Yeremia 11 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 11:1-23

Agano Limevunjwa

1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 2“Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu. 311:3 Kum 11:26-28; 27:26; Gal 3:10; Kum 28:15-68Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili, 411:4 Law 26:3; Kum 4:20; 1Fal 8:51; Kut 24:8; Yer 7:23; Eze 11:20maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. 511:5 Kum 7:12; Kut 6:8; 13:5; Za 105:8-11; Kut 3:8; Kum 27:26Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.”

Nikajibu, “Amen, Bwana.”

611:6 Kut 15:26; Yn 13:17; Rum 2:13; Yak 1:22; Yer 4:5; Kum 15:5Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata. 711:7 2Nya 36:15Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.” 811:8 Yer 7:26; Law 26:14-43; Yos 23:15; Mhu 9:3; Yer 3:17; 2Nya 7:19; Za 78:10Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’ ”

911:9 Hos 6:9; Eze 1:28; 22:25Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu. 1011:10 Eze 20:18; Kum 9:7; 2Nya 30:7; Amu 2:11-13; 10:13; Zek 7:11; Yer 16:11; 34:18Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao. 1111:11 Eze 8:8-18; Ay 27:9; Za 66:18; 2Fal 22:16; Zek 7:13; Ay 11:20; Yer 14:12Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza. 1211:12 Kum 32:37-38; Amu 10:14; Yer 44:17; Isa 45:20Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga. 1311:13 Yer 44:21; 3:24; Kut 20:3; Yer 19:4; 2Fal 17:29; Yer 7:9Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’

1411:14 Kut 32:10; Yer 7:16“Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.

1511:15 Eze 16:25; Hag 2:12; Yer 7:9-10“Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu,

anapofanya mashauri yake maovu na wengi?

Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza

kuondolea mbali adhabu yako?

Unapojiingiza katika ubaya wako,

ndipo unashangilia.”

1611:16 Yer 7:20; 21:14; Rum 11:17-24; Hos 14:6; Isa 27:11Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi

ulio na matunda mazuri kwa sura.

Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu

atautia moto,

nayo matawi yake yatavunjika.

1711:17 Kut 15:17; Isa 5:2; Yer 7:9; 12:2; 7:18Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.

Shauri Baya Dhidi Ya Yeremia

18Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya. 1911:19 Za 54:3; Yer 20:10; Ay 28:13; Za 83:4; 44:22; Yer 18:18; Ay 28:13; Isa 53:8Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema,

“Sisi na tuuangamize mti na matunda yake;

nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai,

ili jina lake lisikumbukwe tena.”

2011:20 Mdo 17:31; Za 7:8-9, 11; 1Sam 2:3; 1Nya 29:17; Za 58:10; Mao 3:60Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki,

nawe uchunguzaye moyo na akili,

wacha nione ukiwalipiza wao kisasi,

kwa maana kwako nimeweka shauri langu.

2111:21 Yer 12:6; Amo 2:12; Yer 38:4; Ay 21:18; Yer 21:7; 34:20; Isa 30:10“Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’: 2211:22 Isa 9:17; Yer 18:21kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa. 2311:23 Lk 19:44; Yer 6:9; 23:12Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’ ”

New International Version

Jeremiah 11:1-23

The Covenant Is Broken

1This is the word that came to Jeremiah from the Lord: 2“Listen to the terms of this covenant and tell them to the people of Judah and to those who live in Jerusalem. 3Tell them that this is what the Lord, the God of Israel, says: ‘Cursed is the one who does not obey the terms of this covenant— 4the terms I commanded your ancestors when I brought them out of Egypt, out of the iron-smelting furnace.’ I said, ‘Obey me and do everything I command you, and you will be my people, and I will be your God. 5Then I will fulfill the oath I swore to your ancestors, to give them a land flowing with milk and honey’—the land you possess today.”

I answered, “Amen, Lord.”

6The Lord said to me, “Proclaim all these words in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem: ‘Listen to the terms of this covenant and follow them. 7From the time I brought your ancestors up from Egypt until today, I warned them again and again, saying, “Obey me.” 8But they did not listen or pay attention; instead, they followed the stubbornness of their evil hearts. So I brought on them all the curses of the covenant I had commanded them to follow but that they did not keep.’ ”

9Then the Lord said to me, “There is a conspiracy among the people of Judah and those who live in Jerusalem. 10They have returned to the sins of their ancestors, who refused to listen to my words. They have followed other gods to serve them. Both Israel and Judah have broken the covenant I made with their ancestors. 11Therefore this is what the Lord says: ‘I will bring on them a disaster they cannot escape. Although they cry out to me, I will not listen to them. 12The towns of Judah and the people of Jerusalem will go and cry out to the gods to whom they burn incense, but they will not help them at all when disaster strikes. 13You, Judah, have as many gods as you have towns; and the altars you have set up to burn incense to that shameful god Baal are as many as the streets of Jerusalem.’

14“Do not pray for this people or offer any plea or petition for them, because I will not listen when they call to me in the time of their distress.

15“What is my beloved doing in my temple

as she, with many others, works out her evil schemes?

Can consecrated meat avert your punishment?

When you engage in your wickedness,

then you rejoice.11:15 Or Could consecrated meat avert your punishment? / Then you would rejoice

16The Lord called you a thriving olive tree

with fruit beautiful in form.

But with the roar of a mighty storm

he will set it on fire,

and its branches will be broken.

17The Lord Almighty, who planted you, has decreed disaster for you, because the people of both Israel and Judah have done evil and aroused my anger by burning incense to Baal.

Plot Against Jeremiah

18Because the Lord revealed their plot to me, I knew it, for at that time he showed me what they were doing. 19I had been like a gentle lamb led to the slaughter; I did not realize that they had plotted against me, saying,

“Let us destroy the tree and its fruit;

let us cut him off from the land of the living,

that his name be remembered no more.”

20But you, Lord Almighty, who judge righteously

and test the heart and mind,

let me see your vengeance on them,

for to you I have committed my cause.

21Therefore this is what the Lord says about the people of Anathoth who are threatening to kill you, saying, “Do not prophesy in the name of the Lord or you will die by our hands”— 22therefore this is what the Lord Almighty says: “I will punish them. Their young men will die by the sword, their sons and daughters by famine. 23Not even a remnant will be left to them, because I will bring disaster on the people of Anathoth in the year of their punishment.”