Ayubu 35 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 35:1-16

Elihu Analaumu Mtu Kujiona Kuwa Mwenye Haki

1Ndipo Elihu akasema:

235:2 Ay 33:32; 2:9; 32:2“Je, unadhani hili ni haki?

Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’

335:3 Ay 21:15; 34:9Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata,

na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’

4“Ningependa nikujibu wewe

pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.

535:5 Kum 10:14; Mwa 15:5; Ay 22:12; Za 19:1-4Tazama juu mbinguni ukaone;

yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.

635:6 Ay 7:20; Mit 8:36Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu?

Kama dhambi zako zikiwa nyingi,

hilo linamfanyia nini Mungu?

735:7 Rum 11:35; Mit 9:12; 1Kor 4:7; Lk 17:10Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini,

au yeye anapokea nini mkononi kwako?

835:8 Eze 18:24; 18:5-9; Zek 7:9-10Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe,

nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.

935:9 Kut 2:23; Ay 5:15; 12:19; Lk 18:3-7“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso;

huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

1035:10 Ay 4:17; Isa 51:13; Za 77:6; Mdo 16:25; 1Pet 4:19Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu,

yeye anifanyaye niimbe usiku,

1135:11 Za 94:12; Lk 12:24; Ay 32:8yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia,

na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’

1235:12 1Sam 8:18; Mit 1:1Yeye hajibu wakati watu waliapo

kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

1335:13 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Ay 15:31; Mit 15:8Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili;

Mwenyezi hayazingatii.

1435:14 Ay 9:11; Yer 11:11Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza

wewe usemapo humwoni,

tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake

na wewe lazima umngojee,

15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu

wala haangalii uovu hata kidogo?

1635:16 Ay 34:35-37; 1Kor 4:20Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana;

anaongea maneno mengi bila maarifa.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

約伯記 35:1-16

1以利戶又說:

2「你在上帝面前自以為義,

你認為這合理嗎?

3你還說,『這與我何干?

我不犯罪又有何益處?』

4我要答覆你和你的朋友。

5要抬頭觀看諸天,

瞻望頭頂的穹蒼。

6你若犯罪,與上帝何妨?

你若罪惡纍纍,對祂有何影響?

7你若為人公義,與祂何益?

祂從你手上能得什麼好處?

8你的罪惡只能傷害你的同類,

你的公義只能令世人受益。

9「人們因飽受壓迫而呼求,

因強權者的壓制而求救。

10但無人問,『創造我的上帝在哪裡?

祂使人夜間歡唱,

11使我們比地上的走獸聰明,

比天上的飛鳥有智慧。』

12他們因惡人的囂張而呼求,

上帝卻不回答。

13上帝必不垂聽虛妄的呼求,

全能者必不理會。

14更何況你說你看不見祂,

你的案子已呈上,在等祂裁決。

15你還說祂沒有發怒降罰,

也毫不理會罪惡。

16約伯啊,你說的盡是虛言,

講了一堆無知的話。」