Hekima Ni Bora Kupita Vitu Vyote
14:1 Mit 1:8; 19:20; Ay 8:10Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;
sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
2Ninawapa mafundisho ya maana,
kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
34:3 1Nya 29:1; 2Sam 12:24Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,
ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
44:4 Mit 7:2; 1Nya 28:9baba alinifundisha akisema,
“Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote;
yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
54:5 Mit 3:13-18; 16:16Pata hekima, pata ufahamu;
usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
64:6 2The 2:10; Mit 2:11Usimwache hekima naye atakuweka salama;
mpende, naye atakulinda.
74:7 Mt 13:44-46; Mit 23:23Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.
Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
84:8 1Sam 2:30; Mit 3:18Mstahi, naye atakukweza;
mkumbatie, naye atakuheshimu.
94:9 Mit 1:8-9Atakuvika shada la neema kichwani mwako
na kukupa taji ya utukufu.”
104:10 Kum 11:21; Mit 3:2Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,
nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
114:11 1Sam 12:23; 2Sam 22:37; Za 5:8Ninakuongoza katika njia ya hekima
na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
124:12 Ay 18:7; Yer 13:16; Za 18:36Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;
ukimbiapo, hutajikwaa.
134:13 Mit 3:22Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
mshike, maana yeye ni uzima wako.
144:14 Za 1:1; Mit 1:15Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu
wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
15Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;
achana nayo, na uelekee njia yako.
164:16 Za 36:4; Mik 7:3Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;
wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
174:17 Mwa 49:5; Za 73:6; Mit 1:10-19; Isa 59:6; Yer 22:3; Hab 1:2; Mal 2:16Wanakula mkate wa uovu,
na kunywa mvinyo wa jeuri.
184:18 Mt 5:14; Ay 17:9; Isa 26:7; Dan 12:3; Yn 8:12Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,
ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
194:19 Ay 18:5; Yn 12:35Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;
hawajui kinachowafanya wajikwae.
204:20 Za 34:11-16; Mit 1:8-9; 5:1Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;
sikiliza kwa makini maneno yangu.
214:21 Mit 3:21Usiruhusu yaondoke machoni pako,
yahifadhi ndani ya moyo wako;
224:22 Mit 3:8kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata
na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
234:23 Mit 10:11; Mt 12:34Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,
maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24Epusha kinywa chako na ukaidi;
weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
254:25 Ay 31:1Macho yako na yatazame mbele,
kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
264:26 Ebr 12:13Sawazisha mapito ya miguu yako
na njia zako zote ziwe zimethibitika.
274:27 Law 10:11; Kum 28:14Usigeuke kulia wala kushoto;
epusha mguu wako na ubaya.