الأمثال 20 – NAV & NEN

New Arabic Version

الأمثال 20:1-30

1الْخَمْرُ مُسْتَهْزِئَةٌ، وَالْمُسْكِرُ صَخَّابٌ، وَمَنْ يُدْمِنْ عَلَيْهَا فَلَيْسَ بِحَكِيمٍ. 2سَخَطُ الْمَلِكِ مِثْلُ زَمْجَرَةِ الأَسَدِ، وَمَنْ يُثِيرُ غَيْظَهُ يُسِيءُ إِلَى نَفْسِهِ. 3مِنْ دَوَاعِي شَرَفِ الْمَرْءِ أَنْ يَتَفَادَى الْخُصُومَةَ، وَالأَحْمَقُ يَخُوضُ مُعْتَرَكَ النِّزَاعِ. 4لَا يَحْرُثُ الْكَسُولُ فِي الْمَوْسِمِ خَشْيَةَ الْبَرْدِ، وَفِي أَوَانِ الْحَصَادِ يَطْلُبُ غَلَّةً فَلا يَجِدُ. 5نَوَايَا قَلْبِ الْمَرْءِ كَمَاءٍ عَمِيقٍ وَالْعَاقِلُ مَنْ يَسْتَخْرِجُهَا. 6كَثِيرُونَ يَدَّعُونَ الصَّلاحَ، أَمَّا الأَمِينُ فَمَنْ يَعْثُرُ عَلَيْهِ؟ 7الصِّدِّيقُ يَسْلُكُ بِكَمَالِهِ، فَطُوبَى لأَبْنَائِهِ مِنْ بَعْدِهِ. 8الْمَلِكُ الْمُتَرَبِّعُ عَلَى عَرْشِ الْقَضَاءِ يُغَرْبِلُ بِعَيْنِهِ الْبَصِيرَةِ الْخَيْرَ مِنْ كُلِّ شَرٍّ. 9مَنْ يَدَّعِي قَائِلاً: إِنِّي نَقَّيْتُ قَلْبِي، وَتَطَهَّرْتُ مِنْ خَطِيئَتِي؟

10الْغِشُّ مَا بَيْنَ أَوْزَانِ وَمَعَايِيرِ وَمَكَايِيلِ الشِّرَاءِ، وَأَوْزَانِ وَمَعَايِيرِ وَمَكَايِيلِ الْبَيْعِ رِجْسٌ لَدَى الرَّبِّ. 11حَتَّى الصَّبِيُّ يَكْشِفُ بِتَصَرُّفِهِ هَلْ عَمَلُهُ نَقِيٌّ وَقَوِيمٌ أَمْ لا. 12اللهُ هُوَ صَانِعُ الأُذُنِ الْمُطِيعَةِ وَالْعَيْنِ الْبَصِيرَةِ. 13لَا تُوْلَعْ بِالنَّوْمِ لِئَلّا تَفْتَقِرَ، اسْتَيْقِظْ وَاعْمَلْ فَتَشْبَعَ خُبْزاً. 14يَقُولُ الْمُشْتَرِي: هَذِهِ بِضَاعَةٌ رَدِيئَةٌ! هَذِهِ بِضَاعَةٌ رَدِيئَةٌ! وَإذَا مَضَى بِها فِي حَالِ سَبِيلِهِ يَشْرَعُ فِي الافْتِخَارِ.

15مَعَ أَنَّ الذَّهَبَ مَوْجُودٌ وَاللَّآلِئَ كَثِيرَةٌ، فَإِنَّ الشِّفَاهَ النَّاطِقَةَ بِالْمَعْرِفَةِ جَوْهَرَةٌ نَادِرَةٌ. 16خُذْ ثَوْبَ الْمَرْءِ الَّذِي ضَمِنَ غَرِيباً، وَارْتَهِنْهُ مِنْهُ، لأَنَّهُ كَفَلَ أَجْنَبِيًّا. 17الْخُبْزُ الْمُكْتَسَبُ حَرَاماً سَائِغٌ فِي حَلْقِ الإِنْسانِ، إِنَّمَا لَا يَلْبَثُ أَنْ يَمْتَلِئَ فَمُهُ حَصىً! 18بِالْمَشُورَةِ تَتَرَسَّخُ الْمَقَاصِدُ، وَبِحُسْنِ الدِّرَايَةِ خُضْ حَرْباً. 19النَّمَّامُ يُفْشِي الأَسْرَارَ، فَلا تُخَالِطْ مَنْ يُكْثِرُ الثَّرْثَرَةَ. 20مَنْ يَشْتِمُ أَبَاهُ أَوْ أُمَّهُ يُطْفِئُ الرَّبُّ سِرَاجَ حَيَاتِهِ فِي الظُّلْمَةِ الْحَالِكَةِ.

21رُبَّ مُلْكٍ يُوْرَثُ عَلَى عَجَلٍ فِي بِدَايَتِهِ، يَفْتَقِرُ إِلَى الْبَرَكَةِ فِي نِهَايَتِهِ. 22لَا تَقُلْ: لأُجَازِيَنَّ مَنْ أَسَاءَ إِليَّ شَرّاً. انْتَظِرْ، فَالرَّبُّ يُعِينُكَ. 23التَّلاعُبُ بِالْمَعَايِيرِ رِجْسٌ عِنْدَ الرَّبِّ، وَمِيزَانُ الْغِشِّ أَمْرٌ رَدِيءٌ. 24خَطْوَاتُ الإِنْسَانِ يُوَجِّهُهَا الرَّبُّ، فَكَيْفَ يُمْكِنُ لِلْمَرْءِ أَنْ يَفْهَمَ طَرِيقَهُ؟ 25شَرَكٌ لِلإِنْسَانِ أَنْ يَتَسَرَّعَ فِي النَّذْرِ لِلرَّبِّ ثُمَّ يَنْدَمَ عَلَى مَا نَذَرَ. 26الْمَلِكُ الْحَكِيمُ يُغَرْبِلُ الأَشْرَارَ، ثُمَّ يَسْحَقُهُمْ بِالنَّوَارِجِ، 27نَفْسُ الإِنْسَانِ سِرَاجُ الرَّبِّ الَّذِي يَبْحَثُ فِي كُلِّ أَغْوَارِ ذَاتِهِ. 28الرَّحْمَةُ وَالْحَقُّ يَحْفَظَانِ الْمَلِكَ، وَبِالرَّحْمَةِ يُدْعَمُ عَرْشُهُ. 29فَخْرُ الشُّبَّانِ فِي قُوَّتِهِمْ، أَمَّا بَهَاءُ الشُّيُوخِ فَفِي مَشِيبهِمْ. 30جُرُوحُ الضَّرْبَاتِ تُنَقِّي مِنَ الشُّرُورِ، وَالْجَلْدَاتُ تُطَهِّرُ أَغْوَارَ النَّفْسِ.

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 20:1-30

120:1 Law 10:9; Hab 2:5; 1Sam 25:36; 1Fal 20:16; Mit 31:4Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi;

yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.

220:2 Mit 8:36; 19:12; Es 7:7Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;

yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.

320:3 Mwa 13:8; Mit 17:14Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi,

bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

420:4 Mit 6:6; Mhu 10:18Mvivu halimi kwa majira;

kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama

lakini hapati chochote.

520:5 Za 18:16Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina,

lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.

620:6 Za 12:1; Mt 6:2; Mhu 7:28; Lk 18:8Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma,

bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?

720:7 Za 26:1; 37:25-26; 112:2Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama,

wamebarikiwa watoto wake baada yake.

820:8 1Fal 7:7; Mit 25:4-5Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu,

hupepeta ubaya wote kwa macho yake.

920:9 Mhu 7:20; 1Fal 8:46; 1Yn 1:8Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi;

mimi ni safi na sina dhambi?”

1020:10 Mit 20:23; 11:1Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti,

Bwana huchukia vyote viwili.

1120:11 Za 39:1; Mt 7:16Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,

kama tabia yake ni safi na adili.

1220:12 Kut 4:11; Rum 11:26; Za 94:9Masikio yasikiayo na macho yaonayo,

Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.

1320:13 Mit 6:11; 19:15; Rum 12:11Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini,

uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.

14“Haifai, haifai!” asema mnunuzi,

kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.

1520:15 Ay 28:12, 16, 17, 18, 19Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi,

lakini midomo inenayo maarifa

ni kito cha thamani kilicho adimu.

1620:16 Kut 22:26; Mit 27:13Chukua vazi la yule awekaye dhamana

kwa ajili ya mgeni;

lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo

kwa ajili ya mwanamke mpotovu.

17Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu,

bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.

1820:18 Mit 11:14; 24:6Fanya mipango kwa kutafuta mashauri,

ukipigana vita, tafuta maelekezo.

1920:19 Mit 11:13Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika,

kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.

2020:20 Kut 21:17; Mit 30:11; Ay 18:5; Law 20:9Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake,

taa yake itazimwa katika giza nene.

2120:21 Mit 28:8; Hab 2:6Urithi upatikanao haraka mwanzoni,

hautabarikiwa mwishoni.

2220:22 Mit 24:29; Yer 42:11; Kum 32:35; Rum 12:17-19Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!”

Mngojee Bwana, naye atakuokoa.

2320:23 Kum 25:13Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu,

nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.

2420:24 Mit 19:21; Yer 10:23; Rum 8:26Hatua za mtu huongozwa na Bwana.

Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?

2520:25 Mhu 5:2-5; Yer 44:25Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka

na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.

2620:26 Mit 20:8Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu,

hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.

2720:27 Za 119:105; Mit 16:2Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu,

huchunguza utu wake wa ndani.

2820:28 Mit 29:14; Isa 16:5Upendo na uaminifu humweka mfalme salama,

kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.

2920:29 Mit 16:31Utukufu wa vijana ni nguvu zao,

mvi ni fahari ya uzee.

3020:30 Za 51:2; Mit 22:15Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,

nayo michapo hutakasa utu wa ndani.