Mwanzo 35 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 35:1-29

Yakobo Arudi Betheli

135:1 Mwa 12:8Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”

235:2 Yos 24:15; Kut 19:10, 14Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu. 335:3 Mwa 32:7; Amu 2:15Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.” 435:4 Mwa 24:22Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu. 535:5 Kut 15:16Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.

635:6 Mwa 28:19; 10:19Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani. 735:7 Mwa 8:20Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli,35:7 El-Betheli maana yake Mungu wa Betheli. kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.

835:8 Mwa 24:59; 12:8Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.35:8 Alon-Bakuthi maana yake Mwaloni wa Kilio.

935:9 Mwa 28:13; 32:29Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki. 1035:10 Mwa 17:5Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.

1135:11 Mwa 17:1; 17:6Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi,35:11 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako. 1235:12 Mwa 28:13; 12:7Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.” 1335:13 Mwa 17:22Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.

1435:14 Mwa 28:18; Kut 29:40Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake. 1535:15 Mwa 12:8Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.35:15 Betheli maana yake Nyumba ya Mungu.

Vifo Vya Raheli Na Isaki

1635:16 Mwa 48:7Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu. 1735:17 Kut 1:15; Mwa 30:24Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.” 1835:18 1Sam 4:21Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni.35:18 Benoni maana yake Mwana wa huzuni yangu. Lakini babaye akamwita Benyamini.35:18 Benyamini maana yake Mwana wa mkono wangu wa kuume.

1935:19 Mwa 48:7Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu). 2035:20 1Sam 10:2; 6:18Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.

21Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi. 22Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili.

Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:

23Wana wa Lea walikuwa:

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo,

Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.

2435:24 Mwa 30:24; 35:18Wana wa Raheli walikuwa:

Yosefu na Benyamini.

2535:25 Mwa 30:24Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa:

Dani na Naftali.

2635:26 Mwa 37:2Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa:

Gadi na Asheri.

Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.

2735:27 Mwa 13:18; Amu 1:10Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki. 2835:28 Mwa 25:7Isaki aliishi miaka 180. 2935:29 Mwa 15:15; 25:8-9Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 35:1-29

雅各遷往伯特利

1上帝對雅各說:「你到伯特利去住,你要在那裡為上帝築一座壇,祂在你逃避你哥哥以掃時曾向你顯現。」 2於是,雅各吩咐家人和所有的隨從:「你們要除掉你們當中的外族神像,潔淨自己,更換衣服。 3我們要上伯特利去,在那裡為上帝築一座壇,祂在我遭遇患難時聽了我的禱告,一路都與我同在。」 4他們把所有外族的神像和自己的耳環都交給雅各雅各把這些東西埋在示劍的橡樹下。

5他們就出發了,上帝使恐懼籠罩周圍的城邑,沒有人敢追趕他們。 6雅各和所有的隨從來到迦南路斯,也就是伯特利7他在那裡建造了一座壇,稱那地方為伊勒·伯特利35·7 「伊勒·伯特利」意思是「伯特利的上帝」。,因為在他逃避哥哥的時候,上帝曾在那裡向他顯現。 8後來利百加的奶媽底波拉死了,葬在伯特利下面的橡樹下,那棵樹叫亞倫·巴古35·8 「亞倫·巴古」意思是「哭泣的橡樹」。

9雅各巴旦·亞蘭回來後,上帝又向他顯現,賜福給他。 10上帝對他說:「你叫雅各,但從今以後不要再叫雅各了,你要改名叫以色列。」這樣雅各改名為以色列11上帝又說:「我是全能的上帝,你要生養眾多,人丁興旺,一國,甚至多國必從你而出,許多君王必出自你的子孫。 12我要把賜給亞伯拉罕以撒的土地賜給你和你的後代。」 13上帝說完就離開雅各升上天去。 14雅各在上帝跟他說話的地方立了一根石柱,又在柱子上奠酒、澆油, 15稱那地方為伯特利

拉結和以撒去世

16他們從伯特利繼續前行,離以法他還有一段路時,拉結要分娩,出現難產。 17接生婆對難產的她說:「不要害怕,你又添了一個兒子!」 18拉結嚥氣前給兒子取名叫便·俄尼35·18 「便·俄尼」意思是「我在苦難中生的兒子」。雅各卻叫他便雅憫35·18 「便雅憫」意思是「右手之子」,「右手」希伯來文有幸運或力量的意思。19拉結死後就葬在通往以法他的路旁,以法他伯利恆20雅各在她的墳上立了石碑,這碑至今還在。 21以色列繼續前行,在以得塔附近搭起了帳篷。 22以色列在那裡居住時,呂便和父親的妾辟拉通姦,以色列也知道這件事。

雅各有十二個兒子。 23利亞生了雅各的長子呂便,還有西緬利未猶大以薩迦西布倫24拉結生了約瑟便雅憫25拉結的婢女辟拉生了拿弗他利26利亞的婢女悉帕生了迦得亞設。他們都是雅各的兒子,是在巴旦·亞蘭出生的。

27雅各來到他父親以撒住的幔利,即基列·亞巴,也就是亞伯拉罕以撒寄居的地方。基列·亞巴就是希伯崙28以撒享年一百八十歲, 29年紀老邁,壽終正寢,歸到他祖先那裡。他的兒子以掃雅各把他安葬了。