Isaya 62 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 62:1-12

Jina Jipya La Sayuni

1Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza,

kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,

mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,

wokovu wake kama mwanga wa moto.

262:2 Isa 1:26; Za 67:2; Ufu 3:12; Mwa 32:28; Ufu 2:7; Es 4:14; Za 50:12Mataifa wataona haki yako,

nao wafalme wote wataona utukufu wako;

wewe utaitwa kwa jina jipya

lile ambalo kinywa cha Bwana kitatamka.

362:3 Zek 9:16; 1The 2:19; Isa 28:5Utakuwa taji ya fahari mkononi mwa Bwana,

taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.

462:4 Law 26:43; 1Pet 2:10; Hos 2:19; Yer 3:14; Sef 3:17; Mal 3:12; Isa 6:12; 54:6Hawatakuita tena Aliyeachwa,

wala nchi yako kuiita Ukiwa.

Bali utaitwa Hefsiba,62:4 Hefsiba maana yake Yeye ninayemfurahia.

nayo nchi yako itaitwa Beula,62:4 Beula maana yake Aliyeolewa.

kwa maana Bwana atakufurahia,

nayo nchi yako itaolewa.

562:5 Kum 28:63; Wim 3:11; Isa 65:19; Yer 31:12; Sef 3:17Kama vile kijana aoavyo mwanamwali,

ndivyo wanao62:5 Au: wajenzi wako. watakavyokuoa wewe;

kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,

ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

662:6 Eze 3:17; Ebr 13:17; Isa 52:8; Za 132:4Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, ee Yerusalemu,

hawatanyamaza mchana wala usiku.

Ninyi wenye kumwita Bwana,

msitulie,

762:7 Mt 15:21-28; Sef 3:20; Lk 18:1-8; Isa 60:18; Kum 26:19msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu

na kuufanya uwe sifa ya dunia.

862:8 Kum 28:30-33; Yer 5:17; Mwa 22:16; Isa 14:25; 49:18Bwana ameapa kwa mkono wake wa kuume

na kwa mkono wake wenye nguvu:

“Kamwe sitawapa tena adui zenu

nafaka zenu kama chakula chao;

kamwe wageni hawatakunywa tena

divai mpya ambayo mmeitaabikia,

9lakini wale waivunao nafaka wataila

na kumsifu Bwana,

nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake

katika nyua za patakatifu pangu.”

1062:10 Isa 11:10-16; 57:14; Za 24:7; Isa 60:11Piteni, piteni katika malango!

Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.

Jengeni, jengeni njia kuu!

Ondoeni mawe.

Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.

1162:11 Amo 9:14; Kum 12:7; Yoe 2:26; Isa 1:10Bwana ametoa tangazo

mpaka miisho ya dunia:

“Mwambie Binti Sayuni,

‘Tazama, mwokozi wako anakuja!

Tazama ujira wake uko pamoja naye,

na malipo yake yanafuatana naye!’ ”

1262:12 Za 9:14; Mt 21:5; Isa 35:4; Ufu 22:12; Kum 30:4; Zek 9:9; Isa 40:10Wataitwa Watu Watakatifu,

Waliokombolewa na Bwana;

nawe utaitwa Aliyetafutwa,

Mji Usioachwa Tena.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

以賽亞書 62:1-12

錫安蒙主喜悅

1為了錫安我不再緘默,

為了耶路撒冷我不再沉默,

直到她的公義如明光照耀,

她的救恩如燃燒的火把。

2耶路撒冷啊,

列國必看見你的公義,

列王必看見你的榮耀,

耶和華必親口賜你一個新名字。

3你必成為耶和華手中的華冠,

你上帝手上的榮冕。

4你不再被稱為「棄婦」,

你的土地不再被稱為「荒涼之地」。

你要被稱為「主所喜悅的」,

你的土地要被稱為「有夫之婦」,

因為耶和華必喜愛你,

做你土地的丈夫。

5你的人民必娶你,

好像少男娶少女;

上帝必喜愛你,

如同新郎喜愛新娘。

6耶路撒冷啊,

我已在你城牆上設立守望者。

他們晝夜不停地禱告。

呼求耶和華的人啊,

你們不可歇息,

7要常常敦促祂,

直到祂建立耶路撒冷

使耶路撒冷得到普世的讚美。

8耶和華憑祂的右手,憑祂大能的臂膀起誓說:

「我再也不會把你的五穀給你的仇敵吃,

再也不會讓外族人喝你辛苦釀製的新酒。

9收割的人必享受五穀,

讚美耶和華,

摘葡萄的人必在我聖所的院內喝酒。」

10你們要出去,去城外,

為百姓修平道路。

你們要修築,修築大道,

清除石頭,

為萬民豎立旗幟。

11看啊,耶和華已經向普世宣告:「要對少女錫安說,

『看啊,你的拯救者帶著獎賞和報酬來了!』」

12他們將被稱為聖民,是耶和華救贖的人。

你將被稱為蒙眷愛、不再被撇棄的城。