Matendo 12 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Matendo 12:1-25

Yakobo Auawa, Petro Atiwa Gerezani

112:1 Mt 14:1Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa. 212:2 Mt 4:21; Mk 10:39Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga. 312:3 Mdo 24:27; 25:9; Kut 12:15; 23:15; Mdo 20:6Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. 412:4 Yn 11:15Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.

512:5 Mdo 1:14; Efe 6:18Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.

612:6 Mdo 21:33Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza. 712:7 Mdo 5:19; Za 107:14; Mdo 16:26Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.

8Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.” 912:9 Mdo 9:10Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono. 1012:10 Mdo 5:19; 16:26Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.

1112:11 Lk 15:17; Za 34:7; Dan 3:28; 6:22; 2Kor 11:10; 2Pet 2:9Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”

1212:12 Mdo 12:25; 15:37; Kol 4:10; 2Tim 4:11; 1Pet 5:13Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi. 1312:13 Yn 18:16Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia. 1412:14 Lk 24:41Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”

1512:15 Mt 18:10Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”

16Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana. 1712:17 Mdo 19:33; 21:40Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.

1812:18 Mdo 5:21, 22Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro. 1912:19 Mdo 8:1-4; 16:27; 8:40Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.

Kifo Cha Herode Agripa

2012:20 Mt 11:21; 1Fal 5:9, 11; Eze 27:17Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.

21Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu. 2212:22 Eze 28:2Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.” 2312:23 Mdo 5:19; 1Sam 25:38; 2Sam 24:16; 2Fal 19:35Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.

2412:24 Ebr 4:12; Mdo 6:7; 19:20Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.

2512:25 Mdo 4:36; 11:30; 12:12Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.

New International Version

Acts 12:1-25

Peter’s Miraculous Escape From Prison

1It was about this time that King Herod arrested some who belonged to the church, intending to persecute them. 2He had James, the brother of John, put to death with the sword. 3When he saw that this met with approval among the Jews, he proceeded to seize Peter also. This happened during the Festival of Unleavened Bread. 4After arresting him, he put him in prison, handing him over to be guarded by four squads of four soldiers each. Herod intended to bring him out for public trial after the Passover.

5So Peter was kept in prison, but the church was earnestly praying to God for him.

6The night before Herod was to bring him to trial, Peter was sleeping between two soldiers, bound with two chains, and sentries stood guard at the entrance. 7Suddenly an angel of the Lord appeared and a light shone in the cell. He struck Peter on the side and woke him up. “Quick, get up!” he said, and the chains fell off Peter’s wrists.

8Then the angel said to him, “Put on your clothes and sandals.” And Peter did so. “Wrap your cloak around you and follow me,” the angel told him. 9Peter followed him out of the prison, but he had no idea that what the angel was doing was really happening; he thought he was seeing a vision. 10They passed the first and second guards and came to the iron gate leading to the city. It opened for them by itself, and they went through it. When they had walked the length of one street, suddenly the angel left him.

11Then Peter came to himself and said, “Now I know without a doubt that the Lord has sent his angel and rescued me from Herod’s clutches and from everything the Jewish people were hoping would happen.”

12When this had dawned on him, he went to the house of Mary the mother of John, also called Mark, where many people had gathered and were praying. 13Peter knocked at the outer entrance, and a servant named Rhoda came to answer the door. 14When she recognized Peter’s voice, she was so overjoyed she ran back without opening it and exclaimed, “Peter is at the door!”

15“You’re out of your mind,” they told her. When she kept insisting that it was so, they said, “It must be his angel.”

16But Peter kept on knocking, and when they opened the door and saw him, they were astonished. 17Peter motioned with his hand for them to be quiet and described how the Lord had brought him out of prison. “Tell James and the other brothers and sisters about this,” he said, and then he left for another place.

18In the morning, there was no small commotion among the soldiers as to what had become of Peter. 19After Herod had a thorough search made for him and did not find him, he cross-examined the guards and ordered that they be executed.

Herod’s Death

Then Herod went from Judea to Caesarea and stayed there. 20He had been quarreling with the people of Tyre and Sidon; they now joined together and sought an audience with him. After securing the support of Blastus, a trusted personal servant of the king, they asked for peace, because they depended on the king’s country for their food supply.

21On the appointed day Herod, wearing his royal robes, sat on his throne and delivered a public address to the people. 22They shouted, “This is the voice of a god, not of a man.” 23Immediately, because Herod did not give praise to God, an angel of the Lord struck him down, and he was eaten by worms and died.

24But the word of God continued to spread and flourish.

Barnabas and Saul Sent Off

25When Barnabas and Saul had finished their mission, they returned from12:25 Some manuscripts to Jerusalem, taking with them John, also called Mark.