Zaburi 105
Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli
(1 Nyakati 16:8-22)
1105:1 1Nya 16:34; Za 80:18; 99:6; 116:13; Yoe 2:32; Mdo 2:21; Isa 12:4Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake,
wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
2105:2 Za 30:4; 146:2; 33:3; 96:1; 7:17; 18:49; 27:6; 59:17; 71:22; 75:1Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,
waambieni matendo yake yote ya ajabu.
3105:3 Za 89:16Lishangilieni jina lake takatifu,
mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
4105:4 Za 24:6; 27:8Mtafuteni Bwana na nguvu zake,
utafuteni uso wake siku zote.
5105:5 Za 40:5; Kum 7:18; 8:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,
miujiza yake na hukumu alizozitamka,
6105:6 Za 105:42; Kum 10:15; Za 106:5enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,
enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7105:7 Isa 26:8Yeye ndiye Bwana Mungu wetu,
hukumu zake zimo duniani pote.
8105:8 Mwa 9:15; Za 106:45; 111:5; Eze 16:60; Lk 1:72Hulikumbuka agano lake milele,
neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
9105:9 Mwa 22:16-18; 15:18; Ebr 6:17; Lk 1:73; 17:2; 12:7; Gal 3:15-18; Dan 9:4agano alilolifanya na Abrahamu,
kiapo alichomwapia Isaki.
10105:10 Mwa 28:13-15; Isa 55:3Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,
kwa Israeli liwe agano la milele:
11105:11 Mwa 12:7; Hes 34:2“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani
kuwa sehemu utakayoirithi.”
12105:12 Kum 7:7; Ebr 11:9; Mwa 17:8; 23:4; 34:30Walipokuwa wachache kwa idadi,
wachache sana na wageni ndani yake,
13105:13 Mwa 15:13-16; Hes 32:13; 33:3-49walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,
kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
14105:14 Mwa 35:5; 12:17-20; 20:3; Za 9:5Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;
kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
15105:15 Mwa 26:11; 20:7; 1Sam 12:3“Msiwaguse niliowatia mafuta;
msiwadhuru manabii wangu.”
16105:16 Isa 3:1; Law 26:26; Mwa 12:10; 41:54; 2Fal 8:1; Eze 4:16Akaiita njaa juu ya nchi
na kuharibu chakula chao chote,
17105:17 Mwa 45:5; 37:28; Mdo 7:9naye akatuma mtu mbele yao,
Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.
18105:18 Mwa 40:15Walichubua miguu yake kwa minyororo,
shingo yake ilifungwa kwa chuma,
19105:19 Mwa 12:10; 41:40; 40:20-21hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia,
hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.
20105:20 Mwa 41:14Mfalme alituma watu wakamfungua,
mtawala wa watu alimwachia huru.
21Alimfanya mkuu wa nyumba yake,
mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,
22105:22 Mwa 41:43-44; 41:40kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo
na kuwafundisha wazee wake hekima.
23105:23 Mdo 7:15; 13:17; Mwa 46:6; 47:28; Za 78:51Kisha Israeli akaingia Misri,
Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.
24105:24 Kut 1:7; Kum 26:7; Mdo 7:17Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana,
akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,
25105:25 Kut 4:21; 1:6-10; Mdo 7:19ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,
wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.
26105:26 Kut 3:10; 4:16; Hes 33:1; 16:5; 17:5-8Akamtuma Mose mtumishi wake,
pamoja na Aroni, aliyemchagua.
27105:27 Za 105:28-37; Kut 7:8; 12:51; 4:17; 10:1; 3:20; Dan 4:3Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,
miujiza yake katika nchi ya Hamu.
28105:28 Mwa 1:4; Za 99:7; Kut 10:22; 7:22Alituma giza na nchi ikajaa giza,
kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
29105:29 Za 78:44; Kut 7:21Aligeuza maji yao kuwa damu,
ikasababisha samaki wao kufa.
30105:30 Kut 8:2, 6Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia
hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
31105:31 Za 78:45; 107:25; 148:8; Kut 8:16-18; 8:21-24Alisema, yakaja makundi ya mainzi,
na viroboto katika nchi yao yote.
32105:32 Kut 9:22-25; Ay 38:22; Za 78:47Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,
yenye umeme wa radi nchini yao yote,
33105:33 Za 78:47; Kut 10:5, 12akaharibu mizabibu yao na miti ya tini,
na akaangamiza miti ya nchi yao.
34105:34 Za 107:25; Kut 10:4, 12-15; 1Fal 8:27; Yoe 1:6Alisema, nzige wakaja,
tunutu wasio na idadi,
35wakala kila jani katika nchi yao,
wakala mazao ya ardhi yao.
36105:36 Kut 4:23; 12:12Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao,
matunda ya kwanza ya ujana wao wote.
37105:37 Kut 3:21, 22Akawatoa Israeli katika nchi
wakiwa na fedha na dhahabu nyingi,
wala hakuna hata mmoja
kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38105:38 Kut 15:16Misri ilifurahi walipoondoka,
kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
39105:39 Kut 13:21; 1Kor 10:1; Za 78:14; Neh 9:12Alitandaza wingu kama kifuniko,
na moto kuwamulikia usiku.
40105:40 Za 78:18; Kut 16:4; Yn 6:31; Kut 16:12Waliomba, naye akawaletea kware,
akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41105:41 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17:6; Neh 9:15; Isa 48:21Alipasua mwamba, maji yakabubujika,
yakatiririka jangwani kama mto.
42105:42 Mwa 15:1-4, 13-16; 13:14-17Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,
aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43105:43 Kut 15:1-19; Za 106:12Aliwatoa watu wake kwa furaha,
wateule wake kwa kelele za shangwe,
44105:44 Kum 6:10-11; Za 106:12akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi
wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45105:45 Kum 6:14-21; 4:1, 40; Za 105:35; 78:5-7alifanya haya ili wayashike mausia yake
na kuzitii sheria zake.
Msifuni Bwana.105:45 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.
第105篇
上帝和祂的子民
(平行经文:历代志上16:8‑22)
1你们要称谢耶和华,呼求祂的名,
在列邦传扬祂的作为。
2要歌颂、赞美祂,
述说祂一切奇妙的作为。
3要以祂的圣名为荣,
愿寻求耶和华的人心中快乐。
4要寻求耶和华和祂的能力,
时常来到祂面前。
5-6祂仆人亚伯拉罕的后裔啊,
祂所拣选的雅各的子孙啊,
要记住祂所行的神迹奇事和祂口中的判词。
7祂是我们的上帝耶和华,
祂在普天下施行审判。
8祂永远记得祂的约,
历经千代也不忘祂的应许,
9就是祂与亚伯拉罕所立的约,
向以撒所起的誓。
10祂将这约定为律例赐给雅各,
定为永远的约赐给以色列。
11祂说:“我必把迦南赐给你,
作为你的产业。”
12那时他们人丁稀少,寥寥可数,
在当地寄居。
13他们在异国他乡流离飘零。
14耶和华不容人压迫他们,
还为他们的缘故责备君王,
15说:“不可加害我膏立的人,
也不可伤害我的先知。”
16祂命饥荒降在那里,
断绝一切食物供应。
17祂派一个人先去,
这人就是被卖为奴隶的约瑟。
18他被戴上脚镣,套上枷锁,
19直到后来他的预言应验,
耶和华的话试炼了他。
20埃及王派人释放他,
百姓的首领给他自由,
21派他执掌朝政,
管理国中的一切,
22有权柄管束王的大臣,
将智慧传授王的长老。
23以色列来到埃及,
雅各寄居在含地。
24耶和华使祂的子民生养众多,
比他们的仇敌还要强盛。
25祂使仇敌转念憎恨祂的子民,
用诡计虐待祂的仆人。
26祂派遣祂的仆人摩西和祂拣选的亚伦,
27在埃及行神迹,
在含地行奇事。
28祂使黑暗降下笼罩那里;
他们没有违背祂的话。
29祂使埃及的水变成血,
鱼都死去;
30又使国中到处是青蛙,
王宫禁院也不能幸免。
31祂一发命令,
苍蝇蜂拥而至,虱子遍满全境。
32祂使雨变成冰雹,
遍地电光闪闪。
33祂击倒他们的葡萄树和无花果树,
摧毁他们境内的树木。
34祂一发声,
就飞来无数蝗虫和蚂蚱,
35吃尽他们土地上的植物,
吃尽他们田间的出产。
36祂又击杀他们境内所有的长子,
就是他们年轻力壮时生的长子。
37祂带领以色列人携金带银地离开埃及,
各支派中无人畏缩。
38埃及人惧怕他们,
乐见他们离去。
39祂铺展云彩为他们遮荫,
晚上用火给他们照明。
40他们祈求,
祂就赐下鹌鹑,降下天粮,
叫他们饱足。
41祂使磐石裂开、涌出水来,
在干旱之地奔流成河。
42因为祂顾念祂赐给仆人亚伯拉罕的神圣应许。
43祂带领祂的子民欢然离去,
祂所拣选的百姓欢呼前行。
44祂把列国的土地赐给他们,
使他们获得别人的劳动成果。
45祂这样做是要使他们持守祂的命令,
遵行祂的律法。
你们要赞美耶和华!