Isaya 34 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 34:1-17

Hukumu Dhidi Ya Mataifa

134:1 Isa 43:9; Kum 4:26; 32:1; Za 24:1; Isa 33:13Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize;

sikilizeni kwa makini,

enyi kabila za watu!

Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake,

ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!

234:2 Isa 13:5; Zek 5:3; Isa 10:25; 30:25Bwana ameyakasirikia mataifa yote;

ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote.

Atawaangamiza kabisa,

atawatia mikononi mwa wachinjaji.

334:3 Yoe 2:20; Amo 4:10; Eze 38:22; Isa 5:25; Za 110:6; Eze 5:17; 14:19Waliouawa watatupwa nje,

maiti zao zitatoa uvundo,

milima itatota kwa damu zao.

434:4 2Pet 3:10; Yoe 2:31; Eze 32:7-8; Ay 9:7; Ufu 6:13; Isa 13:13; Mt 24:29; Ay 8:12; Mk 13:15; Isa 15:6; Ebr 1:12Nyota zote za mbinguni zitayeyuka

na anga litasokotwa kama kitabu,

jeshi lote la angani litaanguka

kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu,

kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.

534:5 Yer 49:7; 46:10; Zek 13:7; 2Sam 8:13-14; Yos 6:17; Kum 32:41-42; Amo 3:14-15; Yer 47:6; Eze 21:5; 2Nya 28:17; Amo 1:11-12; 6:11; Mal 1:4Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni,

tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu,

wale watu ambao nimeshawahukumu,

kuwaangamiza kabisa.

634:6 Kum 32:41; Law 3:9; Mwa 36:33; Isa 30:25; Yer 25:34; Ufu 19:17Upanga wa Bwana umeoga katika damu,

umefunikwa na mafuta ya nyama:

damu ya kondoo na mbuzi,

mafuta kutoka figo za kondoo dume.

Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra,

na machinjo makuu huko Edomu.

734:7 Hes 23:22; Za 68:30; 2Sam 1:22Nyati wataanguka pamoja nao,

ndama waume na mafahali wakubwa.

Nchi yao italowana kwa damu,

nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.

834:8 Isa 2:12; 1:24; 59:18; Yoe 3:4; Eze 25:12-17; Amo 1:6-10Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi,

mwaka wa malipo,

siku ya kushindania shauri la Sayuni.

934:9 Mwa 19:24Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami,

mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho,

nchi yake itakuwa lami iwakayo!

1034:10 Ufu 14:10-11; 19:3; Yer 49:18; Mal 1:3; Isa 13:20; Eze 29:12; 35:3Haitazimishwa usiku wala mchana,

moshi wake utapaa juu milele.

Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa,

hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.

1134:11 Law 11:16-18; Ufu 18:2; Mao 2:8; Amo 7:8; Kum 14:15-17; Yoe 3:19; 2Fal 21:13Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki,

bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo.

Mungu atanyoosha juu ya Edomu

kamba ya kupimia ya machafuko matupu,

na timazi ya ukiwa.

1234:12 Isa 41:11-12; Za 107:10; Ay 12:21; Isa 40:23; Eze 24:5; Yer 39:6Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote

kitakachoitwa ufalme huko,

nao wakuu wao wote watatoweka.

1334:13 Hos 9:6; Isa 32:13; 13:22; Yer 9:11; Isa 7:19; Za 44:19Miiba itaenea katika ngome za ndani,

viwawi na michongoma itaota

kwenye ngome zake.

Itakuwa maskani ya mbweha,

makao ya bundi.

1434:14 Za 74:14; Isa 13:22; Ufu 18:2Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi,

nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana;

huko viumbe vya usiku vitastarehe pia

na kujitafutia mahali pa kupumzika.

1534:15 Za 17:8; Kum 14:13Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai,

atayaangua na kutunza makinda yake

chini ya uvuli wa mabawa yake;

pia huko vipanga watakusanyika,

kila mmoja na mwenzi wake.

1634:16 Isa 30:8; Dan 7:10; Isa 1:20; 58:14; 48:13Angalieni katika gombo la Bwana na msome:

Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana,

hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake.

Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza,

na Roho wake atawakusanya pamoja.

1734:17 Za 78:55; Isa 17:14; Yer 13:25Huwagawia sehemu zao,

mkono wake huwagawanyia kwa kipimo.

Wataimiliki hata milele

na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 34:1-17

审判列国

1列国啊,近前来听吧!

列邦啊,留心听吧!

大地和地上的万物、世界和世上的一切都要听。

2因为耶和华向列国发怒,

向他们的军队发烈怒。

祂要毁灭他们,杀尽他们。

3他们必暴尸在外,

臭气熏天,

血浸山岭。

4天上的万象必融化,

穹苍像书卷卷起;

星辰陨落,

像凋零的葡萄叶,

又像枯落的无花果。

5耶和华的刀剑在天上饱饮了血后,

必降下来惩罚祂决意要毁灭的以东人。

6祂的刀沾满了血和脂肪,

是羊羔、公山羊的血和公绵羊肾脏上的脂肪。

因为耶和华在波斯拉有祭物,

以东有大杀戮。

7野牛和他们一同倒下,

牛犊与公牛一同被杀。

他们的土地被血浸透,

土壤被脂肪覆盖。

8因为这是耶和华报应的日子,

是祂为锡安报仇之年。

9以东的河流要变为沥青,

土壤要变成硫磺,

土地要成为燃烧的沥青,

10昼夜燃烧,浓烟滚滚,

永不止息。

以东必世世代代荒废,

永远人踪绝迹。

11老鹰和刺猬必占据那里,

猫头鹰和乌鸦必在那里做窝。

耶和华要用空虚的准绳丈量以东

用混沌的线锤丈量它。

12以东没有一个显贵可以称王,

那里所有的首领全都消失。

13那里的宫殿荆棘丛生,

蒺藜、刺草遍布坚城,

成了野狗的巢穴和鸵鸟的住处。

14在那里,豺狼和旷野的其他走兽出没,

野山羊对叫,

夜间的怪物在那里栖息,

找到安歇之处。

15猫头鹰在那里做窝,

下蛋,孵化,

把幼鸟保护在翅膀底下,

鸷鸟也成双成对地聚集在那里。

16你们要去查考并阅读耶和华的书卷:

以上的动物必一个不少,

无一缺少配偶。

因为这是耶和华亲口说的,

祂的灵必把它们聚在一起。

17祂亲手为它们抽签,

用准绳为它们分地。

它们必永远占据那里,

世世代代住在那里。