Jina Jipya La Sayuni
1Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza,
kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,
mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,
wokovu wake kama mwanga wa moto.
262:2 Isa 1:26; Za 67:2; Ufu 3:12; Mwa 32:28; Ufu 2:7; Es 4:14; Za 50:12Mataifa wataona haki yako,
nao wafalme wote wataona utukufu wako;
wewe utaitwa kwa jina jipya
lile ambalo kinywa cha Bwana kitatamka.
362:3 Zek 9:16; 1The 2:19; Isa 28:5Utakuwa taji ya fahari mkononi mwa Bwana,
taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.
462:4 Law 26:43; 1Pet 2:10; Hos 2:19; Yer 3:14; Sef 3:17; Mal 3:12; Isa 6:12; 54:6Hawatakuita tena Aliyeachwa,
wala nchi yako kuiita Ukiwa.
Bali utaitwa Hefsiba,62:4 Hefsiba maana yake Yeye ninayemfurahia.
nayo nchi yako itaitwa Beula,62:4 Beula maana yake Aliyeolewa.
kwa maana Bwana atakufurahia,
nayo nchi yako itaolewa.
562:5 Kum 28:63; Wim 3:11; Isa 65:19; Yer 31:12; Sef 3:17Kama vile kijana aoavyo mwanamwali,
ndivyo wanao62:5 Au: wajenzi wako. watakavyokuoa wewe;
kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,
ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
662:6 Eze 3:17; Ebr 13:17; Isa 52:8; Za 132:4Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, ee Yerusalemu,
hawatanyamaza mchana wala usiku.
Ninyi wenye kumwita Bwana,
msitulie,
762:7 Mt 15:21-28; Sef 3:20; Lk 18:1-8; Isa 60:18; Kum 26:19msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu
na kuufanya uwe sifa ya dunia.
862:8 Kum 28:30-33; Yer 5:17; Mwa 22:16; Isa 14:25; 49:18Bwana ameapa kwa mkono wake wa kuume
na kwa mkono wake wenye nguvu:
“Kamwe sitawapa tena adui zenu
nafaka zenu kama chakula chao;
kamwe wageni hawatakunywa tena
divai mpya ambayo mmeitaabikia,
9lakini wale waivunao nafaka wataila
na kumsifu Bwana,
nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake
katika nyua za patakatifu pangu.”
1062:10 Isa 11:10-16; 57:14; Za 24:7; Isa 60:11Piteni, piteni katika malango!
Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.
Jengeni, jengeni njia kuu!
Ondoeni mawe.
Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.
1162:11 Amo 9:14; Kum 12:7; Yoe 2:26; Isa 1:10Bwana ametoa tangazo
mpaka miisho ya dunia:
“Mwambie Binti Sayuni,
‘Tazama, mwokozi wako anakuja!
Tazama ujira wake uko pamoja naye,
na malipo yake yanafuatana naye!’ ”
1262:12 Za 9:14; Mt 21:5; Isa 35:4; Ufu 22:12; Kum 30:4; Zek 9:9; Isa 40:10Wataitwa Watu Watakatifu,
Waliokombolewa na Bwana;
nawe utaitwa Aliyetafutwa,
Mji Usioachwa Tena.
錫安蒙主喜悅
1為了錫安我不再緘默,
為了耶路撒冷我不再沉默,
直到她的公義如明光照耀,
她的救恩如燃燒的火把。
2耶路撒冷啊,
列國必看見你的公義,
列王必看見你的榮耀,
耶和華必親口賜你一個新名字。
3你必成為耶和華手中的華冠,
你上帝手上的榮冕。
4你不再被稱為「棄婦」,
你的土地不再被稱為「荒涼之地」。
你要被稱為「主所喜悅的」,
你的土地要被稱為「有夫之婦」,
因為耶和華必喜愛你,
做你土地的丈夫。
5你的人民必娶你,
好像少男娶少女;
上帝必喜愛你,
如同新郎喜愛新娘。
6耶路撒冷啊,
我已在你城牆上設立守望者。
他們晝夜不停地禱告。
呼求耶和華的人啊,
你們不可歇息,
7要常常敦促祂,
直到祂建立耶路撒冷,
使耶路撒冷得到普世的讚美。
8耶和華憑祂的右手,憑祂大能的臂膀起誓說:
「我再也不會把你的五穀給你的仇敵吃,
再也不會讓外族人喝你辛苦釀製的新酒。
9收割的人必享受五穀,
讚美耶和華,
摘葡萄的人必在我聖所的院內喝酒。」
10你們要出去,去城外,
為百姓修平道路。
你們要修築,修築大道,
清除石頭,
為萬民豎立旗幟。
11看啊,耶和華已經向普世宣告:「要對少女錫安說,
『看啊,你的拯救者帶著獎賞和報酬來了!』」
12他們將被稱為聖民,是耶和華救贖的人。
你將被稱為蒙眷愛、不再被撇棄的城。