Isaya 54 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 54:1-17

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

154:1 Isa 49:20; Gal 4:27; Mwa 21:6; Za 98:4; Isa 66:7; 49:20“Imba, ewe mwanamke tasa,

wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;

paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,

wewe ambaye kamwe hukupata utungu;

kwa sababu watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume,”

asema Bwana.

254:2 Mwa 26:22; Isa 26:15; Kut 35:18; 39:40; Isa 49:19-20“Panua mahali pa hema lako,

tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,

wala usiyazuie;

ongeza urefu wa kamba zako,

imarisha vigingi vyako.

354:3 Mwa 13:14; Isa 48:19; Ay 12:23; Isa 14:2; 60:4-11; 49:19Kwa maana utaenea upande wa kuume

na upande wa kushoto;

wazao wako watayamiliki mataifa

na kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

454:4 Isa 30:10; Yoe 2:21; Isa 28:16; Mwa 30:23; Za 25:7; 119:39; Yer 22:21; Isa 47:8“Usiogope, wewe hutaaibika.

Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.

Wewe utasahau aibu ya ujana wako,

wala hutakumbuka tena mashutumu ya ujane wako.

554:5 Wim 3:3; Isa 41:14; 48:17; Rum 3:29; Hos 2:7-16; Za 149:2; Isa 51:13Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,

yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

654:6 Isa 49:14-21; 60:15; 62:4; Yer 44:2; Hos 1:10; Kut 20:14; Mal 2:14Bwana atakuita urudi

kana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni;

kama mke aliyeolewa bado angali kijana

na kukataliwa,” asema Mungu wako.

754:7 Ay 14:13; Isa 26:20; 2Kor 4:17; Isa 27:8; Za 71:11; Isa 49:18“Kwa kitambo kidogo nilikuacha,

lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

854:8 Isa 9:12; Yer 31:3; Za 92:2; Isa 26:20; Za 25:6; Isa 55:3; 63:7; Hos 2:19Katika ukali wa hasira

nilikuficha uso wangu kwa kitambo,

lakini kwa fadhili za milele

nitakuwa na huruma juu yako,”

asema Bwana Mkombozi wako.

954:9 Mwa 8:21; Mik 7:18; Eze 39:29; Isa 14:24; Kum 28:20; Isa 49:18“Kwangu mimi jambo hili ni kama siku za Noa,

nilipoapa kuwa maji ya Noa kamwe hayatafunika tena dunia.

Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,

kamwe sitawakemea tena.

1054:10 Za 46:2; Ebr 12:27; Mwa 9:16; Kut 34:10; Ufu 6:14; Hes 25:12; Isa 55:7Ijapotikisika milima, na vilima viondolewe,

hata hivyo upendo wangu usiokoma kwenu hautatikisika,

wala agano langu la amani halitaondolewa,”

asema Bwana, mwenye huruma juu yenu.

1154:11 Isa 14:32; 29:6; 1Nya 29:2; Ufu 21:18; 21:19-20; Isa 26:18; 28:16; Kut 24:10“Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba na usiyetulizwa,

nitakujenga kwa almasi, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

1254:12 Ufu 21:21Nitafanya minara yako ya akiki,

malango yako kwa vito vingʼaavyo,

nazo kuta zako zote za vito vya thamani.

1354:13 Mik 4:2; Ebr 8:11; Law 26:6; Isa 11:9; 28:9; 48:18; Yn 6:45Watoto wako wote watafundishwa na Bwana,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

1454:14 2Sam 7:10; Isa 9:4; 17:14; 26:2; Yer 30:20; Sef 3:17; Zek 9:8Kwa haki utathibitika:

Kuonewa kutakuwa mbali nawe;

hutaogopa chochote.

Hofu itakuwa mbali nawe;

haitakukaribia wewe.

1554:15 Isa 41:11-16Kama mtu yeyote akikushambulia,

haitakuwa kwa ruhusa yangu;

yeyote akushambuliaye

atajisalimisha kwako.

1654:16 Isa 44:12; 10:5; 13:5“Tazama, ni mimi niliyemuumba mhunzi,

yeye afukutaye makaa kuwa moto,

na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.

Tena ni mimi niliyemwambia mharabu

kufanya uharibifu mwingi.

1754:17 Isa 29:8; Mdo 6:10; Isa 45:24-25; 41:11; 56:6-8; Zek 1:20-21; Isa 65:8-9Hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yako

itakayofanikiwa,

nawe utauthibitisha kuwa mwongo

kila ulimi utakaokushtaki.

Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana

na hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”

asema Bwana.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 54:1-17

主爱不移

1耶和华说:“不生育、未生养的妇人啊,要欢唱;

未曾生产的女子啊,

要欢呼高歌;

因为没有丈夫的比有丈夫的儿女更多。

2要扩大你支帐篷的地方,

尽量铺开帐篷的幔子,

放长绳子,钉牢橛子。

3因为你要向左右扩展,

你的后裔要占据列国,

使荒凉的城邑重新有人居住。

4“不要害怕,因为你不会再受羞辱;

不要恐惧,因为你不会再受凌辱。

你必忘记年轻时的羞辱,

不再想起寡居时的耻辱。

5因为造你的是你的丈夫,

祂名叫万军之耶和华;

你的救赎主是以色列的圣者,

祂被称为普天下的上帝。

6耶和华要召你回来,

如同召一个遭遗弃、

心中忧伤的少妻。

这是你的上帝说的。

7我丢弃了你片刻,

但我要怀着极大的怜悯接你回来。

8我盛怒之下暂时掩面不理你,

但我要以永远不变的慈爱怜悯你。

这是你的救赎主耶和华说的。

9“这对我而言就像挪亚的时代,

我怎样起誓不再让挪亚时代的洪水淹没大地,

我也照样起誓不再向你发怒,

也不再斥责你。

10大山可以挪开,

小山可以迁移,

但我的慈爱必不离开你,

我平安的约也不会更改。

这是怜悯你的耶和华说的。

11“困苦不堪、饱经风雨、

得不着安慰的城啊,

我要以彩石作你的地基,

用蓝宝石建造你的根基,

12用红宝石建你的城楼、

水晶造你的城门、

宝石建你的城墙。

13你的儿女都必受耶和华的训诲,

安享太平。

14你必因公义而坚立,

再不会受欺压,

也不会担惊受怕,

因为恐惧不会临近你。

15倘若有人来攻打你,

那必不是我的旨意。

攻打你的必然失败。

16看啊,是我造了扇旺炭火、

铸造合用兵器的铁匠,

是我造了毁灭者。

17为攻击你而造的兵器必不能奏效,

你必驳倒所有控告你的人。

这是耶和华众仆人的产业,

是我给他们的胜利54:17 “胜利”或译“公义”。

这是耶和华说的。”