Waebrania 8:10-12
8:10 Rum 11:27; 2Kor 3:3; Ebr 10:16; Eze 11:20; Zek 8:8Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli
baada ya siku zile, asema Bwana.
Nitaziweka sheria zangu katika nia zao
na kuziandika mioyoni mwao.
Nitakuwa Mungu wao,
nao watakuwa watu wangu.
8:11 Isa 54:13; Yn 6:45Mtu hatamfundisha tena jirani yake,
wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’
kwa sababu wote watanijua mimi,
tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.
8:12 Ebr 10:17; Yer 31:31-34Kwa sababu nitasamehe uovu wao,
wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”