Mithali 7 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 7:1-27

Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi

17:1 Mt 1:8Mwanangu, shika maneno yangu

na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

27:2 Mit 4:4; Law 18:5; Kum 32:10Shika amri zangu nawe utaishi;

linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

37:3 Kum 6:8; Mit 3:3; Isa 30:8; 2Kor 3:3Yafunge katika vidole vyako;

yaandike katika kibao cha moyo wako.

4Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”

uite ufahamu jamaa yako;

57:5 Ay 31:9; Mit 2:16watakuepusha na mwanamke mzinzi,

kutokana na mwanamke mpotovu

na maneno yake ya kubembeleza.

6Kwenye dirisha la nyumba yangu

nilitazama nje kupitia upenyo

kwenye mwimo wa dirisha.

77:7 Mit 6:32Niliona miongoni mwa wajinga,

nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,

kijana asiye na akili.

8Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,

akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

97:9 Ay 24:15wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,

giza la usiku lilipokuwa likiingia.

107:10 1Tim 2:9Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,

hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

117:11 Mit 9:13; 1Tim 5:13(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,

miguu yake haitulii nyumbani;

127:12 Mit 8:1-36; 23:26-28mara kwenye barabara za mji,

mara kwenye viwanja vikubwa,

kwenye kila pembe huvizia.)

137:13 Mwa 39:12; Mit 1:20Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,

na kwa uso usio na haya akamwambia:

147:14 Law 7:11-18“Nina sadaka za amani nyumbani;

leo nimetimiza nadhiri zangu.

15Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;

nimekutafuta na nimekupata!

167:16 Isa 19:9Nimetandika kitanda changu

kwa kitani za rangi kutoka Misri.

177:17 Amo 6:4; Mwa 37:25Nimetia manukato kitanda changu

kwa manemane, udi na mdalasini.

187:18 Mwa 39:7Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;

tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!

19Mume wangu hayupo nyumbani;

amekwenda safari ya mbali.

20Amechukua mkoba uliojazwa fedha

na hatakuwepo nyumbani karibuni.”

217:21 Mit 1:8-9; 8:32Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;

alimshawishi kwa maneno yake laini.

227:22 Ay 18:10Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke

kama fahali aendaye machinjoni,

kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,

237:23 Ay 15:22; 16:13; Mit 6:26; Mhu 9:12mpaka mshale umchome ini lake,

kama ndege anayenaswa kwenye mtego,

bila kujua itamgharimu maisha yake.

247:24 Mit 1:8-9; 8:32Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

sikilizeni kwa makini nisemalo.

257:25 Mit 5:7-8Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,

wala usitangetange katika mapito yake.

267:26 Neh 13:26Aliowaangusha ni wengi;

aliowachinja ni kundi kubwa.

277:27 Amu 16:19; Ufu 22:15Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.

New Arabic Version

الأمثال 7:1-27

تحذير من إغواء الزانية

1يَا ابْنِي احْفَظْ أَقْوَالِي وَاذْخَرْ وَصَايَايَ مَعَكَ. 2أَطِعْ وَصَايَايَ فَتَحْيَا، وَصُنْ شَرِيعَتِي كَحَدَقَةِ عَيْنِكَ. 3اعْصِبْهَا عَلَى أَصَابِعِكَ، وَاكْتُبْهَا عَلَى صَفْحَاتِ قَلْبِكَ. 4قُلْ لِلْحِكْمَةِ: أَنْتِ أُخْتِي، وَلِلْفِطْنَةِ: أَنْتِ قَرِيبَتِي. 5فَهُمَا تَحْفَظَانِكَ مِنَ الْمَرْأَةِ الْعَاهِرَةِ، وَالزَّوْجَةِ الْفَاسِقَةِ الَّتِي تَتَمَلَّقُ بِكَلامِهَا.

6فَإِنِّي أَشْرَفْتُ مِنْ كُوَّةِ بَيْتِي، وَأَطْلَلْتُ مِنْ خِلالِ نَافِذَتِي، 7فَشَاهَدْتُ بَيْنَ الْبَنِينَ الْحَمْقَى شَابّاً مُجَرَّداً مِنَ الْفَهْمِ، 8يَجْتَازُ الطَّرِيقَ صَوْبَ الْمُنْعَطَفِ، بِاتِّجَاهِ الشَّارِعِ الْمُفْضِي إِلَى بَيْتِهَا. 9عِنْدَ الْغَسَقِ فِي الْمَسَاءِ تَحْتَ جُنْحِ اللَّيْلِ وَالظُّلْمَةِ. 10فَإِذَا بِامْرَأَةٍ تَسْتَقْبِلُهُ فِي زِيِّ زَانِيَةٍ وَقَلْبٍ مُخَادِعٍ. 11صَخَّابَةٌ وَجَامِحَةٌ لَا تَسْتَقِرُّ قَدَمَاهَا فِي بَيْتِهَا. 12تَرَاهَا تَارَةً فِي الْخَارِجِ، وَطَوْراً فِي سَاحَاتِ الأَسْوَاقِ، تَكْمُنُ عِنْدَ كُلِّ مُنْعَطَفٍ. 13فَأَمْسَكَتْهُ وَقَبَّلَتْهُ وَقَالَتْ لَهُ بِوَجْهٍ وَقِحٍ: 14«كَانَ عَلَيَّ أَنْ أُقَدِّمَ ذَبَائِحَ سَلامٍ، فَأَوْفَيْتُ الْيَوْمَ نُذُورِي. 15وَقَدْ خَرَجْتُ لاِسْتِقْبَالِكَ، بَعْدَ أَنْ بَحَثْتُ بِشَوْقٍ عَنْكَ حَتَّى وَجَدْتُكَ. 16قَدْ فَرَشْتُ سَرِيرِي بِأَغْطِيَةٍ كَتَّانِيَّةٍ مُوَشَّاةٍ مِنْ مِصْرَ، 17وَعَطَّرْتُ فِرَاشِي بِطِيبِ الْمُرِّ وَالْقِرْفَةِ. 18فَتَعَالَ لِنَرْتَوِيَ مِنَ الْحُبِّ حَتَّى الصَّبَاحِ، وَنَتَلَذَّذَ بِمُتَعِ الْغَرَامِ. 19فَإِنَّ زَوْجِي لَيْسَ فِي الْبَيْتِ، قَدْ مَضَى فِي رِحْلَةٍ بَعِيدَةٍ. 20وَأَخَذَ مَعَهُ صُرَّةً مُكْتَنِزَةً بِالْمَالِ، وَلَنْ يَعُودَ إِلّا عِنْدَ اكْتِمَالِ الْبَدْرِ». 21فَأَغْوَتْهُ بِكَثْرَةِ أَفَانِينِ كَلامِهَا، وَرَنَّحَتْهُ بِتَمَلُّقِ شَفَتَيْهَا. 22فَمَضَى عَلَى التَّوِّ فِي إِثْرِهَا، كَثَوْرٍ مَسُوقٍ إِلَى الذَّبْحِ، أَوْ أَيِّلٍ وَقَعَ فِي فَخٍّ. 23إِلَى أَنْ يَنْفُذَ سَهْمٌ فِي كَبِدِهِ، وَيَكُونَ كَعُصْفُورٍ مُنْدَفِعٍ إِلَى شَرَكٍ، لَا يَدْرِي أَنَّهُ قَدْ نُصِبَ لِلْقَضَاءِ عَلَيْهِ.

24وَالآنَ أَصْغُوا إِلَيَّ أَيُّهَا الأَبْنَاءُ، وَأَرْهِفُوا آذَانَكُمْ إِلَى أَقْوَالِ فَمِي: 25لَا تَجْنَحْ قُلُوبُكُمْ نَحْوَ طُرُقِهَا، وَلا تُحَوِّمْ فِي دُرُوبِهَا. 26فَمَا أَكْثَرَ الَّذِينَ طَرَحَتْهُمْ مُثْخَنِينَ بِالْجِرَاحِ، وَجَمِيعُ صَرْعَاهَا أَقْوِيَاءُ. 27إِنَّ بَيْتَهَا هُوَ طَرِيقُ الْهَاوِيَةِ الْمُؤَدِّي إِلَى مَخَادِعِ الْمَوْتِ.