Elifazi Anasema: Uovu Wa Ayubu Ni Mkubwa
122:1 Ay 4:1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
222:2 Lk 17:10; Za 16:2“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu?
Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
322:3 Isa 1:11; Hag 1:8; Za 143:2; Ay 35:7; Za 9:12Je, Mwenyezi angefurahia nini
kama ungekuwa mwadilifu?
Au je, yeye angepata faida gani
kama njia zako zingekuwa kamilifu?
422:4 Isa 3:14; Eze 20:35“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea
na kuleta mashtaka dhidi yako?
522:5 Ezr 9:13; Ay 11:6; Ezr 9:13; Ay 15:5; 15:13; 20:29; 29:17Je, uovu wako si mkuu?
Dhambi zako si hazina mwisho?
622:6 Kum 24:6, 17; Eze 18:12-16Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu;
umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
722:7 Ay 31:16-17; Eze 18:7; Mt 25:42Hukumpa maji aliyechoka,
nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
822:8 Ay 15:19; Isa 3:3; 5:13; 9:15; Ay 12:19ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi:
mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
922:9 Isa 10:2; Lk 1:53Umewafukuza wajane mikono mitupu
na kuzivunja nguvu za yatima.
1022:10 Ay 18:9; 10:3; 15:21Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote,
hatari ya ghafula inakutia hofu,
1122:11 Ay 5:14; Isa 58:10-11; Mao 3:54ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona,
tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
1222:12 Ay 11:8; 16:19“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu?
Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
1322:13 Eze 9:9; Efe 6:2; Sef 1:12; Za 139:11Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’
Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
1422:14 Ay 26:9; Za 97:2; 105:39; 105:13; 2Fal 21:16; Ay 37:18; Za 18:11; Mit 8:27; Yer 23:23-24Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi
atembeapo juu ya anga la dunia.
1522:15 Mwa 6:11-13Je, utaifuata njia ya zamani,
ambayo watu waovu waliikanyaga?
1622:16 Ay 15:32; Mwa 7:23; Mt 7:26-27Waliondolewa kabla ya wakati wao,
misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
1722:17 Ay 21:15Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi!
Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
1822:18 Ay 12:6; 21:16Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri,
hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
1922:19 Za 64:10; 97:12; Ay 21:3“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi,
nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
2022:20 Ay 15:30‘Hakika adui zetu wameangamizwa,
nao moto umeteketeza mali zao.’
2122:21 Mit 3:10; 1Pet 5:6; Isa 27:5“Mjue sana Mungu ili uwe na amani,
ndipo mema yatakapokujia.
2222:22 Kum 8:3; Ay 6:10; Eze 3:10; Mit 2:6; Za 37:31Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake,
na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
2322:23 Isa 19:22; 44:22; Eze 18:32; Mdo 20:32; Ay 11:14Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya:
Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
2422:24 Isa 2:20; 30:22kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi,
dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
2522:25 2Fal 18:7; Mt 6:20-21ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako,
naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
2622:26 Za 2:8; Isa 61:10Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi,
nawe utamwinulia Mungu uso wako.
2722:27 Ay 5:27; Isa 58:9Utamwomba yeye, naye atakusikia,
nawe utazitimiza nadhiri zako.
2822:28 Za 103:11; 145:19; Ay 33:28; Mit 4:18; Za 97:11Utakusudia jambo nalo litatendeka,
nao mwanga utaangazia njia zako.
2922:29 Za 18:27; 1Pet 5:5Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’
ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
3022:30 2Sam 22:21; Ay 42:7-8Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia,
ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”