Hesabu 3 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Hesabu 3:1-51

Walawi

13:1 Kut 6:27; 19:11Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.

23:2 Hes 1:20; 26:30; Kut 6:23; 1Nya 6:3Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari. 33:3 Kut 28:41; 29:30Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani. 43:4 Law 10:1-6, 12; Hes 4:28; 1Nya 24:1; Hes 26:61; Kum 4:24; Isa 66:15; 2The 1:8; Ebr 12:29Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.

5Bwana akamwambia Mose, 63:6 Kum 10:8; 31:9; 1Nya 15:2; Hes 8:6-22; 18:1-7; 2Nya 29:11“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie. 73:7 Hes 1:53; 8:19; Law 8:35Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani. 8Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani. 93:9 Hes 8:19; 18:6Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa. 103:10 Kut 30:7; 29:9; Hes 1:51; 18:7; Mdo 6:3-4; Rum 12:7; 1Sam 6:19; Hes 16:40; 18:7Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”

11Bwana akamwambia Mose, 123:12 Neh 13:12; Mal 2:4; Hes 8:14, 16-18; 16:9; Kut 13:2“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu, 133:13 Kut 13:12; Law 11:44kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”

14Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai, 153:15 Hes 1:19; 18:16; 26:62“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.” 16Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

173:17 Mwa 29:34; 46:11; Hes 1:47; 1Nya 15:4; 23:6; 2Nya 29:12; Yos 21:4-6Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi:

Gershoni, Kohathi na Merari.

183:18 Kut 6:16-17Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni:

Libni na Shimei.

193:19 Kut 6:18Koo za Wakohathi zilikuwa ni:

Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

203:20 Mwa 46:11; Kut 6:19Koo za Wamerari zilikuwa ni:

Mahli na Mushi.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.

213:21 Mwa 46:11; Kut 6:17Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni. 22Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500. 233:23 Hes 2:18Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani. 24Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 253:25 Kut 25:9; 26:14, 36; 40:2; Hes 7:1; 4:25; 1Nya 9:14-33; Ezr 8:28-30Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania, 263:26 Kut 27:9; 35:18; Hes 4:26mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.

273:27 Mwa 46:11; Kut 6:18; 1Nya 26:23; Hes 4:15, 37Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi. 283:28 Hes 4:4, 15; Kut 25:8; 30:13; 2Nya 30:19; Za 15:1; 20:2; Eze 44:27Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu. 293:29 Hes 1:53Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani. 303:30 Kut 6:22Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli. 313:31 Kut 25:10-22, 23, 31; 26:33; Kum 10:1-8; 2Nya 5:2; Yer 3:16; 1Nya 28:15; Yer 52:19; Hes 1:50; 4:5, 15; 18:3Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake. 323:32 Kut 6:23; Hes 4:19; 18:3; 20:25-28; 2Fal 25:18Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.

333:33 Kut 6:19; Mwa 46:11Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari. 34Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200. 353:35 Hes 1:53; 2:25Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani. 363:36 Hes 4:32; Kut 26:15-25; 35:20-29; 36:36; Hes 18:3Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake, 373:37 Kut 27:10-19na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.

383:38 Hes 2:3; 18:5; 1:51; 1Nya 9:27; 23:32Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.

393:39 Hes 26:62Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.

40Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao. 413:41 Law 11:44Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”

42Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru. 43Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.

44Bwana akamwambia Mose, 453:45 Hes 3:12; 1Sam 1:28“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana. 463:46 Kut 13:13; Hes 18:15Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi, 473:47 Law 27:6, 25; Kut 30:13; Hes 18:16; Eze 45:12kusanya shekeli tano3:47 Shekeli tano ni sawa na gramu 55. kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.3:47 Gera 20 ni sawa na gramu 11. 48Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”

493:49 1Tim 2:6; Tit 2:14; Gal 4:4-5; 1Pet 1:18; Ebr 9:12Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi. 503:50 1Sam 12:3-4; Mdo 20:33Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,3653:50 Shekeli 1,365 ni sawa na kilo 15.5. kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu. 51Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

New Russian Translation

Числа 3:1-51

Служение левитов при шатре

1Вот родословие Аарона и Моисея к тому времени, когда Господь говорил с Моисеем на горе Синай.

2Имена сыновей Аарона: Надав, его первенец, и Авиуд, Элеазар и Итамар. 3Это имена сыновей Аарона, помазанных священников, которых он посвятил, чтобы они служили как священники. 4Но Надав и Авиуд умерли перед Господом, когда принесли Ему чуждый огонь3:4 См. Лев. 10:1–2. в Синайской пустыне. У них не было сыновей, и лишь Элеазар с Итамаром служили как священники при жизни их отца Аарона.

5Господь сказал Моисею: 6«Приведи род Левия и представь их священнику Аарону, чтобы они помогали ему. 7Пусть они исполняют при шатре собрания обязанности за него и за всё общество, совершая службу при скинии. 8Пусть они заботятся о всей утвари шатра собрания и исполняют обязанности за израильтян, совершая службу при скинии. 9Отдай левитов Аарону и его сыновьям — они должны быть полностью переданы ему3:9 Так в большинстве древн. евр. рукописей. В некот. евр. рукописях и в одном из древн. переводов: Мне. из всех родов израильтян. 10Поставь Аарона и его сыновей, чтобы они служили как священники. Любой посторонний, который приблизится к святилищу, должен быть предан смерти».

11Еще Господь сказал Моисею: 12«Я взял левитов из всех родов израильтян вместо первенцев мужского пола. Левиты — Мои, 13потому что все первенцы — Мои. Когда Я умертвил всех первенцев в Египте, Я отделил Себе всех первенцев в Израиле — и людей, и животных. Они должны быть Моими. Я — Господь».

Перепись левитов

14Господь сказал Моисею в Синайской пустыне: 15«Пересчитай левитов по семьям и кланам. Пересчитай всех людей мужского пола возрастом от месяца и старше». 16И Моисей перечислил их по слову Господа, как ему было велено.

17Вот имена сыновей Левия: Гершон, Кааф и Мерари.

18Вот имена кланов гершонитов: Ливни и Шимей.

19Кланы каафитов: Амрам, Ицгар, Хеврон и Уззиил.

20Кланы мераритов: Махли и Муши.

Это левитские кланы по их семьям.

21От Гершона произошли кланы ливнитов и шимеитов: это кланы гершонитов.

22Всех перечисленных мужчин возрастом от месяца и старше было 7 500 человек. 23Кланы гершонитов должны были ставить лагерь на западе, позади скинии. 24Вождем гершонитских семей был Элиасаф, сын Лаеля. 25При шатре собрания заботе гершонитов были вверены скиния и ее покрытия, завеса к входу в шатер собрания, 26завесы двора, завеса к входу во двор, окружающий скинию и жертвенник, и веревки со всеми их принадлежностями.

27От Каафа произошли кланы амрамитов, ицгаритов, хевронитов и уззиилитов: это кланы каафитов.

28Всех мужчин возрастом от месяца и старше было 8 6003:28 Так в евр. тексте. В некот. евр. рукописях и в одном из древн. переводов: 8 300, см. общее количество в ст. 39. человек. Заботе каафитов было вверено святилище. 29Каафитские кланы должны были ставить лагерь с южной стороны скинии. 30Вождем семей каафитских кланов был Элицафан, сын Уззиила. 31Их заботе были вверены ковчег, стол, светильник, жертвенники, предметы святилища, которыми пользуются при служении, завеса и все принадлежности к ней. 32Главным вождем левитов был Элеазар, сын священника Аарона. Он стоял над теми, чьей заботе было вверено святилище.

33От Мерари произошли кланы махлитов и мушитов: это кланы мераритов.

34Всех исчисленных мужчин возрастом от месяца и старше было 6 200 человек. 35Вождем семей мераритских кланов был Цуриил, сын Авихаила. Они должны были вставать лагерем с северной стороны скинии. 36Мераритам было велено заботиться о брусьях скинии, ее перекладинах, столбах, основаниях, всей ее оснастке со всеми принадлежностями 37и о столбах окружающего двора с их основаниями, шатровыми кольями и веревками.

38Моисей, Аарон и его сыновья ставили лагерь к востоку от скинии, к восходу, перед шатром собрания. Они должны были заботиться о святилище за израильтян. Любого постороннего, который приближался к святилищу, нужно было предать смерти.

39Всего левитов, которых Моисей и Аарон исчислили по повелению Господа, по их семьям, всех мужчин возрастом от месяца и старше, было 22 000 человек.

Замена израильских первенцев левитами

40Господь сказал Моисею: «Посчитай всех израильских первенцев мужского пола от месяца и старше и составь список их имен. 41Отдели Мне левитов вместо всех израильских первенцев и отдели также весь скот левитов вместо всего первородного скота израильтян. Я — Господь».

42Моисей исчислил всех первенцев израильтян, как повелел ему Господь. 43Всего первенцев мужского пола от месяца и старше, перечисленных по именам, было 22 273 человека.

44Еще Господь сказал Моисею: 45«Возьми левитов вместо всех первенцев израильтян и скот левитов вместо их скота. Левиты должны быть Моими. Я — Господь. 46Чтобы выкупить 273 израильских первенца, которые превышают число левитов, 47собери за каждого по 5 шекелей3:47 Около 58 г. по шекелю святилища, который весит 20 гер. 48Отдай серебро за выкуп излишка Аарону и его сыновьям».

49Моисей собрал выкуп у тех, кто превысил число выкупленных левитами. 50У первенцев израильтян он собрал серебра на 1 365 шекелей3:50 Около 16 кг. серебра по шекелю святилища. 51Моисей отдал выкуп Аарону и его сыновьям, по слову Господа, как ему повелел Господь.