ، (فَيَرَاهُ) يُلْقَى بِهِ إِلَى الْبَلايَا.

كنوز الحكيم

13مَنْ أَصَمَّ أُذُنَهُ عَنْ صُرَاخِ الْمِسْكِينِ، يَصْرُخُ هُوَ أَيْضاً وَلا مِنْ مُجِيبٍ. 14الْهَدِيَّةُ فِي الْخَفَاءِ تُخْمِدُ الْغَضَبَ، وَالرِّشْوَةُ فِي الْحِضْنِ تُسَكِّنُ السَّخَطَ. 15الْحُكْمُ بِالْعَدْلِ فَرَحٌ لِلصِّدِّيقِ، وَرُعْبٌ لِفَاعِلِي الإِثْمِ. 16الرَّجُلُ الشَّارِدُ عَنْ طَرِيقِ الْمَعْرِفَةِ يَسْكُنُ بَيْنَ جَمَاعَةِ الْمَوْتَى. 17عَاشِقُ اللَّذَّةِ فَقِيرٌ، وَالْمُوْلَعُ بِالْخَمْرِ وَالطِّيبِ لَا يَغْتَنِي. 18الشِّرِّيرُ فِدَاءٌ عَنِ الصِّدِّيقِ، وَالْغَادِرُ عَنِ الْمُسْتَقِيمِينَ. 19الإِقَامَةُ فِي أَرْضٍ مُقْفِرَةٍ خَيْرٌ مِنَ السُّكْنَى مَعَ امْرَأَةٍ مُشَاكِسَةٍ شَرِسَةٍ. 20فِي بَيْتِ الْحَكِيمِ كُنُوزٌ وَزَيْتٌ مُدَّخَرَةٌ، أَمَّا الإِنْسَانُ الْجَاهِلُ فَيُتْلِفُ مَا لَدَيْهِ. 21مَنِ اتَّبَعَ الْعَدْلَ وَالرَّحْمَةَ يَلْقَى الْحَيَاةَ وَالْحَقَّ وَالْمَجْدَ. 22الْحَكِيمُ يَتَسَلَّقُ سُورَ مَدِينَةِ الْجَبَابِرَةِ وَيُدَمِّرُ مَعْقِلَ اعْتِمَادِهِمْ 23مَنْ يَصُونُ فَمَهُ وَلِسَانَهُ عَنِ اللَّغْوِ يَحْفَظُ نَفْسَهُ مِنَ الْمَتَاعِبِ. 24الْمُتَشَامِخُ الْمُنْتَفِخُ يُدْعَى الْمُسْتَهْزِئَ لأَنَّهُ يَتَصَرَّفُ بِغُرُورِ الْكِبْرِيَاءِ. 25أَوْهَامُ الْكَسُولِ تَقْتُلُهُ لأَنَّ يَدَيْهِ تَأْبَيَانِ الْعَمَلَ. 26يَظَلُّ طَوَالَ النَّهَارِ مُتَشَهِّياً مُتَمَنِّياً، أَمَّا الصِّدِّيقُ فَيَسْخُو وَلا يَضِنُّ 27ذَبِيحَةُ الشِّرِّيرِ رِجْسٌ عِنْدَ الرَّبِّ، فَكَمْ بِالْحَرِيِّ إِنْ قَرَّبَهَا بِنِيَّةٍ أَثِيمَةٍ؟ 28شَاهِدُ الزُّورِ يَهْلِكُ، أَمَّا أَقْوَالُ الرَّجُلِ الْحَرِيصِ عَلَى الاسْتِمَاعِ فَتَدُومُ. 29الرَّجُلُ الشِّرِّيرُ يُغْلِظُ وَجْهَهُ، أَمَّا الْمُسْتَقِيمُ فَيَعْمَلُ عَلَى تَقْوِيمِ طُرُقِهِ. 30لَيْسَ مِنْ حِكْمَةٍ، وَلا مِنْ مَشُورَةٍ، وَلا مِنْ فِطْنَةٍ بِقَادِرَةٍ عَلَى مُقَاوَمَةِ اللهِ. 31مَعَ أَنَّ الْفَرَسَ مُعَدٌّ لِيَوْمِ الْقِتَالِ، فَإِنَّ النَّصْرَ هُوَ مِنْ عِنْدِ اللهِ.

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 21:1-31

121:1 Es 5:1; Yer 39:11-12Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana;

huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.

221:2 Mit 24:12; Lk 16:15; Yer 17:10; 1Sam 16:7Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,

bali Bwana huupima moyo.

321:3 Hos 6:6; Mik 6:6-8Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika

zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.

421:4 Ay 41:34; Mit 6:17Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,

ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!

521:5 Mit 10:4Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,

kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.

621:6 Mit 10:2; 2Pet 2:3Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo

ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.

721:7 Mit 11:5Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,

kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.

821:8 Mit 2:15Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,

bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.

921:9 Mit 21:19; 19:13; 25:24Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,

kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

1021:10 Yak 4:5Mtu mwovu hutamani sana ubaya,

jirani yake hapati huruma kutoka kwake.

1121:11 Mit 19:25Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,

mjinga hupata hekima;

wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,

hupata maarifa.

1221:12 1Kor 10:10; Rum 2:8; Mit 14:11Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,

naye atawaangamiza waovu.

1321:13 Ay 29:12; Zek 7:11; Mdo 7:57; Yak 2:13Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini,

yeye pia atalia, wala hatajibiwa.

1421:14 Mwa 32:20; Mit 18:16Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira

na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.

1521:15 Mit 21:9Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,

bali kitisho kwa watenda mabaya.

1621:16 Za 49:14; Eze 18:24Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu,

hupumzika katika kundi la waliokufa.

1721:17 Mit 23:20-21, 29-35Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,

yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.

1821:18 Isa 43:3-4; Mit 11:8Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,

nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.

1921:19 Mit 21:9Ni afadhali kuishi jangwani

kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.

2021:20 Za 112:3; Mit 10:22; Mt 25:3Katika nyumba ya mwenye hekima

kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,

lakini mtu mpumbavu

hutafuna vyote alivyo navyo.

2121:21 1Kor 15:58; Za 25:13; Mt 5:6Yeye afuatiaye haki na upendo

hupata uzima, mafanikio na heshima.

2221:22 Mit 8:14; Mhu 9:15-16Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,

na kuangusha ngome wanazozitegemea.

2321:23 Za 34:13; Yak 3:2; Mit 12:13Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake

hujilinda na maafa.

2421:24 Yer 43:2Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;

hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.

2521:25 Mit 13:4Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,

kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.

2621:26 Law 25:35; Mt 5:42Mchana kutwa hutamani zaidi,

lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

2721:27 1Fal 14:24; Amo 5:22; Mit 15:8Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,

si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

2821:28 Isa 29:21; Mit 19:5Shahidi wa uongo ataangamia,

bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.

2921:29 Mit 14:8Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,

bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.

3021:30 Ay 12:13; Yer 9:23; 2Nya 13:12; Mdo 5:39Hakuna hekima, wala akili, wala mpango

unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.

3121:31 Isa 31:1; Za 3:8Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,

bali ushindi huwa kwa Bwana.