Mwanzo 25 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 25:1-34

Kifo Cha Abrahamu

1Abrahamu alioa mke mwingine, ambaye jina lake aliitwa Ketura. 225:2 Yer 25:25; Mwa 36:35; 37:28, 36; Kut 2:15; Hes 22:4; 25:6; Amu 6:1-3; 8:22-24; 9:17; Za 83:9; Isa 9:4; 10:26; Hab 3:7; Ay 2:11Huyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. 3Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi. 425:4 Isa 60:6Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Hawa wote walikuwa uzao wa Ketura.

525:5 Mwa 24:36Abrahamu akamwachia Isaki kila kitu alichokuwa nacho. 625:6 Mwa 22:24; 21:10; Amu 6:3, 33; 1Fal 4:30; Eze 25:4Lakini Abrahamu alipokuwa bado hai, akawapa watoto wa masuria wake zawadi, kisha akawaondoa waende kuishi pande za mashariki mbali na mwanawe Isaki.

725:7 Mwa 12:4; 35:28; 47:9, 28; 50:22; Ay 42:16Kwa jumla, Abrahamu aliishi miaka 175. 825:8 Mwa 35:29; 49:29; Hes 20:24; 31:2; Kum 31:14; 32:50; 34:5Ndipo Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa akiwa mwenye umri mzuri, mzee aliyeshiba siku, naye akakusanywa pamoja na watu wake. 925:9 Mwa 35:29; 47:30; 49:31; 23:9; 13:18; 50:13Watoto wake Isaki na Ishmaeli wakamzika katika pango la Makpela karibu na Mamre, katika shamba lililokuwa la Efroni mwana wa Sohari Mhiti, 1025:10 Mwa 10:15Shamba ambalo Abrahamu alilinunua kwa Wahiti. Hapo ndipo Abrahamu alipozikwa pamoja na mkewe Sara. 1125:11 Mwa 12:2; 16:14Baada ya kifo cha Abrahamu, Mungu akambariki mwanawe Isaki, ambaye baadaye aliishi karibu na Beer-Lahai-Roi.

Wana Wa Ishmaeli

1225:12 Mwa 2:4; 17:20; 21:18Hivi ndivyo vizazi vya Ishmaeli mtoto wa Abrahamu, ambaye mjakazi wake Sara, Hagari Mmisri, alimzalia Abrahamu.

1325:13 Mwa 28:9; 36:3; Za 120:5; Isa 21:16; 42:11; 60:7; Yer 2:10; 49:28; Eze 27:21Haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, yaliyoorodheshwa kulingana na jinsi walivyozaliwa: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli ni Nebayothi, akafuatia Kedari, Adbeeli, Mibsamu, 1425:14 Yos 15:25; Oba 1:1; Isa 21:11Mishma, Duma, Masa, 1525:15 Ay 6:19; Isa 21:14; Yer 25:23; 1Nya 5:19Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema. 1625:16 Mwa 17:20; 13:16; Za 83:9Hawa walikuwa wana wa Ishmaeli na haya ni majina ya viongozi wa makabila kumi na mawili kulingana na makao yao na kambi zao. 17Kwa jumla Ishmaeli aliishi miaka 137. Akapumua pumzi ya mwisho, akafa, naye akakusanywa pamoja na watu wake. 1825:18 Mwa 17:20; 21:18; 16:7, 12Wazao wa Ishmaeli waliishi kuanzia nchi ya Havila hadi Shuri, karibu na mpaka wa Misri, unapoelekea Ashuru. Hao waliishi kwa uhasama na ndugu zao wote.

Yakobo Na Esau

19Hivi ndivyo vizazi vya Isaki mwana wa Abrahamu.

Abrahamu akamzaa Isaki, 2025:20 Mwa 26:34; 48:7; 35:28; 24:67; 22:22; 28:2-6; 30:20; 31:18; 33:18; 46:15; 24:29; Kum 26:5Isaki alikuwa na umri wa miaka arobaini alipomwoa Rebeka binti Bethueli Mwaramu kutoka Padan-Aramu, nduguye Labani Mwaramu.

2125:21 Mwa 30:17, 22; 11:30; Ezr 8:23; 1Sam 1:17, 23; 1Nya 5:20; 2Nya 33:13; Za 127:3Isaki akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, kwa sababu alikuwa tasa. Bwana akajibu maombi yake na Rebeka mkewe akapata mimba. 2225:22 Kut 18:15; 28:30; 33:7; Law 24:12; Hes 9:6-8; 27:5; Kum 17:9; 2Fal 3:11; 22:13; Isa 30:2; Yer 21:2; 37:7; Eze 14:7; 2Watoto wakashindana tumboni mwake, akasema, “Kwa nini haya yanatokea kwangu?” Kwa hiyo akaenda kumuuliza Bwana.

23Bwana akamjibu,

“Mataifa mawili yamo tumboni mwako,

na mataifa hayo mawili

kutoka ndani yako watatenganishwa.

Mmoja atakuwa na nguvu zaidi kuliko mwingine,

na yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.”

24Wakati wake wa kujifungua ulipotimia, walikuwepo mapacha wa kiume tumboni mwake. 25Wa kwanza kuzaliwa alikuwa mwekundu, mwili wake wote ulikuwa kama mtu aliyevaa vazi lenye nywele; wakamwita jina lake Esau.25:25 Esau maana yake Mwenye nywele nyingi. 26Baadaye, ndugu yake akatoka, mkono wake ukiwa umemshika Esau kisigino; akaitwa jina lake Yakobo.25:26 Yakobo maana yake Ashikaye kisigino, au Atwaaye mahali pa mwingine, au Mdanganyaji, au Mwenye hila, au Mlaghai, au Mjanja. Isaki alikuwa mwenye miaka sitini Rebeka alipowazaa.

27Watoto wakakua, naye Esau akakuwa mwindaji hodari, mtu wa mbugani, wakati Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa nyumbani. 28Isaki, ambaye alikuwa anapendelea zaidi nyama za porini, alimpenda Esau, bali Rebeka alimpenda Yakobo.

29Siku moja Yakobo alipika mchuzi wa dengu, Esau akarudi kutoka porini akiwa na njaa kali. 30Esau akamwambia Yakobo, “Haraka, nipe huo mchuzi mwekundu! Nina njaa kali sana!” (Hii ndiyo sababu pia aliitwa Edomu.)25:30 Edomu maana yake Mwekundu.

31Yakobo akamjibu, “Niuzie kwanza haki yako ya mzaliwa wa kwanza.”

32Esau akasema, “Tazama, mimi niko karibu ya kufa, itanifaa nini haki ya mzaliwa wa kwanza?”

33Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Hivyo Esau akamwapia, akamuuzia Yakobo haki yake ya kuzaliwa.

34Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake.

Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 25:1-34

亞伯拉罕的其他後代

1亞伯拉罕又娶了基土拉為妻。 2基土拉亞伯拉罕生了心蘭約珊米但米甸伊施巴書亞3約珊生了示巴底但底但的子孫是亞書利族、利都示族和利烏米族。 4米甸的兒子是以法以弗哈諾亞比大以勒大。這些都是基土拉的子孫。 5亞伯拉罕把所有的財產都給了以撒6他趁自己還在世的時候,把一些財物送給他的妾所生的兒子們,讓他們離開他的兒子以撒到東方去。

7亞伯拉罕活了一百七十五歲, 8享盡天年,壽終正寢,歸到他祖先那裡。 9他的兩個兒子以撒以實瑪利把他安葬在麥比拉洞,那山洞在幔利附近、瑣轄的兒子以弗崙的地裡。 10那塊地是亞伯拉罕人買的,他和妻子撒拉都葬在那裡。 11亞伯拉罕去世以後,上帝賜福給他的兒子以撒以撒住在庇耳·拉海·萊附近。

12以實瑪利亞伯拉罕撒拉的婢女埃及夏甲所生的兒子,以下是以實瑪利的後代。 13以實瑪利的兒子按出生的次序名字如下:長子尼拜約,然後是基達亞德別米比衫14米施瑪度瑪瑪撒15哈大提瑪伊突拿非施基底瑪16這些都是以實瑪利的兒子,他們按照其村莊和營寨分別作了十二個族的族長。 17以實瑪利活了一百三十七歲,壽終正寢,歸到他祖先那裡。 18他子孫居住的地方從哈腓拉一直延伸到埃及東面、通往亞述方向的書珥,他們與其他親屬作對25·18 「與其他親屬作對」或譯「住在其他親屬的東面」。

利百加生以掃和雅各

19以下是關於亞伯拉罕的兒子以撒的記載。

亞伯拉罕以撒20以撒四十歲娶利百加利百加巴旦·亞蘭的亞蘭人彼土利的女兒、拉班的妹妹。 21以撒因為利百加不生育,就為她祈求耶和華。耶和華應允了他的祈求,利百加就懷了孕。 22兩個胎兒在她腹中彼此相爭,她說:「怎麼會這樣?」於是,她去求問耶和華。 23耶和華對她說:

「你腹中有兩個國家,

兩族從你裡面分出,

一族要比另一族強大,

將來大的要服侍小的。」

24到了生產的時候,利百加果然生下雙胞胎。 25先出生的嬰兒身體通紅,渾身長毛,好像穿了皮衣,因此給他取名叫以掃25·25 「以掃」意思是「有毛」。26隨後出生的弟弟手抓著以掃的腳跟,因此給他取名叫雅各25·26 「雅各」意思是「抓住」。。那時以撒六十歲。

以掃出賣長子名分

27孩子們漸漸長大,以掃擅長狩獵,常在田野活動;雅各性情安靜,喜歡待在家裡。 28以撒疼愛以掃,因為他喜歡吃以掃打的野味,利百加卻疼愛雅各

29一天,雅各正在熬湯,以掃筋疲力盡地從田野回來。 30以掃雅各說:「我要累死了,給我一些紅湯喝吧!」因此,以掃又叫以東25·30 「以東」意思是「紅色」。31雅各回答說:「你今天把長子的名分賣給我吧!」 32以掃說:「我都快死了,長子的名分對我有什麼用呢?」 33雅各說:「你現在向我起誓保證吧!」於是,以掃就起誓把長子的名分賣給了雅各34雅各把餅和豆湯給以掃以掃吃完喝完便起身走了。以掃就這樣輕看自己長子的名分。