Unabii Dhidi Ya Kushi
118:1 Mwa 10:6; Sef 2:12; Isa 5:8; Za 68:31; Eze 29:10; Oba 1:1Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa,18:1 Au: wa nzige.
kando ya mito ya Kushi,
218:2 Mwa 10:8-9; 2Nya 12:3; Kut 2:3; Ay 9:26; Mwa 41:14iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari
kwa mashua za mafunjo juu ya maji.
Nendeni, wajumbe wepesi,
kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,
kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,
taifa gomvi lenye lugha ngeni,
ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
318:3 Za 60:4; Yer 4:21; Za 33:8; Isa 5:26; 5:26; 31:9; Yos 6:21; Amu 3:27Enyi mataifa yote ya ulimwengu,
ninyi mnaoishi duniani
wakati bendera itakapoinuliwa milimani,
mtaiona,
nayo tarumbeta itakapolia,
mtaisikia.
418:4 Hos 5:15; 2Sam 1:21; Za 133:3; Isa 64:12; 26:21; Amu 5:31; Za 18:12; Isa 26:19Hili ndilo Bwana aliloniambia:
“Nitatulia kimya na kutazama
kutoka maskani yangu,
kama joto linalometameta katika mwanga wa jua,
kama wingu la umande
katika joto la wakati wa mavuno.”
518:5 Isa 17:10-11; Eze 17:6; Isa 10:33Kwa maana, kabla ya mavuno,
wakati wa kuchanua ukishapita
na maua yakawa zabibu zinazoiva,
atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi,
naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
618:6 Yer 7:33; Eze 32:4; 39:17; Isa 37:36; 8:8; 56:9Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani
na wanyama pori,
ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi,
nao wanyama pori wakati wote wa masika.
718:7 Sef 3:10; Za 68:31; 2Nya 9:24; Isa 60:7; Mwa 41:4; 41:14Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote
kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,
kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,
kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni,
ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito,
matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
A Prophecy Against Cush
1Woe to the land of whirring wings18:1 Or of locusts
along the rivers of Cush,18:1 That is, the upper Nile region
2which sends envoys by sea
in papyrus boats over the water.
Go, swift messengers,
to a people tall and smooth-skinned,
to a people feared far and wide,
an aggressive nation of strange speech,
whose land is divided by rivers.
3All you people of the world,
you who live on the earth,
when a banner is raised on the mountains,
you will see it,
and when a trumpet sounds,
you will hear it.
4This is what the Lord says to me:
“I will remain quiet and will look on from my dwelling place,
like shimmering heat in the sunshine,
like a cloud of dew in the heat of harvest.”
5For, before the harvest, when the blossom is gone
and the flower becomes a ripening grape,
he will cut off the shoots with pruning knives,
and cut down and take away the spreading branches.
6They will all be left to the mountain birds of prey
and to the wild animals;
the birds will feed on them all summer,
the wild animals all winter.
7At that time gifts will be brought to the Lord Almighty
from a people tall and smooth-skinned,
from a people feared far and wide,
an aggressive nation of strange speech,
whose land is divided by rivers—
the gifts will be brought to Mount Zion, the place of the Name of the Lord Almighty.