Kutoka 1 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 1:1-22

Waisraeli Waonewa

11:1 Mwa 46:8Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake: 2Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda; 3Isakari, Zabuloni na Benyamini; 41:4 Mwa 35:22-26; Hes 1:20-43Dani na Naftali, Gadi na Asheri. 51:5 Mwa 46:26Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.

61:6 Mwa 50:26; Mdo 7:15Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa, 71:7 Mwa 12:2; Kum 7:13; Eze 16:7lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.

81:8 Yer 43:11; 46:2Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri. 91:9 Mwa 26:16Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi. 101:10 Mwa 15:13; Kut 3:7; 18:11; Za 64:2; 71:10; 83:3; 105:24-25; Isa 53:3; Mdo 7:17-19Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”

111:11 Kut 3:7; 5:4, 10-14; 6:6-7; 2:11; Mwa 15:13; 47:11; Yos 9:27; Isa 60:10; 1Fal 9:19, 21; 1Nya 22:2; 2Nya 8:4Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao. 12Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli, 131:13 Mwa 15:13-14; Kut 5:21; 16:3; Law 25:43-53; Kum 4:20; 26:6; 1Fal 8:15; Za 129:1; Isa 30:6; 48:10; Yer 11:4kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili. 141:14 Kum 26:6; Ezr 9:9; Isa 14:3; Mwa 11:3; Kut 2:23; 3:9; Hes 20:15; Mdo 7:19; 1Sam 10:11; 2Sam 13:4Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.

151:15 Mwa 35:17Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua, 16“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.” 171:17 Mit 16:6; 1Sam 22:17; Dan 3:16-18; Mdo 4:18-20; 5:29Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi. 18Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”

191:19 Law 19:11; Yos 2:4-6; 1Sam 19:14; 2Sam 17:20Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”

201:20 Mit 11:18; 22:8; Mhu 8:12; Isa 3:10; Ebr 6:10Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi. 211:21 1Sam 2:35; 2Sam 7:11, 27-29; 1Fal 11:38; 14:10Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.

221:22 Mwa 41:1; Mdo 7:19Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”

Swedish Contemporary Bible

2 Moseboken 1:1-22

Uttåget ur Egypten

(1:1—15:21)

1Här följer namnen på Israels söner, som tillsammans med sina familjer följde med Jakob till Egypten:

2Ruben, Simon, Levi, Juda, 3Isaskar, Sebulon, Benjamin, 4Dan, Naftali, Gad och Asher.

5Hela antalet som härstammade från honom var sjuttio personer. Josef var ju redan i Egypten. 6Så småningom dog Josef och hans bröder och hela deras generation. 7Men israeliterna var mycket fruktsamma, ökade snabbt i antal och blev oerhört många. Snart uppfyllde de hela landet.

8Men då fick Egypten en ny kung1:8 Antagligen en ny dynasti., en som inte kände till Josef. 9”De där israeliterna blir för många och för starka för oss”, sa han till sitt folk. 10”Vi måste handla klokt, så att de inte blir ännu fler. Om det blir krig skulle de kunna förena sig med våra fiender och strida mot oss, och sedan fly ut ur landet.”

11Därför satte de slavdrivare över israeliterna för att kuva dem med hårt arbete. De tvingades bygga upp faraos förrådsstäder Pitom och Ramses. 12Men ju mer israeliterna förtrycktes, desto mer ökade de i antal och bredde ut sig, så att egypterna började frukta dem. 13De tvingade dem till slavarbete 14och deras liv förbittrades av det tunga arbetet med lera och tegel och all sorts arbete på fälten, alltihop påtvingat slitgöra.

15Kungen i Egypten talade till de hebreiska barnmorskorna Shifra och Pua 16och befallde dem att när de hjälpte de hebreiska kvinnorna vid förlossningen, skulle de se efter om det var en pojke och då döda honom fast låta flickorna leva. 17Men barnmorskorna fruktade Gud och gjorde inte som kungen hade sagt. De lät även pojkarna få leva. 18Då kallade kungen dem till sig och frågade: ”Varför gör ni så här, låter pojkarna leva?”

19”De hebreiska kvinnorna är inte som de egyptiska. De är starka och föder sina barn snabbt”, svarade de honom. ”Barnmorskan hinner aldrig fram i tid.”

20Gud beskyddade barnmorskorna, och folket fortsatte att föröka sig och blev allt fler. 21Eftersom barnmorskorna fruktade Gud, gav han dem också egna familjer.

22Då befallde farao hela sitt folk att kasta alla nyfödda pojkar i Nilen men låta flickorna leva.