Zaburi 33
Ukuu Na Wema Wa Mungu
133:1 Za 64:10; 101:1; 147:1; 11:7Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki;
kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
233:2 Mwa 4:21; 1Kor 14:7; Ufu 5:8; Za 92:3; 144:9Msifuni Bwana kwa kinubi,
mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
333:3 Za 40:3; 35:27; 47:1; Isa 42:10; Ufu 5:9; Ay 3:7Mwimbieni wimbo mpya;
pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
433:4 Ufu 19:9; 22:6; Za 19:8; 18:25; 119:142; 25:10Maana neno la Bwana ni haki na kweli,
ni mwaminifu kwa yote atendayo.
533:5 Za 11:7; 6:4Bwana hupenda uadilifu na haki;
dunia imejaa upendo wake usiokoma.
633:6 Ebr 11:3; Kut 8:19; Mwa 1:3, 16; 2Nya 2:12; Yn 1:1-3; Ay 26:13Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa,
jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
733:7 Mwa 1:10; Yos 3:16Ameyakusanya maji ya bahari
kama kwenye chungu;
vilindi vya bahari
ameviweka katika ghala.
833:8 Kum 6:13; 14:23; Za 2:11; 49:1; Isa 18:3; Mik 1:2Dunia yote na imwogope Bwana,
watu wote wa dunia wamche.
933:9 Za 148:5; Mwa 1:3Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,
aliamuru na ikasimama imara.
1033:10 Isa 44:25; Za 2:1; Ay 5:12Bwana huzuia mipango ya mataifa,
hupinga makusudi ya mataifa.
1133:11 Hes 23:19; Yer 51:12, 29; Ay 23:13; Mit 19:21; Eze 38:10; Mdo 4:27, 28Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele,
makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
1233:12 Za 144:15; 65:4; 4:3; 84:4; Kum 7:6; Kut 8:22; 34:9Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao,
watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
1333:13 Za 53:2; 102:19; 11:4; 14:2; Ebr 4:13; 2Nya 16:9; Ay 28:24Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini
na kuwaona wanadamu wote;
1433:14 Law 15:31; 1Fal 8:39kutoka maskani mwake huwaangalia
wote wakaao duniani:
1533:15 Ay 10:8; 11:11; 10:4; Yer 32:19; Isa 64:8; Hes 7:2; Za 44:21; 119:73; Mit 24:12yeye ambaye huumba mioyo yao wote,
ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
1633:16 1Sam 14:6Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;
hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
1733:17 Za 20:7Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,
licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
1833:18 Kut 3:16; Ay 36:7; Za 11:4; 6:4; 34:15; 1Pet 3:12Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao,
kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
1933:19 Za 56:13; Ay 5:20; Mdo 12:11ili awaokoe na mauti,
na kuwahifadhi wakati wa njaa.
2033:20 Za 27:14Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini,
yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
2133:21 1Sam 2:1; Yoe 2:23; Za 30:4; 99:3Mioyo yetu humshangilia,
kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
2233:22 Za 6:4Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana,
tunapoliweka tumaini letu kwako.