Warumi 9 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Warumi 9:1-33

Kuteuliwa Kwa Israeli Na Mungu

19:1 Gal 1:20; 1Tim 2:7; Rum 1:9Ninasema kweli katika Kristo, wala sisemi uongo, dhamiri yangu inanishuhudia katika Roho Mtakatifu. 29:2 Rum 10:1Nina huzuni kuu na uchungu usiokoma moyoni mwangu. 39:3 Kut 32:32; 1Kor 12:3; 16:22; Rum 11:14Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu hasa, wale walio wa kabila langu kwa jinsi ya mwili, 49:4 Kut 6:7; Kum 7:6; 4:13; Flp 1:12; Za 147:19; Ebr 9:1; Mdo 13:32; Gal 3:16yaani, watu wa Israeli, ambao ndio wenye kule kufanywa wana, ule utukufu wa Mungu, yale maagano, kule kupokea sheria, ibada ya kwenye Hekalu na zile ahadi. 59:5 Mt 1:1-16; Yn 1:1; Kol 2:9; Rum 1:3, 25; 2Kor 11:31Wao ni wa uzao wa mababa wakuu wa kwanza, ambao kutoka kwao Kristo alikuja kwa jinsi ya mwili kama mwanadamu, yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, mwenye kuhimidiwa milele! Amen.

69:6 Rum 2:28, 29; Gal 6:16Si kwamba Neno la Mungu limeshindwa. Kwa maana si kila Mwisraeli ambaye ni wa uzao utokanao na Israeli ni Mwisraeli halisi. 79:7 Mwa 21:12; Ebr 11:18Wala hawakuwi wazao wa Abrahamu kwa sababu wao ni watoto wake, lakini: “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.” 89:8 Rum 8:14; Gal 3:16; 4:23Hii ina maana kwamba, si watoto waliozaliwa kimwili walio watoto wa Mungu, bali ni watoto wa ahadi wanaohesabiwa kuwa uzao wa Abrahamu. 99:9 Mwa 18:10; 18:14Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitakurudia tena wakati kama huu, naye Sara atapata mtoto wa kiume.”

109:10 Mwa 25:23; 25:21Wala si hivyo tu, bali pia watoto aliowazaa Rebeka walikuwa na baba huyo huyo mmoja, yaani, baba yetu Isaki. 119:11 Rum 8:28; 9:16; 8:28Lakini, hata kabla hao mapacha hawajazaliwa au kufanya jambo lolote jema au baya, ili kwamba kusudi la Mungu la kuchagua lipate kusimama, 129:12 Mwa 25:23si kwa matendo, bali kwa yeye mwenye kuita, Rebeka aliambiwa, “Yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.” 139:13 Mal 1:2-3; Kum 21:15; Mit 13:24; Mt 10:37; Lk 14:26; Yn 12:25Kama vile ilivyoandikwa, “Nimempenda Yakobo, lakini nimemchukia Esau.”

Mungu Hana Upendeleo

149:14 2Nya 19:7; Kum 32:4; Ay 8:3; 34:10; Za 92:15Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha! 159:15 Kut 33:19Kwa maana Mungu alimwambia Mose,

“Nitamrehemu yeye nimrehemuye,

na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”

169:16 Efe 2:8; Tit 3:5Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu. 179:17 Kut 14:4; Za 76:10Kwa maana Maandiko yamwambia Farao, “Nilikuinua kwa kusudi hili hasa, ili nipate kuonyesha uweza wangu juu yako, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.”

189:18 Yos 11:20; Rum 11:25Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia yeye atakaye kumhurumia na humfanya mgumu yeye atakaye kumfanya mgumu.

199:19 1Kor 15:35; Yos 2:18; 2Sam 16:10; Dan 4:35Basi mtaniambia, “Kama ni hivyo, kwa nini basi bado Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kupinga mapenzi yake?” 209:20 Isa 64:8; Yer 18:6; Isa 10:15Lakini, ewe mwanadamu, u nani wewe ushindane na Mungu? “Je, kilichoumbwa chaweza kumwambia yeye aliyekiumba, ‘Kwa nini umeniumba hivi?’ ” 219:21 2Tim 2:20Je, mfinyanzi hana haki ya kufinyanga kutoka bonge moja vyombo vya udongo, vingine kwa matumizi ya heshima na vingine kwa matumizi ya kawaida?

229:22 Rum 2:4Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu? 239:23 Rum 8:28; 8:30Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vile vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake, 249:24 Rum 8:28; 3:29yaani pamoja na sisi, ambao pia alituita, si kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa?

Yote Yalitabiriwa Katika Maandiko

259:25 Hos 2:23; 1Pet 2:10Kama vile Mungu asemavyo katika Hosea:

“Nitawaita ‘watu wangu’

wale ambao si watu wangu;

nami nitamwita ‘mpenzi wangu’

yeye ambaye si mpenzi wangu,”

269:26 Hos 1:10; Mt 16:16tena,

“Itakuwa hasa mahali pale walipoambiwa,

‘Ninyi si watu wangu,’

wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’ ”

279:27 Mwa 22:17; Isa 10:22-23; Hos 1:10; Yoe 2:32; Rum 11:5Isaya anapiga kelele kuhusu Israeli:

“Ingawa idadi ya wana wa Israeli

ni wengi kama mchanga wa pwani,

ni mabaki yao tu watakaookolewa.

28Kwa kuwa Bwana ataitekeleza

hukumu yake duniani kwa haraka

na kwa ukamilifu.”

299:29 Yak 5:4; Isa 1:9; 13:19; Yer 50; 40Ni kama vile alivyotabiri Isaya akisema:

“Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote

asingelituachia uzao,

tungelikuwa kama Sodoma,

tungelifanana na Gomora.”

Kutokuamini Kwa Israeli

309:30 Flp 3:9; Ebr 11:17Kwa hiyo tuseme nini basi? Kwamba watu wa Mataifa ambao hawakutafuta haki, wamepata haki ile iliyo kwa njia ya imani. 319:31 Isa 51:11; Rum 11:7; Gal 5:4Lakini Israeli, ambao walijitahidi kupata haki kwa njia ya sheria, hawakuipata. 329:32 1Pet 2:8Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa njia ya imani bali kwa njia ya matendo. Wakajikwaa kwenye lile “jiwe la kukwaza.” 339:33 Isa 8:14; 1Pet 2:6, 8Kama ilivyoandikwa:

“Tazama naweka katika Sayuni jiwe la kukwaza watu

na mwamba wa kuwaangusha.

Yeyote atakayemwamini

hataaibika kamwe.”

Nueva Versión Internacional

Romanos 9:1-33

La elección soberana de Dios

1Digo la verdad en Cristo; no miento. Mi conciencia me lo confirma en el Espíritu Santo. 2Me invade una gran tristeza y me embarga un continuo dolor. 3Desearía yo mismo ser maldecido y separado de Cristo por el bien de mis hermanos, los de mi propio pueblo, 4el pueblo de Israel. De ellos son la adopción como hijos, la gloria divina, los pactos, la Ley, el privilegio de adorar a Dios y el de contar con sus promesas. 5De ellos son los patriarcas y de ellos, según la naturaleza humana, nació Cristo, quien es Dios sobre todas las cosas. ¡Alabado sea por siempre!9:5 Cristo … siempre! Alt. Cristo. ¡Dios, que está sobre todas las cosas, sea alabado por siempre! Amén.

6Ahora bien, no digamos que la palabra de Dios ha fracasado. Lo que sucede es que no todos los que descienden de Israel son Israel. 7Tampoco por ser descendientes de Abraham son todos hijos suyos. Al contrario: «Tu descendencia se establecerá por medio de Isaac».9:7 Gn 21:12. 8En otras palabras, los hijos de Dios no son los descendientes naturales; más bien, se considera descendencia de Abraham a los hijos de la promesa. 9Y la promesa es esta: «Dentro de un año volveré y para entonces Sara tendrá un hijo».9:9 Gn 18:10,14.

10No solo eso. También sucedió que los hijos de Rebeca tuvieron un mismo padre, que fue nuestro antepasado Isaac. 11Sin embargo, antes de que los mellizos nacieran o hicieran algo bueno o malo, y para confirmar el propósito de la elección divina, 12no con base en las obras, sino al llamado de Dios, se le dijo a ella: «El mayor servirá al menor».9:12 Gn 25:23. 13Y así está escrito: «Amé a Jacob, pero aborrecí a Esaú».9:13 Mal 1:2,3.

14¿Qué concluiremos? ¿Acaso es Dios injusto? ¡De ninguna manera! 15Es un hecho que a Moisés le dice:

«Tendré misericordia de quien quiera tenerla

y seré compasivo con quien quiera serlo».9:15 Éx 33:19.

16Por lo tanto, la elección no depende del deseo ni del esfuerzo humano, sino de la misericordia de Dios. 17Porque la Escritura le dice al faraón: «Te he levantado precisamente para mostrar en ti mi poder y para que mi nombre sea proclamado por toda la tierra».9:17 Éx 9:16. 18Así que Dios tiene misericordia de quien él quiere tenerla y endurece a quien él quiere endurecer.

19Pero tú me dirás: «Entonces, ¿por qué todavía nos echa la culpa Dios? ¿Quién puede oponerse a su voluntad?». 20Respondo: ¿Quién eres tú para pedirle cuentas a Dios? «Acaso le dirá la olla de barro al que la modeló: “¿Por qué me hiciste así?”».9:20 Is 29:16; 45:9. 21¿No tiene derecho el alfarero de hacer del mismo barro unas vasijas para usos especiales y otras para fines ordinarios?

22¿Y qué si Dios, queriendo mostrar su ira y dar a conocer su poder, soportó con mucha paciencia a los que eran objeto de su castigo9:22 objeto de su castigo. Lit. vasijas de ira. y estaban destinados a la destrucción? 23¿Qué si lo hizo para dar a conocer sus gloriosas riquezas a los que eran objeto de su misericordia, y a quienes de antemano preparó para esa gloria? 24Esos somos nosotros, a quienes Dios llamó no solo de entre los judíos, sino también de entre los no judíos. 25Así lo dice Dios en el libro de Oseas:

«Llamaré “mi pueblo” a los que no son mi pueblo;

y llamaré “mi amada” a la que no es mi amada».9:25 Os 2:23.

26«Y sucederá que en el mismo lugar donde se les dijo:

“Ustedes no son mi pueblo”,

serán llamados “hijos del Dios viviente”».9:26 Os 1:10.

27Isaías, por su parte, proclama respecto a Israel:

«Aunque los israelitas sean tan numerosos

como la arena del mar,

solo el remanente será salvo;

28porque plenamente y sin demora

el Señor cumplirá su sentencia en la tierra».9:28 Is 10:22,23.

29Así había dicho Isaías:

«Si el Señor de los Ejércitos

no nos hubiera dejado descendientes,

seríamos ya como Sodoma,

nos pareceríamos a Gomorra».9:29 Is 1:9.

Incredulidad de Israel

30¿Qué concluiremos? Pues que los no judíos, que no buscaban la justicia, la han alcanzado. Me refiero a la justicia que es por la fe. 31En cambio Israel, que iba en busca de justicia a través de la Ley, no ha alcanzado esa justicia. 32¿Por qué no? Porque no la buscaron mediante la fe, sino mediante las obras, como si fuera posible alcanzarla así. Por eso tropezaron con la «piedra de tropiezo», 33como está escrito:

«Miren, yo pongo en Sión una piedra de tropiezo

y una roca que hace caer;

pero el que confíe en él no será defraudado».9:33 Is 8:14; 28:16.