Amosi 9 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Amosi 9:1-15

Israeli Kuangamizwa

19:1 Za 68:21; Yer 11:11Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema:

“Piga vichwa vya nguzo

ili vizingiti vitikisike.

Viangushe juu ya vichwa vya watu wote;

na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga.

Hakuna awaye yote atakayekimbia,

hakuna atakayetoroka.

29:2 Za 139:8-10; Ay 20:6; 7:9; Yer 51:33; Oba 1:4; Eze 26:20Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu,

kutoka huko mkono wangu utawatoa.

Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu,

kutoka huko nitawashusha.

39:3 Yer 23:24; 6:16-17; Za 139:8-10; 68:22; Mwa 49:17; Ay 11:20Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli,

huko nitawawinda na kuwakamata.

Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu

katika vilindi vya bahari,

huko nako nitaamuru joka kuwauma.

49:4 Law 26:33; 17:10; Eze 5:12; 15:7; Kum 28:65; Yer 39:16; 21:10; 44:11Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao,

huko nako nitaamuru upanga uwaue.

Nitawakazia macho yangu kwa mabaya

wala si kwa mazuri.”

59:5 Za 46:2; Amo 8:8; Mik 1:4Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka,

na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza:

nayo nchi yote huinuka kama Naili,

kisha hushuka kama mto wa Misri;

69:6 Za 104:1-3, 5-13; Amo 5:8; Yer 43:9yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu

na kuisimika misingi yake juu ya dunia,

yeye aitaye maji ya bahari

na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:

Bwana ndilo jina lake.

79:7 2Nya 12:3; Kum 2:23; Isa 43:3; 22:6; 2Fal 16:9; Yer 47:4; Amo 1:5; Mwa 10:14“Je, Waisraeli,

ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?”

asema Bwana.

“Je, sikuleta Israeli kutoka Misri,

Wafilisti kutoka Kaftori,9:7 Yaani Krete.

na Washamu kutoka Kiri?

89:8 Yer 30:11; 44:27; Za 11:4“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi

yako juu ya ufalme wenye dhambi.

Nami nitauangamiza

kutoka kwenye uso wa dunia:

hata hivyo sitaiangamiza kabisa

nyumba ya Yakobo,”

asema Bwana.

99:9 Lk 22:31; Isa 30:28; Yer 31:36; Dan 9:7“Kwa kuwa nitatoa amri,

na nitaipepeta nyumba ya Israeli

miongoni mwa mataifa yote,

kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo,

na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.

109:10 Yer 5:12; 23:17; 49:37; Eze 20:38; Amo 6:3Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu

watauawa kwa upanga,

wale wote wasemao,

‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’

Kurejezwa Kwa Israeli

119:11 Mdo 15:16; Mik 7:8-11; Zek 12:7; Isa 7:2; 49:8; Mwa 26:22; Eze 17:24“Katika siku ile nitaisimamisha

hema ya Daudi iliyoanguka.

Nitakarabati mahali palipobomoka

na kujenga upya magofu yake,

na kuijenga kama ilivyokuwa awali,

129:12 Hes 24:18; Isa 43:7; Oba 1:19; Yer 25:29; Mdo 15:16-17ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu,

na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,”

asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.

139:13 Law 26:5; Amu 9:27; Yoe 3:18; 2:24; Yer 31:38; 33:14; Rut 2:3“Siku zinakuja,” asema Bwana,

“wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima,

naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu.

Divai mpya itadondoka kutoka milimani,

na kutiririka kutoka vilima vyote.

149:14 Isa 32:18; 49:8; 62:9; 61:4; Eze 34:13-14; Yer 29:14; 33:7; 30:18Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa;

wataijenga tena miji iliyoachwa magofu,

nao wataishi ndani mwake.

Watapanda mizabibu na kunywa divai yake;

watalima bustani na kula matunda yake.

159:15 Kut 15:17; Isa 60:21; 65:9; Yer 18:9; 23:8; 3:18; 24:6; 32:15; Eze 28:26; 34:28; Yoe 3:20Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe,

hawatangʼolewa tena

kutoka nchi ambayo nimewapa,”

asema Bwana Mungu wenu.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

阿摩司書 9:1-15

耶和華的審判

1我看見主站在祭壇旁,祂說:

「你要擊打柱頂,使殿的根基震動;

要打碎它們,使殿宇坍塌壓死眾人。

僥倖生還的,我要用刀劍殺掉,

無人能逃脫,無人能倖免。

2即使他們挖洞鑽進陰間,

我也要把他們揪出來;

即使他們爬上高天,

我也要把他們拉下來;

3即使他們藏在迦密山的峰頂,

我也要去搜尋,捉住他們;

即使他們潛到海底,

我也要派海蛇去吞咬他們;

4即使他們被敵人擄去,

我也要命刀劍追殺他們。

我要定睛在他們身上,

不是要賜福而是要降禍。」

5主——萬軍之耶和華觸摸大地,

大地就消融,地上的人都要哀號;

大地如埃及尼羅河漲起退落。

6那位在天上建造樓閣,

在大地之上立定穹蒼,

召來海水澆在大地上的——

祂的名字是耶和華。

7耶和華說:

以色列人啊,

在我眼中,你們不是和古實人一樣嗎?

我不是領你們出埃及

非利士人出迦斐托9·7 「迦斐托」即克里特島。

亞蘭人出吉珥嗎?

8主耶和華的眼目察看這罪惡的國家,

我要從地上除滅它,

但不會完全毀滅雅各家。

這是耶和華說的。

9「因為我要下令在萬國中篩以色列家,

就像人篩穀物,一粒石子也不會落在地上。

10在我的子民中,

所有誇口說『災禍不會追上我們,也不會迎面而來』的罪人,

都要死在刀下。

以色列的復興

11「到那日,

我要重建大衛已傾覆的棚子,

修補它城牆的缺口。

我要從廢墟中重建它,

恢復它往日的榮耀。

12這樣,以色列人必擁有以東所剩的和所有屬於我名下的國家。

這是要成就這事的耶和華說的。」

13耶和華說:

「時候將到,

五穀還未收完又該耕種了,

葡萄還未踩完又該栽種了。

甜酒從群山上滴下,在丘嶺間流淌。

14我要使我被擄的以色列子民返鄉,

他們要重建廢城並住在城中,

栽種葡萄園,喝園中釀出的美酒,

整理園圃,吃園中出產的佳果。

15我要將以色列人栽種在他們自己的土地上,

他們永不再從我賜給他們的土地上被剷除。」

這是你們的上帝耶和華說的。