约书亚记 22 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

约书亚记 22:1-34

建祭坛之争

1约书亚召来了吕便迦得玛拿西半个支派的人来, 2对他们说:“你们都遵守了耶和华的仆人摩西的一切吩咐,也听从了我的一切吩咐。 3这些日子以来,你们从没有离弃自己的弟兄,遵守了你们的上帝耶和华的吩咐。 4现在你们的上帝耶和华已经照祂的应许使你们的弟兄安居,你们可以回到约旦河东,到摩西赐给你们作产业的地方。 5不过,你们要谨遵耶和华的仆人摩西吩咐你们的诫命和律法,要爱你们的上帝耶和华,遵行祂的旨意,听从祂的命令,依靠祂,全心全意地事奉祂。”

6于是,约书亚为他们祝福,送他们回去,他们就各自返回家园去了。

7摩西已经在巴珊把土地分给了玛拿西半个支派,约书亚约旦河西的土地分给了玛拿西另外的半个支派及其他支派。约书亚派他们回家的时候,为他们祝福, 8说:“现在你们带着大量财物、牲畜、金银、铜、铁和衣物返回家园,要把从敌人那里得来的财物分给你们的弟兄。” 9于是,吕便迦得玛拿西半个支派的人便离开在迦南示罗以色列人,返回耶和华借摩西分配给他们的基列

10他们来到约旦河附近的迦南境内,就在约旦河边筑了一座高大的祭坛。 11以色列人听见吕便迦得玛拿西半个支派的人在约旦河西的迦南境内筑起了一座祭坛, 12便全部聚集在示罗,要讨伐他们。

13以色列人派祭司以利亚撒的儿子非尼哈基列见他们, 14又从每支派差遣一位族长,共十位随行。 15他们来到基列吕便迦得玛拿西半个支派的人那里,对他们说: 16“耶和华的全体会众问你们,你们怎能这样背叛以色列的上帝,离弃耶和华,为自己另建祭坛呢? 17从前拜毗珥的罪恶不够大吗?那一次,瘟疫降到耶和华的会众身上,直到今日我们还没有洗净这罪。 18你们今日要离弃耶和华吗?今日你们背叛耶和华,明日祂必向以色列全体会众发怒。 19你们如果认为自己的土地不洁净,可以搬到耶和华的土地上跟我们一起居住,这里有耶和华的圣幕。只是不可在耶和华的祭坛以外,为自己另筑祭坛,以致背叛耶和华,背叛我们。 20从前谢拉的曾孙亚干私自留下那些耶和华吩咐要毁灭之物,耶和华的烈怒难道没有临到以色列全体会众吗?因他的罪而死的不只他一个人!”

21吕便迦得玛拿西半个支派的人便回答这些以色列的族长说: 22“大能的上帝耶和华,大能的上帝耶和华,祂知道一切!以色列人也当知道!如果我们悖逆或干犯耶和华,愿祂今天就不放过我们! 23如果我们离弃耶和华,为自己造祭坛,或在坛上献燔祭、素祭和平安祭,愿耶和华亲自惩罚我们。 24我们这样做是怕以后你们的子孙可能会对我们的子孙说,‘你们和以色列的上帝耶和华有什么关系? 25耶和华把约旦河定为我们跟你们吕便人和迦得人的边界,你们与耶和华一点关系也没有。’这样,恐怕你们的子孙会使我们的子孙不再敬畏耶和华。 26因此,我们便商议在这里筑一座祭坛,这坛不是用来献燔祭或别的祭, 27只是在你们和我们之间,也在彼此的后人之间立个证据,证明我们也献燔祭、平安祭及其他祭事奉耶和华,免得日后你们的子孙对我们的子孙说,‘你们与耶和华一点关系也没有。’ 28我们商议,万一你们对我们或我们的子孙这样说,我们可以回答说,‘你们看我们祖先筑的这座祭坛跟耶和华的祭坛一模一样,只是这座坛不是用来献燔祭或别的祭,而是作为你们和我们之间的证据!’ 29我们根本无意背叛、离弃我们的上帝耶和华,在祂圣幕前的祭坛以外另筑祭坛来献燔祭、素祭和别的祭。”

30祭司非尼哈以色列会众的族长听了他们的解释,都很满意。 31以利亚撒的儿子祭司非尼哈对他们说:“今日我们知道耶和华在我们当中,因为你们没有对耶和华不忠,现在你们使以色列人免遭耶和华的惩罚了。”

32以利亚撒的儿子非尼哈祭司和众族长便离开吕便人和迦得人,从基列回到迦南以色列人报告这事。 33众人听后,都很满意,便颂赞耶和华,打消了出兵讨伐吕便人和迦得人、毁灭他们家园的念头。

34吕便人和迦得人给那座祭坛取名叫“证坛”,意思是这坛在我们中间证明耶和华是上帝。

Kiswahili Contemporary Version

Yoshua 22:1-34

Makabila Ya Mashariki Yarudi Nyumbani

122:1 Hes 32:25Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, 222:2 Kum 3:18; Hes 32:20naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru. 3Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa. 422:4 Kut 33:14; Hes 32:22; Kum 3:22; Hes 32:18; Yos 1:13-15Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani. 522:5 Isa 43:22; Mal 3:14; Yos 23:11; Kum 5:29; 6:5-6, 17Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”

622:6 Mwa 24:60; Kut 39:43; Mwa 47:7; Yos 14:13; 2Sam 6:18; Lk 24:50Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao. 722:7 Hes 32:19, 33; Yos 12:5; 17:2; 14:13; Lk 24:50(Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki, 822:8 Kum 20:14; Hes 31:22, 27; Mwa 49:27; 1Sam 30:16; 2Sam 1:1; Isa 9:3akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”

922:9 Yos 18:1; Hes 32:26Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.

1022:10 Yos 18:17; Isa 19:19; 56:7Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani. 1122:11 Law 17:8; Kum 13:12; Amu 20:12Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli, 1222:12 Yos 18:1kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.

1322:13 Hes 25:7; 25:7; Yos 24:33; Kum 13:14; Kut 6:25Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase. 1422:14 Hes 1:4Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.

15Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia: 1622:16 Kum 7:3; 1Sam 15:11; Kum 12:13-14“Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi? 1722:17 Hes 23:28; 25:1-9Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo! 1822:18 Law 10:6; Hes 16:22; Mwa 18:23-25; Yos 7:11-12; 2Sam 1:17; 1Nya 21:1, 14Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana?

“ ‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli. 1922:19 Kut 26:1; Law 17:8-9; Yos 18:1Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu. 2022:20 Yos 7:1; Za 7:11; Law 10:6; Yos 7:5Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’ ”

21Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema: 2222:22 Kum 10:17; Za 50:1; 1Sam 2:3; 16:7; 1Fal 8:39; 1Nya 28:9; Za 11:4; 40:9; 44:21; 139:4; Yer 17:10; Ay 10:7“Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo. 2322:23 Yer 41:5; Kum 12:11; 1Sam 20:16; Za 7:3, 5, 10, 13, 14Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.

24“Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli? 25Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.

26“Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’ 2722:27 Mwa 21:30; Yos 24:27; Isa 19:20; Kum 12:6Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’

2822:28 Mwa 21:30“Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’

2922:29 Yos 24:16; Kut 26:1; Kum 12:13-14“Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”

30Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika. 3122:31 Law 26:11-12; 2Nya 15:2; Kut 25:8; 29:45; Zek 8:23; Ufu 21:3Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”

32Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli. 3322:33 Dan 2:19; Lk 2:28; 1Nya 29:20; 29:30; Neh 8:6Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.

3422:34 Mwa 21:30; Yos 24:27Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.