1 Samweli 2:1-8
2:1 Lk 1:46-55; Za 13:5; 33:21; 18:2; 89:17; 148:4; 6:8; Hes 10:35; Zek 10:7; Flp 4:6Kisha Hana akaomba na kusema:
“Moyo wangu wamshangilia Bwana,
katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu.
Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu,
kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2:2 Kut 15:11; 8:10; 33:22; Law 11:44; Isa 40:25; 46:5; Mwa 49:25; Kum 32:37; 2Sam 22:2-32; 23:2-3; Za 31:3; 71:3“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana,
hakuna mwingine zaidi yako;
hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
2:3 Za 17:10; 31:18; 73:8; 75:4; 94:4; Yos 22:22; 1Sam 16:7; 1Fal 8:39; 1Nya 28:9; 2Nya 6:30; Mit 15:11; 24:11-12; Yer 11:20; 17:16“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo
wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi,
kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye,
na kwa yeye matendo hupimwa.
2:4 2Sam 1:27; Za 37:15; 46:9; 76:3; Ay 17:9; Isa 40:31; 41:1; 52:1; 57:10“Pinde za mashujaa zimevunjika,
lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
2:5 Lk 1:53; Za 113:9; Isa 54:1; Yer 15:9; Gal 4:27Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe
ili kupata chakula,
lakini wale waliokuwa na njaa
hawana njaa tena.
Mwanamke yule aliyekuwa tasa
amezaa watoto saba,
lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi
amedhoofika.
2:6 Kum 32:39; Ay 5:18; Hos 6:1; Yn 5:25-29; 11:25, 26; Ufu 1:18“Bwana huua na huleta uhai,
hushusha chini mpaka kaburini na hufufua.
2:7 Kum 8:18; Ay 5:11; 40:12; Za 75:7; Isa 2:12; 13:11; 22:19; Dan 4:37; Za 75:8Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha,
hushusha na hukweza.
2:8 Za 113:7-8; 72:12; 107:41; 145:14; 146:8; 104:5; Mit 8:29; Mt 23:12; 2Sam 7:8; Ay 36:7; 15:7; 38:4; Isa 22:23; 40:12; Yer 10:12; Eze 21:26; Yak 2:5; 1Fal 16:2Humwinua maskini kutoka mavumbini
na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu;
huwaketisha pamoja na wakuu
na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima.
“Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana;
juu yake ameuweka ulimwengu.