Yeremia 14 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 14:1-22

Ukame, Njaa Na Upanga

1Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:

214:2 Isa 3:26; Yer 8:21; Mit 21:13“Yuda anaomboleza,

miji yake inayodhoofika;

wanaomboleza kwa ajili ya nchi,

nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.

314:3 Kum 28:48; 2Fal 18:31; 2Sam 15:30; Es 6:12; Ay 6:19-20Wakuu wanawatuma watumishi wao maji;

wanakwenda visimani

lakini humo hakuna maji.

Wanarudi na vyombo bila maji;

wakiwa na hofu na kukata tamaa,

wanafunika vichwa vyao.

414:4 Amo 4:8; Zek 14:17; Yer 3:3; 12:11Ardhi imepasuka nyufa

kwa sababu hakuna mvua katika nchi;

wakulima wana hofu

na wanafunika vichwa vyao.

514:5 Isa 15:6Hata kulungu mashambani

anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo

kwa sababu hakuna majani.

614:6 Ay 39:5-6; Yer 2:24; Za 104:11; Mwa 47:4Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame

na kutweta kama mbweha;

macho yao yanakosa nguvu za kuona

kwa ajili ya kukosa malisho.”

714:7 Isa 3:9; Hos 5:5; Yer 2:19; 8:14; Za 25:11; 79:9; 1Sam 12:22Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu,

Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako.

Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa,

nasi tumetenda dhambi dhidi yako.

814:8 Za 9:18; Mdo 28:20; Yer 17:13; 50:7; Za 18:46; Isa 25:9Ee Tumaini la Israeli,

Mwokozi wake wakati wa taabu,

kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi,

kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?

914:9 Isa 50:2; Mwa 17:7; Yer 8:19; 15:16; Kut 29:45; Isa 63:19; Za 27:9Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa,

kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa?

Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana,

nasi tunaitwa kwa jina lako;

usituache!

1014:10 Yer 2:25; Za 119:101; Yer 6:20; Hes 8:13; Ebr 8:12; Amo 5:22; Hos 7:2; 9:9; Yer 44:21Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa:

“Wanapenda sana kutangatanga,

hawaizuii miguu yao.

Hivyo Bwana hawakubali;

sasa ataukumbuka uovu wao

na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”

1114:11 Kut 32:10; 1Sam 2:25Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa. 1214:12 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Yer 7:21; Law 1:1-17; Yer 11:11; Amo 5:22; Isa 51:19; Yer 9:16Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”

13Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’ ”

1414:14 Yer 23:25; 2The 2:9-11; Eze 13:2-6; Yer 23:16; Mao 2:9; Eze 12:24; Yer 27:14Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe. 1514:15 Yer 20:6; Eze 14:9; Yer 16:4; Mao 1:19; Yer 23:15; 5:12-13Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa. 1614:16 Yer 17:10; Mit 1:31; Yer 7:33; Za 79:3; Mt 15:14Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.

1714:17 Za 119:136; Yer 8:21; Mao 1:16; 2Fal 19:21; Yer 23:12“Nena nao neno hili:

“ ‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi

usiku na mchana bila kukoma;

kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu,

amepata jeraha baya,

pigo la kuangamiza.

1814:18 Eze 7:14-15; 2Nya 36:10; Yer 13:17Kama nikienda mashambani,

ninaona wale waliouawa kwa upanga;

kama nikienda mjini,

ninaona maangamizi ya njaa.

Nabii na kuhani kwa pamoja

wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’ ”

1914:19 Yer 7:29; 30:12-13; 8:15; Isa 1:6Je, umemkataa Yuda kabisa?

Umemchukia Sayuni kabisa?

Kwa nini umetuumiza

hata hatuwezi kuponyeka?

Tulitarajia amani,

lakini hakuna jema lililotujia;

tulitarajia wakati wa kupona

lakini kuna hofu kuu tu.

2014:20 Amu 10:10; Dan 9:7-8; Yer 3:13; Law 26:40; 1Fal 8:47; Ezr 9:6Ee Bwana, tunatambua uovu wetu

na kosa la baba zetu;

kweli tumetenda dhambi dhidi yako.

2114:21 Yer 17:12; Yos 7:9; Isa 62:7; Yer 3:17; Kut 2:24Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa;

usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka.

Kumbuka agano lako nasi

na usilivunje.

2214:22 1Fal 8:36; Isa 30:23; Za 135:7; Isa 41:24; 44:10; Yer 10:15Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa

iwezayo kuleta mvua?

Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua?

La hasha, ni wewe peke yako,

Ee Bwana, Mungu wetu.

Kwa hiyo tumaini letu liko kwako,

kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

耶利米书 14:1-22

预言旱灾

1耶和华告诉耶利米有关旱灾的事:

2犹大悲泣,

她的城邑衰败,

人人坐在地上痛哭,

耶路撒冷哀鸣四起。

3贵族派仆人去水池打水,

仆人去那里发现没有水,

就带着空瓶垂头丧气、

羞愧地抱头而归。

4天不下雨,

土地干裂,

农夫沮丧地抱着头。

5因为没有草,

田野的母鹿抛弃了刚生下来的小鹿;

6因为没有草,

野驴站在光秃的山头上像豺狼一样喘气,双目无神。”

7耶和华啊,虽然我们的罪控告我们,

我们屡屡叛逆得罪你,

求你为了自己的名而拯救我们。

8以色列的盼望和患难时的救主啊,

你为什么在本地像个异乡人,

像个只住一夜的客旅呢?

9你为什么像个受惊的人,

像个无力救人的勇士呢?

耶和华啊,你一直都在我们中间,

我们属于你的名下,

求你不要抛弃我们。

10关于这些百姓,耶和华说:

“他们喜欢游荡,

不约束自己的脚步,

因此耶和华不悦纳他们。

现在祂要追忆他们的罪恶,

追讨他们的罪。”

11耶和华对我说:“你不要为这百姓求好处。 12即使他们禁食,我也不会听他们的呼求;他们献上燔祭和素祭,我也不会悦纳。我要用刀剑、饥荒和瘟疫灭绝他们。” 13我说:“主耶和华啊!众先知不停地告诉他们不会有战争,也不会遭遇饥荒,说耶和华必在这地方赐给他们永久的平安。”

14耶和华对我说:“那些先知奉我的名说假预言,我并没有差派他们,没有委任他们,也没有对他们说话。他们对你们说的预言是假异象,是占卜,是他们心中的妄想。 15我没有差派他们,他们却奉我的名预言这地方必没有刀剑和饥荒。他们必死于刀剑和饥荒。这是耶和华说的。 16听他们说预言的人及其妻子儿女,必因饥荒和战争而暴尸耶路撒冷街头,无人掩埋。因为我要使他们受到应得的报应。

17耶利米,你要对他们说,

‘让我昼夜泪眼汪汪吧,

因为我的处女同胞遭受重创,

伤势危重。

18我走到田间,

眼前是死于刀下的尸体;

我进入城里,

见饥荒肆虐,

先知和祭司也流亡异乡14:18 “先知和祭司也流亡异乡”或译“连先知和祭司也浑浑噩噩,茫然无措”。。’”

19耶和华啊,你完全丢弃犹大了吗?

你厌恶锡安吗?

你为什么重重地打我们,以致无法医治?

我们期待平安,却没有祥和;

渴望得到医治,却饱受惊吓。

20耶和华啊,我们承认自己和我们祖先的罪,

我们诚然得罪了你。

21为了你的尊名,

求你不要厌恶我们,

不要让你荣耀的宝座蒙羞。

求你顾念你与我们立的约,

不要废除它。

22在列国供奉的偶像中,

谁能赐下雨水呢?

天能自降甘霖吗?

我们的上帝耶和华啊,

难道不是只有你能行这些事吗?

是你行了这一切,

所以我们仰望你。