Israeli Kuangamizwa
19:1 Za 68:21; Yer 11:11Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema:
“Piga vichwa vya nguzo
ili vizingiti vitikisike.
Viangushe juu ya vichwa vya watu wote;
na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga.
Hakuna awaye yote atakayekimbia,
hakuna atakayetoroka.
29:2 Za 139:8-10; Ay 20:6; 7:9; Yer 51:33; Oba 1:4; Eze 26:20Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu,
kutoka huko mkono wangu utawatoa.
Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu,
kutoka huko nitawashusha.
39:3 Yer 23:24; 6:16-17; Za 139:8-10; 68:22; Mwa 49:17; Ay 11:20Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli,
huko nitawawinda na kuwakamata.
Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu
katika vilindi vya bahari,
huko nako nitaamuru joka kuwauma.
49:4 Law 26:33; 17:10; Eze 5:12; 15:7; Kum 28:65; Yer 39:16; 21:10; 44:11Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao,
huko nako nitaamuru upanga uwaue.
Nitawakazia macho yangu kwa mabaya
wala si kwa mazuri.”
59:5 Za 46:2; Amo 8:8; Mik 1:4Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,
yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka,
na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza:
nayo nchi yote huinuka kama Naili,
kisha hushuka kama mto wa Misri;
69:6 Za 104:1-3, 5-13; Amo 5:8; Yer 43:9yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu
na kuisimika misingi yake juu ya dunia,
yeye aitaye maji ya bahari
na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:
Bwana ndilo jina lake.
79:7 2Nya 12:3; Kum 2:23; Isa 43:3; 22:6; 2Fal 16:9; Yer 47:4; Amo 1:5; Mwa 10:14“Je, Waisraeli,
ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?”
asema Bwana.
“Je, sikuleta Israeli kutoka Misri,
Wafilisti kutoka Kaftori,9:7 Yaani Krete.
na Washamu kutoka Kiri?
89:8 Yer 30:11; 44:27; Za 11:4“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi
yako juu ya ufalme wenye dhambi.
Nami nitauangamiza
kutoka kwenye uso wa dunia:
hata hivyo sitaiangamiza kabisa
nyumba ya Yakobo,”
asema Bwana.
99:9 Lk 22:31; Isa 30:28; Yer 31:36; Dan 9:7“Kwa kuwa nitatoa amri,
na nitaipepeta nyumba ya Israeli
miongoni mwa mataifa yote,
kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo,
na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
109:10 Yer 5:12; 23:17; 49:37; Eze 20:38; Amo 6:3Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu
watauawa kwa upanga,
wale wote wasemao,
‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
Kurejezwa Kwa Israeli
119:11 Mdo 15:16; Mik 7:8-11; Zek 12:7; Isa 7:2; 49:8; Mwa 26:22; Eze 17:24“Katika siku ile nitaisimamisha
hema ya Daudi iliyoanguka.
Nitakarabati mahali palipobomoka
na kujenga upya magofu yake,
na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
129:12 Hes 24:18; Isa 43:7; Oba 1:19; Yer 25:29; Mdo 15:16-17ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu,
na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,”
asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
139:13 Law 26:5; Amu 9:27; Yoe 3:18; 2:24; Yer 31:38; 33:14; Rut 2:3“Siku zinakuja,” asema Bwana,
“wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima,
naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu.
Divai mpya itadondoka kutoka milimani,
na kutiririka kutoka vilima vyote.
149:14 Isa 32:18; 49:8; 62:9; 61:4; Eze 34:13-14; Yer 29:14; 33:7; 30:18Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa;
wataijenga tena miji iliyoachwa magofu,
nao wataishi ndani mwake.
Watapanda mizabibu na kunywa divai yake;
watalima bustani na kula matunda yake.
159:15 Kut 15:17; Isa 60:21; 65:9; Yer 18:9; 23:8; 3:18; 24:6; 32:15; Eze 28:26; 34:28; Yoe 3:20Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe,
hawatangʼolewa tena
kutoka nchi ambayo nimewapa,”
asema Bwana Mungu wenu.
耶和華的審判
1我看見主站在祭壇旁,祂說:
「你要擊打柱頂,使殿的根基震動;
要打碎它們,使殿宇坍塌壓死眾人。
僥倖生還的,我要用刀劍殺掉,
無人能逃脫,無人能倖免。
2即使他們挖洞鑽進陰間,
我也要把他們揪出來;
即使他們爬上高天,
我也要把他們拉下來;
3即使他們藏在迦密山的峰頂,
我也要去搜尋,捉住他們;
即使他們潛到海底,
我也要派海蛇去吞咬他們;
4即使他們被敵人擄去,
我也要命刀劍追殺他們。
我要定睛在他們身上,
不是要賜福而是要降禍。」
5主——萬軍之耶和華觸摸大地,
大地就消融,地上的人都要哀號;
大地如埃及的尼羅河漲起退落。
6那位在天上建造樓閣,
在大地之上立定穹蒼,
召來海水澆在大地上的——
祂的名字是耶和華。
7耶和華說:
「以色列人啊,
在我眼中,你們不是和古實人一樣嗎?
我不是領你們出埃及,
領非利士人出迦斐托9·7 「迦斐托」即克里特島。,
領亞蘭人出吉珥嗎?
8主耶和華的眼目察看這罪惡的國家,
我要從地上除滅它,
但不會完全毀滅雅各家。
這是耶和華說的。
9「因為我要下令在萬國中篩以色列家,
就像人篩穀物,一粒石子也不會落在地上。
10在我的子民中,
所有誇口說『災禍不會追上我們,也不會迎面而來』的罪人,
都要死在刀下。
以色列的復興
11「到那日,
我要重建大衛已傾覆的棚子,
修補它城牆的缺口。
我要從廢墟中重建它,
恢復它往日的榮耀。
12這樣,以色列人必擁有以東所剩的和所有屬於我名下的國家。
這是要成就這事的耶和華說的。」
13耶和華說:
「時候將到,
五穀還未收完又該耕種了,
葡萄還未踩完又該栽種了。
甜酒從群山上滴下,在丘嶺間流淌。
14我要使我被擄的以色列子民返鄉,
他們要重建廢城並住在城中,
栽種葡萄園,喝園中釀出的美酒,
整理園圃,吃園中出產的佳果。
15我要將以色列人栽種在他們自己的土地上,
他們永不再從我賜給他們的土地上被剷除。」
這是你們的上帝耶和華說的。