Zaburi 90:1-10 NEN

Zaburi 90:1-10

KITABU CHA NNE

(Zaburi 90–106)

Zaburi 90

Umilele Wa Mungu Na Udhaifu Wa Mwanadamu

Maombi ya Mose, mtu wa Mungu.

90:1 Kum 33:27; Efe 2:22; Ufu 21:3Bwana, wewe umekuwa makao yetu

katika vizazi vyote.

90:2 Ay 38:4, 5; 10:5; 15:7; Mwa 21:33; Isa 9:6; 57:15; Za 102:24-27; Mit 8:23-26Kabla ya kuzaliwa milima

au hujaumba dunia na ulimwengu,

wewe ni Mungu tangu milele hata milele.

90:3 Mwa 2:7; 3:9; Ay 7:21; 34:15; 1Kor 15:47; Mhu 12:7Huwarudisha watu mavumbini,

ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”

90:4 Ebr 13:8; 2Pet 3:8; Ay 10:5Kwa maana kwako miaka elfu

ni kama siku moja iliyokwisha pita,

au kama kesha la usiku.

90:5 Mwa 19:15; Isa 40:6Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo,

nao ni kama majani machanga ya asubuhi:

90:6 Isa 40:6-8; Ay 14:2; Za 92:7ingawa asubuhi yanachipua,

ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.

Tumeangamizwa kwa hasira yako

na tumetishwa kwa ghadhabu yako.

90:8 2Kor 4:2; Efe 5:12; Ebr 4:13; 4:12, 13; Za 19:12; 50:21; Yer 16:17; Mit 5:21; Mhu 12:14; Rum 2:16; 1Kor 4:5Umeyaweka maovu yetu mbele yako,

dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako.

90:9 Za 78:33Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako,

tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.

90:10 Isa 23:15, 17; 2Sam 19:35; Ay 5:7; 20:8; 34:15; Yer 25:11Siku zetu za kuishi ni miaka sabini,

au miaka themanini ikiwa tuna nguvu,

lakini yote ni ya shida na taabu,

nazo zapita haraka, nasi twatoweka.

Read More of Zaburi 90