Nahumu 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Nahumu 2:1-13

Ninawi Kuanguka

12:1 Yer 51:20Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi.

Linda ngome,

chunga barabara,

jitieni nguvu wenyewe,

kusanya nguvu zako zote!

22:2 Eze 37:23; Isa 60:15Bwana atarudisha fahari ya Yakobo,

kama fahari ya Israeli,

ingawa waangamizi wamewaacha ukiwa

na wameharibu mizabibu yao.

32:3 Eze 23:14-15Ngao za askari wake ni nyekundu,

mashujaa wamevaa nguo nyekundu.

Chuma kwenye magari ya vita chametameta,

katika siku aliyoyaweka tayari,

mikuki ya mierezi inametameta.

42:4 Yer 4:13; Eze 23:24Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani,

yakikimbia nyuma na mbele uwanjani.

Yanaonekana kama mienge ya moto;

yanakwenda kasi kama umeme.

52:5 Yer 46:12Anaita vikosi vilivyochaguliwa,

lakini bado wanajikwaa njiani.

Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wa mji,

ile ngao ya kuwakinga imetayarishwa.

62:6 Isa 45:1; Nah 3:13Malango ya mto yamefunguliwa wazi,

na jumba la kifalme limeanguka.

72:7 Mwa 8:8; Isa 59:11; 32:12Imeagizwa kwamba mji uchukuliwe

na upelekwe uhamishoni.

Vijakazi wake wanaomboleza kama hua

na kupigapiga vifua vyao.

8Ninawi ni kama dimbwi,

nayo maji yake yanakauka.

Wanalia, “Simama! Simama!”

Lakini hakuna anayegeuka nyuma.

9Chukueni nyara za fedha!

Chukueni nyara za dhahabu!

Wingi wake hauna mwisho,

utajiri kutoka hazina zake zote!

102:10 Yos 2:11; 7:5; Isa 29:22Ameharibiwa, ametekwa nyara, ameachwa uchi!

Mioyo inayeyuka, magoti yanalegea,

miili inatetemeka,

na kila uso umebadilika rangi.

112:11 Isa 5:29Liko wapi sasa pango la simba,

mahali ambapo waliwalisha watoto wao,

ambapo simba dume na simba jike walikwenda

na ambapo wana simba walikwenda

bila kuogopa chochote?

122:12 Yer 51:34; 4:7; Isa 37:18Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake,

alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake,

akijaza makao yake kwa alivyoua

na mapango yake kwa mawindo.

132:13 Isa 10:5-13; Yer 21:13; Nah 3:5; Za 46:9; 2Sam 2:26; Mik 5:6Bwana Mwenye Nguvu Zote anatangaza,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Magari yenu ya vita nitayateketeza kwa moto,

na upanga utakula wana simba wako.

Sitawaachia mawindo juu ya nchi.

Sauti za wajumbe wako

hazitasikika tena.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

那鴻書 2:1-13

尼尼微的覆滅

1尼尼微啊,

攻擊者已經向你撲來。

你要進駐堡壘,

把守道路,

集中全力,

準備上陣!

2雖然擄掠者曾擄掠雅各

擄掠以色列

毀壞他們的葡萄樹枝,

但耶和華必恢復雅各的榮耀,

恢復以色列的榮耀。

3他的勇士手持紅色盾牌,

他的士兵身穿朱紅戰衣。

他們整裝待發之日,

戰車鐵光閃閃,

松木矛槍在空中揮舞。

4戰車在街道上狂奔,

在廣場上橫衝直撞,

亮如火炬,疾似閃電。

5亞述王召集將領,

他們一路跌跌撞撞,

奔上城牆,架起防禦盾牌。

6河閘大開,宮殿坍塌。

7王后赤身被擄;

宮女捶胸悲泣,

像鴿子一樣哀鳴。

8尼尼微城自古以來就像聚水的池子,

如今居民卻像洩漏的池水四散奔逃。

雖有人喊:「站住!站住!」

卻無人回頭。

9搶銀子吧!搶金子吧!

城裡有無盡的財富和數不清的寶物。

10尼尼微被洗劫一空!

淪為廢墟!

一片荒涼!

人們膽戰心驚,雙膝哆嗦,

渾身發抖,面色蒼白。

11如今那獅子的洞穴,

那餵養猛獅的地方在哪裡呢?

從前,雄獅、母獅和幼獅曾在那裡出入,

無人驚擾。

12雄獅為幼獅撕碎充足的食物,

為母獅絞殺獵物,

洞穴裡堆滿獵物,

堆滿撕碎的肉。

13萬軍之耶和華說:

「我與你為敵,

我要燒毀你的戰車,

使刀劍吞噬你的猛獅;

我要使你無法再擄掠他國,

你使者的聲音將從此消逝。」