Zaburi 6:1-10
Zaburi 6
6:1 Za 2:5Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako,
wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
6:2 Za 4:1; 26:11; 61:2; 77:3; 142:3; Yer 3:12; 8:18; 12:15; 31:20; Hos 6:1; Isa 40:31; Za 32:3; 38:3; 42:10; 102:3Unirehemu Bwana,
kwa maana nimedhoofika;
Ee Bwana, uniponye,
kwa maana mifupa yangu
ina maumivu makali.
6:3 Ay 7:11; Za 4:2; 31:7; 38:8; 55:4; 89:46; Yn 12:27; Isa 6:11; Rum 9:2; 2Kor 2:4; Hab 1:12; 1Sam 1:14; 1Fal 18:21; Yer 4:14; Mt 26:38; Mit 18:14Nafsi yangu ina uchungu mwingi.
Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
6:4 Za 25:16; 69:16; 71:2; 86:16; 88:2; 102:2; 119:132; 13:5; 31:2, 16; 77:8; 85:7; 119:41; Isa 54:8, 10Geuka Ee Bwana, unikomboe,
uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
6:5 Za 30:9; 88:10-12; 115:17; Isa 38:18; Mhu 9:10Hakuna mtu anayekukumbuka
akiwa amekufa.
Ni nani awezaye kukusifu
akiwa kuzimu?
6:6 Ay 3:24; 16:16; 7:3; Lk 7:38; Za 77:3; 102:5; 12:5; Mdo 20:19; Mao 1:8, 11, 21, 22; Amu 8:5Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;
usiku kucha nafurikisha
kitanda changu kwa machozi;
nimelowesha viti vyangu vya fahari
kwa machozi.
6:7 Ay 16:8; Za 31:9; 69:3; 119:82; Isa 38:14Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,
yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
6:8 Za 119:115; 5:5; 139:19; Mt 7:23Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,
kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
6:9 Za 31:22; 116:1; 3:4; 40:1, 2; 28:6Bwana amesikia kilio changu kwa huruma,
Bwana amekubali sala yangu.
6:10 2Fal 19:26; Za 40:14Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,
watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.